Mtoto apendi kula, je mbinu gani itumike apende kula?

kama haya unayosema ni kweli
Nitafute PM Mkuu
Kuna Unga ambao mtoto akipata uji wake siku moja, ya pili anakula kama kawaida,
ni tatizo la kawaida
Nipem namba
Unga ni TZS 5000 kilo moja
Habari, na mimi Naweza kupata huo unga plz mtoto anasumbua sana kula, 0754610880 namba yangu. Asante.
 
Ni mtoto wa kiume, ndio anatimiza mwaka mmoja. Hapendi kula, licha ya kumbadilishia chakula mara kwa mara. Mama yake humlazimisha kula angalao vijiko viwili.
mwekee sahani moja na watoto wenzie
 
Mpe uji wa unga wa viazi vitamu na ulezi...ataanza kula mpaka ukimbie. Kanunue supermaket yoyote. Ukikosa nitafute nikupe pakti 2 au 3 umtest.
 
Kwel kabsa sidhan kama kuna mtoto anaepend kula ktk umri huo,,,cha muhim ni kumlisha kwa nguv tu angalau asishinde njaa,,,ukimwonea hurum itakula kwko
 
1.Bado ananyonya?
2. Amewai kula dawa za minyoo?
3. Anabadilishiwa vyakula?
4. Anamkatalia kila MTU au mama yake tu

Nikipata hayo majibu,ntakushauri vizuri
 
Ni mtoto wa kiume, ndio anatimiza mwaka mmoja. Hapendi kula, licha ya kumbadilishia chakula mara kwa mara. Mama yake humlazimisha kula angalao vijiko viwili.
Dawa ya watoto wanaokataa kula!

Mdau mmoja ameomba ushauri kwa mtoto asiependa kula, matatizo ya mtoto kutopenda kula ni mengi yanaweza kusababishwa na tabia binafsi au maradhi. Kama mtoto yuko salama hana maradhiila hapendi tu kula kazi ni ndogo sana kumbadilisha ili apende kula.

Inawezekana unandaa chakula safi sana lakini bado mtoto anasumbua kula ili kumbadilisha tabia apende kula unatakiwa kumtengenezea kwanza hamu ya kula maana bila ya kuwa na hamu ya kula hata chakula kiwe kizuri vipi huwezi kula vizuri.

Hamu ya kula inatakiwa kuanzia asubuhi unapofungua kinywa, tengeneza chai iwe ya rangi au ya maziwa weka tangawizi ya unga kwenye nusu lita ya maji au maziwa weka tangawizi kijiko kidogo cha chai mzoweshe mwanao chai hii kila siku asubuhi tangawizi ni kiungo kizuri kinachosaidia kumengenya chakula tumboni na kusababisha njaa haraka na hamu ya kula.

Hapo utakua umemtengenezea mtoto hamu ya kula mchana, kwa kumuandalia mtoto hamu ya kula chakula cha usiku tengeneza juisi ya Pasheni au Embe au Nanasi au tunda lolote lile kumbuka kuchanganya tena kijiko kidogo cha chai kilicho jaa tangawizi na usage pamoja na mchanyanyiko wako mpe mtoto glasi moja saafi kabla ya kula na mabadiliko utayaona usimpatie baada ya kula maana itamsababishia njaa.
 
Mpeleke uswazi akae wiki mbili alafu umrudishe kwako atakula tu bila kutumia dawa
 
Ni mtoto wa kiume, ndio anatimiza mwaka mmoja. Hapendi kula, licha ya kumbadilishia chakula mara kwa mara. Mama yake humlazimisha kula angalao vijiko viwili.


Pengine kakasirika kwa nini kasingiziwa baba anayeishi naye wakati baba yake mzazi yuko kwingine. Watoto bwana, wana hisia kali ila bahati mbaya tu twawadharau.
 
Mtoto chakula chake maziwa, mwache anyonye muda ukifika, atakula tuu !! Mate ya mtoto ni mepesi na chakula chake kinatakiwa kiwe chepesi pia, Sasa wewe unampa dona na dagaa chakula ambacho hata wewe unakula kwa kujilazimisha, Terrible !!
 
Mwanangu pia napenda kunyonya tuuu na kula samaki na maziwa mtindi. Vingine hataki
 
Ila kama mzazi tumia kila njia
-kukaba
-kuimba nyimbo (za chekechea zile)
- kumuacha acheze, unakuwa unamfuata alipo unamlisha kijiko, then akimeza unamfuata tena
-kumlishia nje anakuwa anashangaa shangaa vindege, miti, kunguru
Njia ya kukaba watoto sio sahihi, mtoto atajenga picha mbaya kuhusu kula, ukifika muda wa kula tu ataanza kulia.
 
Weeee tumekabwa toka enzi hizo unafurukuta afu unatulia, na chakula unamaliza. .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…