Mtoto mchanga kulia sana usiku wa manane

Mtoto mchanga kulia sana usiku wa manane

Labda mtoto hashibi, niliwahi kumuona mama mmoja akihojiwa kuhusu mtoto wake aliyekuwa anasumbua sana usiku wa manane kwa kulia hata masaa mawili/matatu akahangaika huku na kule kwa madaktari bila ahueni yoyote mpaka alipokutana na daktari aliyemwambia huyu mtoto kote ulikopita hawakuona tatizo la kiafya mchana anashinda vizuri kabisa usiku wa manane ndiyo anaangusha kilio. daktari akasema labda mtoto hashibi jaribu kuhakikisha mtoto anashiba na labda maziwa yako hayamtoshi hivyo alimshauri anunue maziwa ya kopo. Yule mama akadai baada ya kuanza kumpa mtoto maziwa ya kopo pamoja na ya kwake kulia usiku wa manane kukafikia ukomo.
Ni kweli kabisa mkuu, my son alikuwa na tatizo hili likatutesa sana, bt baadae ikaja gundulika maziwa ya mama yake hayatoshi na kijeba hakishibi. Lactogen ikasolve tatizo.
 
Mkuu Jerry zingatia yote uliyoambiwa ila tambua kuwa kwa kipindi cha miezi 3 ya mwanzo ya mtoto kulia ni kawaida kutokana na mijongoo ya ukuaji wake.
Ila makesure unamlisha anashiba na kumchek nepi kama amekojoa, tafadhali usimvishe pampus nyingine sio nzuri zinawaumiza mvishe nepi nene kwa nje na laini ndani.
Ishu ya mapepo ipo sasa wewe kama mkristo makesure unamtolea sadaka ya ukombozi kanisani na kumwombea sana.
 
Mkuu Jerrymsigwa, pole sana kwako na kwa mama mtoto na mtoto pia kwa hali hiyo. Binafsi ilinikuta na nilikuwa na umia sana, sasa hapo kuna jambo moja tu huwa ndiyo tatizo, mtoto atakuwa anasumbuliwa na gesi za tumboni, yaweza kuwa mama haweki chuchu yake vizur mdomoni mwa mtoto wakati wa kunyonya hivyo anakuwa na gesi tumboni, pia kila akimaliza kunyonya ajitahidi kuhakikisha mtoto anabeua kwa kumbeba wima akimuweka begani mwake mara baada ya kunyonya, amrushe rushe kidogo ili kutoa gesi tumboni, yaani hilo ndiyo tatizo kuu. Ukiwa mtu imani haba waweza fikiri mtoto kalogwa, lakini si hivyo.jaribu hii halafu nipe mrejesho hapa.
 
Pia Grip water nyingi ni fake siku hizi, hivyo nashauri wazazi ni bora kumpatia hata maji yenye uvuguvugu tu kuliko hayo ma chemicals
 
Tatizo lililoko hapa kinacho sumbua ni tumbo mfumo wake wa chakula unakuwa haujazoea kujiendesha wenyewe tofaut na alipo kuwa tumboni anatengenezewa tu.
Kwahiyo hapo ndo shuguli huanza asa tumbo humuuma na kulia sana
 
Back
Top Bottom