"Mtoto anapobakwa nakupewa ARV?

"Mtoto anapobakwa nakupewa ARV?

Amavubi

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2010
Posts
30,156
Reaction score
13,258
Nimesikiliza kwa masikio yangu kupitia ITV Dr wa Mwanyamala Hospt akisema hayo leo usiku

Naomba wataalamu mnifafanulie hili
 
Umeambiwa ili kuzuia maambukizo ambayo anaweza pata mtoto. Hii inakuwa kama kinga kwake.

asante................kuna hoja fulani naitafuta maana njia za kujua ni mcili, kuuliza au kubisha
 
Inaitwa PEP yaani Post Exposure Prophylaxis.Ni mchanganyiko wa dawa za ART ambazo hupewa mtu(si lazima awe mtoto tu) katika kipindi kisichozidi saa 72 baada ya kitendo chochote kinachomweka kwenye hatari ya kuambukizwa HIV mf kubakwa ama kunajisiwa,kwa madaktari kujichoma bahati mbaya na sindano ama kitu chenye ncha kali viliyotumika kumhudumia mwathirika ama mgonjwa unayemhudumia.Ukiona mtoto kanajisiwa ama kabakwa muwahishe hospitali ya serikali akapate huduma hiyo upesi ndani ya saa 72.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Sio mtoto tu...ukibakwa especially kwenye nchi zetu hizi kuna uwezekano wa kuambukizwa magonjwa ya zinaa ukimwi ukiwa mmojawapo!
Utaratibu ni kwamba utafanyiwa vipimo vya haraka vya ugonjwa wa zinaa ...kama unao utahitaji tiba na kama hauna utatakiwa kupewa kinga!
Mojawapo ya kinga ni madawa ya ARV ...tunaita PEP(post exposure prophylaxisis) kama alivyosema mdau hapo juu.
 
ARV atapewa kama CD4 zake tayari zimeshuka sana mwilini mara baada tu ya kumaliza kubakwa!

Usiongee kitu usichokijua mkuu utakuwa unapotosha jamii.Si vizuri ingawa unachosema ni kweli kwa mtu aliyebakwa akiwa tayari alikwishaathirika.Huyu hatapewa PEP isipokuwa atatibiwa tu magonjwa mengine kama yapo na kuhusu ARV atatumia wakati muafaka CD4 zitakaposhuka chini.Kwa mtu ambaye hakuwa na HIV halafu akabakwa hupewa hizo ARV kama kinga kama nilivyoeleza hapo juu.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
asanteni sana nadhani nilikua zuzu kutofautisha PEP na ARVs
 
Inaitwa PEP yaani Post Exposure Prophylaxis.Ni mchanganyiko wa dawa za ART ambazo hupewa mtu(si lazima awe mtoto tu) katika kipindi kisichozidi saa 72 baada ya kitendo chochote kinachomweka kwenye hatari ya kuambukizwa HIV mf kubakwa ama kunajisiwa,kwa madaktari kujichoma bahati mbaya na sindano ama kitu chenye ncha kali viliyotumika kumhudumia mwathirika ama mgonjwa unayemhudumia.Ukiona mtoto kanajisiwa ama kabakwa muwahishe hospitali ya serikali akapate huduma hiyo upesi ndani ya saa 72.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums

Sio mtoto tu...ukibakwa especially kwenye nchi zetu hizi kuna uwezekano wa kuambukizwa magonjwa ya zinaa ukimwi ukiwa mmojawapo!
Utaratibu ni kwamba utafanyiwa vipimo vya haraka vya ugonjwa wa zinaa ...kama unao utahitaji tiba na kama hauna utatakiwa kupewa kinga!
Mojawapo ya kinga ni madawa ya ARV ...tunaita PEP(post exposure prophylaxisis) kama alivyosema mdau hapo juu.

Usiongee kitu usichokijua mkuu utakuwa unapotosha jamii.Si vizuri ingawa unachosema ni kweli kwa mtu aliyebakwa akiwa tayari alikwishaathirika.Huyu hatapewa PEP isipokuwa atatibiwa tu magonjwa mengine kama yapo na kuhusu ARV atatumia wakati muafaka CD4 zitakaposhuka chini.Kwa mtu ambaye hakuwa na HIV halafu akabakwa hupewa hizo ARV kama kinga kama nilivyoeleza hapo juu.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
nawashukuru sana kwa somo, kama nilivyosema hapo awali njia za kujifunza ni adha kuuliza sana au kujifanya UNABISHA ili uendelee kupata nondo
 
Back
Top Bottom