Mtoto wa Diamond Platnumz awa mtoto wa kwanza Africa kufikisha followers milioni moja Instagram

Laah!!

hii kweli Tanzania,
(Ninachowaza Mimi sio kama wengine wameshindwa (wazazi mastaa wenye watoto) ila huenda hawajawekeza akili na maarifa yao yote kwaajili ya akaunti za Instagram kwa watoto wao).

Najuwa utabisha ila jiulize;
.
huyo tifa mwenye follower wengi anaweza kupost chochote Instagram?

Hivyo basi tambua wazazi wake maarifa na akili zao zote wamewekeza huko,hata wewe ukitaka unaweza ila kuna mengi mazuri na bora zaidi ya kupigania kwaajili ya mwanao hasa wa kike kuliko kumjazia followers Instagram..
 
Hongera Sana Mtoto kwa kufikisha followers milioni 1 hakika ni mafanikio makubwa sana kwa Africa.
 
Hongera Sana Mtoto kwa kufikisha followers milioni 1 hakika ni mafanikio makubwa sana kwa Africa.
Haha [emoji1] [emoji1] [emoji1]

"Eti mafanikio makubwa kwa afrika"

Hivi ni kweli??

Wewe umenufaika na nini labda tuanzie hapo??
 
Mtoto halelewi instagram hadi iwe sifa kuwa na followers wengi, matokeo yake watu wanamtukana wanamnanga kwa kila aina ya matusi yanini sasa! Muda mwingine mambo yetu ya kikubwa tusiwashirikishe watoto kwa maana hayatokua na manufaa kwao
 
Ally7.
wewe ndio uliehitimisha mjadala, mimi na wezangu tuliokuwa na naniya ya kuchangia, hatutokua na jipya
 
Kufikisha kwake follower 1m taifa limenufaika kwa kuingiza 1.2trilion! Na zote zimeingizwa kwenye ujenzi wa taifa
 
Ally7.
wewe ndio uliehitimisha mjadala, mimi na wezangu tuliokuwa na naniya ya kuchangia, hatutokua na jipya
Mawazo yatakayo kuja baada ya comment ya Ally7 ni majungu mjadala tayari umeshafungwa
 
Mafanikio makubwa sana kwa Tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…