wajukuu zangu babu yenu nimerudi. kwanza nipeni pole kwa maradhi ya uzee yaliyonipata maana imekuwa tabu kila ninaposikia mambo hayaendi vizuri kwa kuwa ENZI ZA MWALIMU................watu walikuwa hawasemi sana tofauti na siku hizi. wenyewe mnaita demokrasia. na kwa kuwa pumzi nimejaaliwa ngoja nami niseme.
katika nchi yetu ambayo demokrasia inazidi kukuwa kuna mambo ambayo nadhani haywezi epukika.lakini pia, mtakubaliana nami kuwa katika jamii ambayo maisha yake ni ya ufugaji uhodari wa mtoto upimwa kwa .......................
labda kidogo niwaeleze jinsi nilivyomfahamu jakaya na familia yake yote.
mzee mrisho kikwete alikuwa ni kiongozi wa kabila la wakwere na kwa nafasi yake hiyo waingereza walimpa nafasi ya kuwa bwana muamua mashtaka na mambo yote yanayotokea katika eneo hilo. ni ukweli kuwa utawala wake ulienziwa sana na kwa nyakati tofauti amekuwa nguzo kubwa sana katika kuimarisha na kuwaamsha watanzani juu ya kugombania haki zao na hasa nazungumzia haki zao ambazo ni za msingi sana (chief marealle,1998).nimeweka kumbukumbuku ili nikukumbusheni maneno ya mtawala huyu wa kichaga , ambaye katika nyakati fulani amekuwa akikutana na mwenzake huyu katika vikao mbalimbali na hivi ndivyo alivyomfahamu.anaendelea kuwa picha anazo na kwa wale watako itaji kumbukumbu wawaone wahusika watazipata.bwana mrisho kikwete ni babu wa mheshimiwa raisi wetu.
khalfan kikwete snr ni baba wa mh.raisi wetu. huyu naye kwa nafasi yake katika nyakati tofauti alifuata nyayo za baba yake. naye alikuwa mtawala katika eneo hilo la ukwere. alifanya kazi zake na hata wakoloni walimuona anafaa na akachaguliwa katika nafasi mbalimbali za kiutawala kipindi hicho. kwa nafasi zake amewahi kuhudumia jamii katika maeneo mbalimbali kama same,lushoto na hata baadae kuja kustaafu huko bagamoyo kwao.
ninajaribu kuonyesha hapa ni kwamba hili suala la siasa na uongozi ndani ya fanilia hii halikuanza leo. ni jambao la siku nyingi na kama hauamini basi angalia hapa.baada ya bwana khalfan snr akaja jakaya kikwete. huyu mwanangu ameshika nafasi nyingi sana za kiuongozi hadi leo. nazungumzia kutoka ukatibu wa chama hadi uraisi. kwa wale wanamfahamu mwanye ridhiwani ni kwamba yeye naye alianzia kama wakuu wake hawa. yeye amekuwa katika chipukizi na hata sasa vijana.
wenzake watakumbuka wakati yupo shule ya msingi na kumbukumbu zinatuonyesha kuwa alikuwa mcheza gwaride na baadae kiongozi wa chipukizi shuleni kwao. sio kiongozi wa kupewa bali alifanya kampeni na wenzake wakamuamini na kumpa nafsi hiyo.
sasa ni nini cha kushangaza kwa khalfan jr kuwa kiongozi ndani ya chipukizi, wajukuuu zangu. ni nini kinachowakwaza hadi mnaona msokoto ndani ya roho zenu. msifanye hivyo.
yawezekana hawa wanangu wamelewa au wanaugua siasa lakini kwangu mimi nashauri nasi tufuate nyayo hizi. viongozi wazuri ni wale wanaolelelwa katika mfumo mzuri. maana nataka kuamini kuwa moja ya matatizo makubwa yanayotukabili leo ni lundo la viongozi ambao hawakijui chama wala hata msingi wa nchi.
watu wameruka kutoka kusiko juliakana wakapewa madaraka makubwa. sasa baada ya kusaidia siasa ya chama kwa kuwasaidia wananchio wao wananeemesha matumbo yao. lakini kwa kijana kama khalfan jr. ni imani yangu kuwa akilelewa vizuri akaelekezwa juu ya nini mambo yanakuwa na jinsi gani yanaendeshwa atakuwa kiongozi mzuri sana. hapa simzungumzii yeye peke yake , nazungumzia yeye na chipukizi wenzake.
nashangaa wajukuu zangu wengine mnaandika humu ndani hata kanuni ya chipukizi hamuijui. kuna mtu anadai huyu ni mtoto hata uendeshaji haujui...........ahahahahaha angalia vizuri utaratibu waliowekeana chipukizi wa ccm. utaratibu umeeleza umri gani mtu anatakiwa kuwa kiongozi.
ni ukweli usiofichika kwamba mfumo mzuri walionao unaweza wasaidia. huu ni umri wa kujifunza na kuwafanya watambue na kwamba wanapoingia kwenye umri wa ujana wawe ni watu wa kufanya kazi tu.
nafikiri umenielewa ngoja nilale kidogo maana mikono inaniuma.