Walichofanya ni kukopi mfumo wa UK ambapo hakuna mitihani kuanzia primary mpaka secondary form four (but then private sector zao zinazotoa viongozi wa taifa leo na vipanga kwenye nchi ya madaraja; do things differently, mpaka fimbo wanachapa zingine).
Ukirudi kwenye public sector wanafunzi wanapimwa kwa uelewa at each level, ukifika muda wa kufanya mtihani wa form 4 wanafunzi wanakuwa wamewekewa level ya mtihani kutokana na uwezo wao,
kuna mitihani mingine aina A+ hata upate sahihi maswali yote. Sijui kama ni exactly in the end lakini it looks that way, ndio ma-Phd wetu nyenzo si wanafunzi tu pia kwa ma-Prof wao maana hapa kama sio kukosa creativity sijui tuite nini.
Eitherway tuna matatizo makubwa sana kwakuwa kuna ma-Professor ambao tumeshawasikia wakilalama kuhusu haya mambo ya elimu na mitaala huko walipo kwa sasa watakuwa vichwa vinawauma kwa kukosa kuwepo kwenye hii system isiyo eleweka kwa sasa.
Hoja kubwa ya Professor mmoja niliowahi kumsikia kutoka UDSM kitengo cha mafunzo ya elimu ni mitaala inayoendana na changamoto za taifa hili kukidhi skills za wakati tulipo (ina maana si vibaya mitaala ikiwa inafanyiwa review after two to three year).
According to the Prof serikari kwa sasa aija harmonize elimu na uhalisia wa mazingira yetu ya kijamii na uchumi kukidhi changamoto. Mfano kuna faida gani ya kufundisha wanafunzi zaidi ya miatano sociology wakati ajira zenyewe hakuna ni waste of resources; both financial maana wanalipiwa na human capital kwa sababu wakimaliza shule wengi hawana ajira.
Kwa madai yake serikari lazima ijue tunahitaji nini kwenye elimu kwa sasa kwa faida za kuchochea uchumi, mahitaji ya wafanyakazi wa serikari na sector binafsi na wanafunzi walengwe huko. Kama ni degree za uchumi au biashara kwanini nyingi zisilenge kwenye fursa za kilimo kama biashara na mambo mengi yenye ku-reason kutokana na uhalisia wetu wa mambo. Kipi kingemsaidia mwanafunzi kwa leo sociology baada ya kumaliza shule au elimu inayo ona fursa kwenye kilimo kilimo na biashara?
Kuna watu ukiwasikiliza kwakweli wanaona mbali sana, hata ukisoma riport za CAG unajiuliza hawa watu ndio pekee walioilewa F8 auditing module au vipi.
Iweje wakiwa nje wanaona wakiwa ndani wanageuka vipofu, kwa sasa Utoh ni mmoja kati ya watu wanaojua matatizo ya administration ya serikari kuliko watu wengi serikarini mchango wake sijui kama umetumika na watunga sera za elimu hili kufundisha wanafunzi sahihi.
Tuna ombwe la uongozi kwa sasa na maarifa; JK kaifungua serikari tuione kama ilivyo mahala tulipo ni kwa sababu ya watendaji sanasana maafisa wa serikari are unqualified or poor expreinced; lakini wapo wenye uwezo wa kutubadilishia mambo na wenye maoni ya za namna sahihi kwenye kutuongoza na wasomi wenye mawazo mbadala ya kutengenza vijana wenye elimu ya leo na kesho kwa faida ya Tanzania.
Sasa kizungu chenyewe kasheshe, wewe tena ukakifute utegemee wataalamu watakaoweza mudu jargon za lugha kwa miaka mitano ya elimu ya mwisho, hata sijui huwa wanafikiria nini.