Mtoto Bahati Cornel wa Umbwe primary school amepotea. Yupo Polisi Kawe

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Mtoto Bahati S/o CORNEL, Mchaga, 8 yrs old, M/Funzi Umbwe primary school, Darasa la tano.

Mtoto huyu yupo hapa police Kawe ambapo alijieleza kuwa amepotea, alikuja jijini DSM akitokea mkoani Kilimanjaro ambako ndiko anakoishi na Baba yake Mzazi aitwae CORNEL JOSEPH MASAWE, ambae anafanya kazi Kiwanda cha COTEX UMBWE.

Mtoto huyo alifika DSM tarehe 05/07/2020 kwa gari za kudandia, tunaomba taarifa hizi zisambazwe kwenye groups zingine kwa msaada zaidi.

 
Bila shaka dogo alichoka kusubiri maana anaona wenzie wanakuja December kula sikukuu wanampa mastori ya mjini halafu January wanasepa wanamwacha peke yake.

Kila dogo mkoani anaiota Dar es salaam. Ila labda kwa akili yake ya kitoto kalidhani kakifika Dar ni maisha mazuri masikini!
 
Kamanda anaanza ubaharia wa nchi kavu akiwa na miaka 8 je akifka 25 itakuwaje nadhan hawa ndio wale yule msanii aliimba MBONGO BAHATI MBAYA
 
Dogo anajua mpaka baba anapofanyia kazi? Huyo hajapotea amekuja kubadilisha menu. Amechoka ndizi maharage Kila uchao
 
Miaka 8 yupo darasa la tano naona alianza la kwanza na miaka mitatu sisi tulichelewa sana kuanza shule!
 
Kwa huo ubaharia aliokuwa nao alipaswa awe Chuo kikuu..[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…