Mtoto katika ndoa hudumisha mahusiano?

Mtoto katika ndoa hudumisha mahusiano?

.Je ni kweli kwamba mkipata mtoto huifanya ndoa yenu iwe imara zaidi? Mi binafsi nachukulia kama mipango ya Mungu tu, labda watafanikiwa mbele ya safari.

Ndugu yangu, nakubaliana na wewe ya kuwa kupata mtoto wako binafsi ni mipango ya Mungu, Ukiacha wale wanaoharibu kizazi kwa kutoa mimba wakati wa ujana halafu baadaye wanatafuta mtoto na kukosa.

Furaha ya mtoto inakujaje? Ukiwa na akili timamu ambayo haijaharibiwa na kilevi mtoto au watoto watakukumbusha daima ya kuwa upende au usipende baba na mama mnawajibika kwa 100% kwa wao kupumua na kuona jua kesho yake. Hivyo basi.. ukiweza kutimiza wajibu huu kwa uwezo wako..unajisikia ufahari.. na moyo wako unakuwa na amani kwani unaona umesaidia malaika wasio na mbele wa nyuma. Kwa upande mwingine kwa sababu watoto ni zao la watu wawili..wanaonekana kama daraja la muunganiko wa mahusiano..

Kuhusu furaha hii kama inawezekana kupatikana kutokana na mtoto wa ku-adopt.. hili linategemea na saikolojia ya wazazi wote wawili na mazingira.. Kama nilivyosema..kama furaha yenu itakuja kwa kujiona ufahari ya kuwa kuna kiumbe kinawategemea kwa asilimia 100% kuona jua ..basi mtakuwa na furaha hata kama mta-adopt mtoto, lakini kama mnashindwa kundoa mawazo ya kuwa hakuna tofauti kati ya biological child na yule wa asili yenu..basi hamtaweza pata hiyo furaha.

..Lakini ukweli utabaki mtoto ni mtoto..kwani ni malaika anayetegemea mtu mwingine iwe yule aliyemleta au yule aliye m - adopt.
 
watoto wana raha yake kwa kweli,kuna siku mtoto wangu wa miezi kadhaa aliniona nikilia huku nimempakata baada ya baba yake kuniudhi sana(nilishindwa kujizuia kulia japokuwa nilikuwa nimebeba mtoto) akaniangaliaaaaa.......then akachukua kitambaa nilichokuwa nimemshikia akanipangusa machozi daaaah yani nilihisi furaha ya ajabu na nikaacha kulia nikamshangaa Mungu!! watoto wanaleta furaha kwenye ndoa.

Acha uongo wewe, miezi mingapi?
 
Nina jamaa zangu wawili ambao wako kwenye ndoa, mmoja ni zaidi ya miaka tisa,lakini hawajafanikiwa kupata mtoto.Japo hawasemi lakini kwa kuwatazama na jinsi watu wanavyonong'ona penbeni inaonyesha kabisa hawako happy kwenye ndoa zao.Je ni kweli kwamba mkipata mtoto huifanya ndoa yenu iwe imara zaidi?Mi binafsi nachukulia kama mipango ya Mungu tu, labda watafanikiwa mbele ya safari.

...hapo penye wekundu ndipo penye kuletesha matatizo. Madhali wenyewe wamekubaliana na hiyo hali, wajibu wenu ndugu jamaa na marafiki ni kukubaliana na hali ilivyo. Miaka tisa mingi, japo si mingi kihivyo.

Mtoto ni majaaliwa. Naamini kina mama wengi walioshindwa kupata watoto wanatamani sana angalau siku moja nao wangeitwa mama. Kina baba wenye shida hiyo nao wanateseka vile vile. La msingi ni kumshukuru mungu kwa majaaliwa yake. Iwapo wao wana lengo, nia na madhumuni,...Options bado zipo nyingi sana za kufanikisha zoezi zima la kupata mtoto ikiwamo IVF hata kama tatizo ni la mwanaume, [Azoospermia]

Tukumbuke pia, wapo wale kina mama wanaobeba mimba lakini zinaharibika kabla ya muda kutimia. Adoption pia inakubalika.
Mtoto ni majaaliwa.
 
...hapo penye wekundu ndipo penye kuletesha matatizo. Madhali wenyewe wamekubaliana na hiyo hali, wajibu wenu ndugu jamaa na marafiki ni kukubaliana na hali ilivyo. Miaka tisa mingi, japo si mingi kihivyo.

Mtoto ni majaaliwa. Naamini kina mama wengi walioshindwa kupata watoto wanatamani sana angalau siku moja nao wangeitwa mama. Kina baba wenye shida hiyo nao wanateseka vile vile. La msingi ni kumshukuru mungu kwa majaaliwa yake. Iwapo wao wana lengo, nia na madhumuni,...Options bado zipo nyingi sana za kufanikisha zoezi zima la kupata mtoto ikiwamo IVF hata kama tatizo ni la mwanaume, [Azoospermia]

Tukumbuke pia, wapo wale kina mama wanaobeba mimba lakini zinaharibika kabla ya muda kutimia. Adoption pia inakubalika.
Mtoto ni majaaliwa.
Tatizo jingine kwa kweli ni familia na jamii nayo hupenda sana kukuza na kufuatilia mambo ya wanandoa.
 
Tatizo jingine kwa kweli ni familia na jamii nayo hupenda sana kukuza na kufuatilia mambo ya wanandoa.

...ndilo nilogusia hapo.

Wengine hufikia hatua ya kumbughudhi mke kwanini hazai, anakula bure na blah blah nyingine. Wengine humshinikiza kaka mtu aoe mwanamke mwingine...sasa kama tatizo ni la mwanaume, ndio hapo utapokuta Mzee Mzima anaadhirika. Inambidi naye ili kuficha aibu, wengine wanafikia hata makubaliano mkewe azae na mwanaume mwingine, wengine hujitia sababu za kujiua nk...

Kama wapendana kiukweli na mkeo, Inabidi kushindilia vigunzi masikioni na kutowasikiliza watu hawa.
 
Kwa kweli mtoto huleta faraja ndani ya family, ila ukikosa usilalamike sana
huwezi jua kwa nini Mungu amefanya iwe hivyo, ila pia shafiq anajitahidi sana
pale agha khan
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Kwa kweli mtoto huleta faraja ndani ya family, ila ukikosa usilalamike sana
huwezi jua kwa nini Mungu amefanya iwe hivyo, ila pia shafiq anajitahidi sana
pale agha khan
Nice stuff Shantel.Japo ni ngumu kumeza ikikukuta.
 
Back
Top Bottom