Mtoto wa Zidane, Enzo astaafu soka akiwa na Umri wa miaka 29

Mtoto wa Zidane, Enzo astaafu soka akiwa na Umri wa miaka 29

Last Seen

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2013
Posts
229
Reaction score
566
Enzo Zidane, mtoto wa Zinedine Zidane, ameamua kustaafu soka akiwa na umri wa miaka 29. Enzo aliwahi kuchezea klabu ya Real Madrid na vilabu vingine, lakini sasa ameamua kustaafu soka.

Enzo Zidane alianza safari yake ya soka akiwa bado kijana mdogo, akifuata nyayo za baba yake Zinedine Zidane. Enzo alijiunga na academy ya Real Madrid, maarufu kama "La Fabrica", ambapo alifanikiwa kuonesha kipaji chake na kujitengenezea jina lake mwenyewe. Ingawa alikabiliwa na shinikizo kubwa kutokana na ukubwa wa jina la familia yake (Zidane), Enzo aliweza kuonyesha uwezo wake uwanjani.

Baada ya muda akiwa kwenye academy ya Real Madrid, Enzo alipandishwa hadi timu ya wakubwa ya Real Madrid, lakini nafasi yake ya kucheza katika kikosi hicho ilikuwa finyu kutokana na ushindani mkali ndani ya timu hiyo. Hii ilimfanya Enzo kutafuta fursa za kucheza katika vilabu vingine, aliamua kutimkia klabu Deportivo Alavés kwa mkopo. Huko, alijaribu kupata muda na nafasi ya kucheza zaidi na kuonyesha uwezo wake.

Safari ya Enzo haikuwa rahisi, kwani alihamia vilabu kadhaa tofauti katika juhudi za kupata nafasi ya kudumu ya kuonyesha kipaji chake. Alicheza kwenye vilabu vya Lausanne-Sport ya nchini Uswisi, Desportivo das Aves ya nchini Ureno, na Almería ya nchini Hispania. Ingawa alionyesha uwezo wake katika vilabu hivi, hakupata nafasi ya kudumu kama alivyotarajia.

Uamuzi wa Enzo kustaafu soka umekuja baada ya kutafakari kwa kina kuhusu mustakabali wake. Katika taarifa aliyotoa, Enzo ameeleza kuwa amefurahia safari yake ya soka na anashukuru kwa fursa alizopata, lakini kwa sasa anahisi ni wakati wa kuanza changamoto mpya katika maisha yake. Aliongeza kuwa anapanga kuendelea kuwa karibu na soka,na kujaribu fursa zingine kama ukocha.

real-madrids-french-midfielder-enzo-255582945.png
 
Hivi kuna mwanasoka gani mahiri ambae mtoto wake nae alikua mchezaji mahiri?
Pele
Maradona
Garincha
Frank Rjikaard
Kluivert
Beckham
Ronaldo
Figo
Zidane
Ronaldinho
List ni ndefu
 
Wapo wakina mao mkami na kijana wake Himid Mao

Wapo wakina Sure boy

Wapo wakina Ngasa

Wapo wakina Maftaa

Wapo wakina Manyika

Wapo wakina tegete

Huku kwetu kiasi chake tumeweza...


Huko Ulaya ni wachache sana kama wakina Jini la Man city...
 
Hivi kuna mwanasoka gani mahiri ambae mtoto wake nae alikua mchezaji mahiri?
Pele
Maradona
Garincha
Frank Rjikaard
Kluivert
Beckham
Ronaldo
Figo
Zidane
Ronaldinho
List ni ndefu
Alfie Halaand =
Erling Halaand.
Peter Schmeichel=
Kasper Schmeichel.
Cesare Maldini =
Paolo Maldini
Johan Cruyff=
Jordi Cruyff
Paolo Maldini =
Daniel Maldini.
Harry Redknapp=
Jamie Redknapp
Orodha hii pia ni ndefu sana
 
Hivi kuna mwanasoka gani mahiri ambae mtoto wake nae alikua mchezaji mahiri?
Pele
Maradona
Garincha
Frank Rjikaard
Kluivert
Beckham
Ronaldo
Figo
Zidane
Ronaldinho
List ni ndefu
Wapo wengi tu,ila hawa ni baadhi yao.
  1. Justin Kluivert,mtoto wa Patrick Kluivert
  2. Marcus Thuram,Mtoto wa Lilian Thuram na mtoto wake mwingine anaitwa Khephren Thuram,
  3. Timothy Weah,mtoto wa George Weah
  4. Giovanni Simeone,mtoto wa Diego Simeone
  5. Ianis Hagi,mtoto wa Gheorghe Hagi,
  6. Erling Haaland,mtoto wa ALf inge Haaland,
  7. Daniel Maldini,mtoto wa Paolo Maldini
  8. Romeo Beckham,mtoto wa David Beckham
  9. Alexis Mac Allister,mtoto wa Carlos Mac Allister
  10. Rubben van Bommel,mtoto wa Mark van Bommel,
 
Hivi kuna mwanasoka gani mahiri ambae mtoto wake nae alikua mchezaji mahiri?
Pele
Maradona
Garincha
Frank Rjikaard
Kluivert
Beckham
Ronaldo
Figo
Zidane
Ronaldinho
List ni ndefu
Abed Pele baba Jordan Ayew na André Ayew awa ndugu wawili mmoja kaichezea timu ya taifa ujerumani mwingine timu ya taifa ya Ghana.
 
Abed Pele baba Jordan Ayew na André Ayew awa ndugu wawili mmoja kaichezea timu ya taifa ujerumani mwingine timu ya taifa ya Ghana.
Kuna hawa brothers pia,
Jerome Boateng,alichezea team ya taifa ya Ujeruman ila Kaka yake anayeitwa Kevin Prince Boateng,yeye alichezea team ya taifa ya Ghana.
 
Hivi kuna mwanasoka gani mahiri ambae mtoto wake nae alikua mchezaji mahiri?
Pele
Maradona
Garincha
Frank Rjikaard
Kluivert
Beckham
Ronaldo
Figo
Zidane
Ronaldinho
List ni ndefu

Paolo Maldini yule beki kitasa wa AC Milan, baba yake Cesare Maldini alikuwa mchezaji mkubwa kitambo wa Italy na AC Milan...
 
Back
Top Bottom