Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Katika uzi wangu uliopita niliuliza wazazi wapo kundi gani kwenye malezi ya watoto na digitali, kama wataruhusu watoto kutumia simu kwa kuwapo mwongozo au kuwa wakoloni na kuacha wakikua mpaka chuo ndio watumie simu.
Nilishangazwa na baadhi ya majibu wakisema kwa mtoto wa kiume haina tabu ila kwa wakike ni mpaka afike chuo ndio atapewa simu.
Dhana hii imejengeka wapi? Ni kweli mtoto wa kike hawezi kujisimamia akiwa na mwongozo mzuri? Ni kweli hawezi kufanya maamuzi mazuri kama ilivyo mtoto wa kiume?
Kama bado tunawatenga toka wakiwa wadogo bado tunategemea wakue wakiwa wanajiamini na kuwa uwezo sawa na wa kiume ambao waliwekewa mazingira mazuri toka wakiwa wadogo?
Nini hasa kinatutisha mpaka tunashindwa kuwa walezi wazuri wa kuonesha njia kwa watoto wakike?
Katika uzi wangu uliopita niliuliza wazazi wapo kundi gani kwenye malezi ya watoto na digitali, kama wataruhusu watoto kutumia simu kwa kuwapo mwongozo au kuwa wakoloni na kuacha wakikua mpaka chuo ndio watumie simu.
Nilishangazwa na baadhi ya majibu wakisema kwa mtoto wa kiume haina tabu ila kwa wakike ni mpaka afike chuo ndio atapewa simu.
Dhana hii imejengeka wapi? Ni kweli mtoto wa kike hawezi kujisimamia akiwa na mwongozo mzuri? Ni kweli hawezi kufanya maamuzi mazuri kama ilivyo mtoto wa kiume?
Kama bado tunawatenga toka wakiwa wadogo bado tunategemea wakue wakiwa wanajiamini na kuwa uwezo sawa na wa kiume ambao waliwekewa mazingira mazuri toka wakiwa wadogo?
Nini hasa kinatutisha mpaka tunashindwa kuwa walezi wazuri wa kuonesha njia kwa watoto wakike?