Mtihani wa kesho huu hapa!!

Kwa heshima yote Mkuu, Rev. Kishoka, Hilo hapana. Muda wake bado sana. Hata katika nchi zilizoendelea. Labda wakina Shy watoweke ghafla kwenye uso wa dunia.... si wata-hack hiyo email address?!! Washenzi wameweza kumfanyizia Palin, itakuwa email ya mwalimu Mkude shule ya Sekondari Biharamlo?!!... uhakika wa kompyuta yake tu kuwaka kwa umeme wa Richmond nako ni kasheshe..... sembuse kusoma email, kuiweka kwenye thumbdrive, kisha kupanda baiskeli kwenda ku-print pale local stationaries mini market, na kurudi shuleni na lundo la karatasi kwa ajili ya kuwatahini form four...... such a process - si atapigwa kikumbo tu njiani na baiskweli yake ichukuliwe?!!
 
Unajua Elimu ina Gharama yake. Zamani miaka ya 90s kurudi chini mitihani ilikuwa under the control of external invigilators ambao wanakuwa chini ya baraza au afisa elimu wa mkoa. Mtu mmoja kila wilaya mitihani ya saa 8.30 am ilikuwa inasambazwa mashuleni alfajiri yaani 3 hours before, baada ya kuona gharama zimekuwa kubwa baraza wakabadilisha utaratibu na wakuu wa shule kuwa na mitiahani yote mashuleni, matokeo yake ni kwamba mtihani ukivuja huwezi jua nani katoa.

Ninakumbuka miaka ya 90 mwishoni nikiwa pale Kazima Sec Tabora form iV kuna jamaa walipita juu ya dari na kutumbukia ofisini kwa headmaster na kuchukua mitihani. Mungu ibariki ilikuwa ya Mock western zone na jamaa walikamatwa kabla ya kusambaza.

Suala la kudhibiti mitihani hapa ni gumu unless Baraza wakubali kuingia cost na kuicentralise kama zamani, ili mtihani ukivuja tu unajua wa kummbana, na kwa sasa wa kumbana ni maghembe na Mama ndalichako ndio wa kuanza nao.
 


I agree with this problem inakuja cost, hawa jamaa wanachofanya ni kupunguza gharama kwa ku-impair standard. wangelweza kutengeza secured network, na kuagiza high speed printers na kufanya kuwa ni lazima kila shule inunue au hata ikopeshwe kama shart la kusajiliwa na baraza. Tatizo linakuja, Internet, Kama baadhi ya wizara na idara nyeti hazina internet na sometimes updates zinafanyika mara moja kwa mwaka unatarajia nini. Hapa cha kufanya ni kuinvest kwenye elimu na sio siasa kama wanavyofanya watawala wetu.
 
@ Wote wenye kujali..

Hii hoja kuwa mtihani ni uleule tangu miaka ile ya vita vya Idd Amin, nadhani haijakaa vizuri ..kwani Historia hubadilika?

Ndiyo historia inabalika wewe fikiria toka miaka ya Id hadi leo ya mseveni kuna historia ngapi zimetokea?

Nadhani ktk mitihani hiyo kungekuwepo na swali afadhali moja la kuelezea anguko la siasa za Nyerere yani ukominist wa Tanzania.
 
The Kenya national Examinations Council (KNEC) has invested over Shs 268 million to pay field officers who will over see this year's primary and secondary examinations. The money will be used to pay allowances for supervisors, invigilators and security personnel to be stationed countrywide, in a bid to curb exam irregularities. Standard.
 


si lazima kila shule, kila wilaya ikiwa kwenye networks, with good printers hilo linawezekana, kwani mitihani inaweza kupelekwa vituoni some hours before

lakini inwezekana leakageni huko bongo dsm, wakubwa wanafundisha watoto wao mitihani ili wafaulu. kwa hili sasa tuombe turudi mahali mitihani ichapishwe tena uingereza. na je kusambaza mitihani kwa helikopta vipi? haiwezekani? mbona huko tarime ccm wanazo 2 na chadema moja? if you think trainining is expensive try ignorance
 

HAhahaha nimecheka sana mkuu....spare my ribs.....
 
Taarifa zinazotufikia zinadai mtihani uliowekwa hapa ulikuwa sahihi, hatua za haraka zinachukuliwa kubadili mtihani huo na kusambaza nakala haraka iwezekanavyo.

Sikuwa nimeziamini habari hizi hadi nilipopata taarifa hii. Watafanikiwa kuusambaza mtihani huo haraka?
 

Duh Mhe. Prof. J. Magembe na bossi wa NECTA wajiuzuru mara moja ili kuonyesha uungwana.
 

