Gang Chomba
JF-Expert Member
- Feb 29, 2008
- 20,649
- 4,786
Kwenye riadha huko Duniani miaka ilee palipata kutokea Mwamba alieitwa Tim Montigomery raia wa Marekani.
Siku Moja Tim alikimbiza upepo huku akisindikizwa na makelele ya wapenzi watazamaji wa Mchezo huo wengi wao wakiwa wamarekani wenzie na kufanikiwa kuwa bingwa wa mita 100.
Wakati hayo yakijiri upande wa pili kwa akina Dada nako mrembo Marion Jones nae alifanikiwa kuubalasa upepo na kuwa bingwa wa mita 100.
Wawili hawa sasa wakafanikiwa kuwa Binadamu wenye kasi zaidi Duniani.
Lakini wakaenda mbali na kufanikiwa kufunga ndoa na kisha wakapata Mtoto.
Nakumbuka katika kipindi cha Michezo cha television ya CNN kilicho kuwa kikiongozwa na Mreno Pedro Pinto, katika kipengele cha Play of the Day aliweka Video mbili tofauti za wawili hao kila mmoja akiwa anachukua ubingwa kisha mwisho akamaliza kwa kusema Mtoto mwenye mbio zaidi Duniani amezaliwa.
Siku Moja Tim alikimbiza upepo huku akisindikizwa na makelele ya wapenzi watazamaji wa Mchezo huo wengi wao wakiwa wamarekani wenzie na kufanikiwa kuwa bingwa wa mita 100.
Wakati hayo yakijiri upande wa pili kwa akina Dada nako mrembo Marion Jones nae alifanikiwa kuubalasa upepo na kuwa bingwa wa mita 100.
Wawili hawa sasa wakafanikiwa kuwa Binadamu wenye kasi zaidi Duniani.
Lakini wakaenda mbali na kufanikiwa kufunga ndoa na kisha wakapata Mtoto.
Nakumbuka katika kipindi cha Michezo cha television ya CNN kilicho kuwa kikiongozwa na Mreno Pedro Pinto, katika kipengele cha Play of the Day aliweka Video mbili tofauti za wawili hao kila mmoja akiwa anachukua ubingwa kisha mwisho akamaliza kwa kusema Mtoto mwenye mbio zaidi Duniani amezaliwa.