Itakuwa kazi kubwa kuubalisha nchi nzima in less than 20 hours zoezi la ku print na kusambaza ukizingatia miundo mbinu yetu na an uphill task, labda wau akhirishe mpaka baada ya say one week or soo.
 
Itakuwa kazi kubwa kuubalisha nchi nzima in less than 20 hours zoezi la ku print na kusambaza ukizingatia miundo mbinu yetu na an uphill task, labda wau akhirishe mpaka baada ya say one week or soo.
Mkuu Masatu,

Binafsi hili ndilo ninalowaza, itawawia ngumu kuweza kufanikisha kurudufu mitihani hiyo haraka kiasi hicho, wasipobadili basi itawagharimu wengi!
 
Mkuu Masatu,

Binafsi hili ndilo ninalowaza, itawawia ngumu kuweza kufanikisha kurudufu mitihani hiyo haraka kiasi hicho, wasipobadili basi itawagharimu wengi!

Wanakuwa na mitihani tofauti mitatu ambayo inasambazwa yote hadi nadhani ngazi ya mkoa. Kwa hiyo wakiamua kubadili ni kusambaza toka mikoani
 
Wakuu,

Labda tujiridhishe kidogo, kuna njia nyingi wakati wa kusahihisha mitihani zinazosaidia kujua wanafunzi ambao wamefaidika na kuvuja kwa huo mtihani. Kikawaida inatakiwa
wasahishaji waweze kuondoa effects za kuvuja kwa mtihani.

Mara nyingi wanaofaidika na kuvuja kwa mitihani ni wale wanafunzi wenye uwezo mkubwa; aliye nacho huongezewa. Wale wa chini, kuna njia za kuhisi na hivyo kuwashughulikia.

Mimi wakati nafanya mtihani wa form six, paper mbili zilivuja, ambazo hata mimi niliziona. Physics ikaangukia kuwa sio kweli, tulipofungua paper, watu wakaanza kupumua kwa nguvu zote. Ni kwamba watu wakaponzeka. Paper nyingine ilikuwa Chemistry, hii ilitoka kama ilivyovuja.

Matokeo yalipotoka kwa shule husika ilikuwa ni reflection ya uwezo wa watu. Kuna watu walichukua F hata kwenye Chemistry. Siamini hao watu walipata F maana baada ya kuona paper hata kama wali panic bado wangetoka japo na D.

Kwa sisi tuliosoma shule za shamba na kisha kusoma A-level shule za Dar, hilo lilikuwa jambo la kusikitisha sana. Lakini cha kufurahisha, hiyo miaka pamoja na kuvuja mitihani mjini, bado sisi watu wa kule shamba kwenye O-level bado tulikuwa tunatesa.

Ushauri ni kukaa chini na kusoma bila kufikiria kuna watu wanaweza kupata mtihani.
 

Pengine ni wakati sasa kuisambaza ile email niliyomwandikia Katibu Mtendaji wa NECTA, ili wengine pia waione wajue alionywa. Wenzangu huko tusaidiane kumsuta, tumwandikie email nyingi za kumtaka awajibike. Anwani yake esnecta@necta.go.tz.
 
Pengine ni wakati sasa kuisambaza ile email niliyomwandikia Katibu Mtendaji wa NECTA, ili wengine pia waione wajue alionywa. Wenzangu huko tusaidiane kumsuta, tumwandikie email nyingi za kumtaka awajibike. Anwani yake esnecta@necta.go.tz.

Mkuu wazo zuri tutajaza inbox yake na wengine huwa na filter huenda zikaishia kwenye spams....pia kumwandikia mail ni kureveal ids zetu!!! nasita kumtwangia mail.
 
Mkuu wazo zuri tutajaza inbox yake na wengine huwa na filter huenda zikaishia kwenye spams....pia kumwandikia mail ni kureveal ids zetu!!! nasita kumtwangia mail.

Mimi simwogopi bana, nimemtwangia tu! Hata hivyo tunazo njia nyingi za kushinikiza, tuzitumie pia.
 
Mkuu wazo zuri tutajaza inbox yake na wengine huwa na filter huenda zikaishia kwenye spams....pia kumwandikia mail ni kureveal ids zetu!!! nasita kumtwangia mail.
Ushi,

Hapo ndipo utaona kuwa dhamira ya sisi (JF) kuwapa anuani pepe kupitia JF tulijua kuna issues kama hizi. Ungekuwa na ushirombo@jamiiforums.com ingekuwa rahisi kwako kutuma barua pepe kwa wakuu hawa.

Got me?
 

Kigarama pls i need the front page immediately if posibo.

I will make it sent to those who want to make us believe that there is no more exams leakage.

waiting
 
Last edited:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…