Mtu huyu Eddo Kumwembe

Mtu huyu Eddo Kumwembe

Pele hawafikii hao watu.. Hata kidogo, usilinganishe wachezaji wa Sheria 3 na 17.

Pele sijamwona live ila clip zake nimeziona, ana mpira wa kawaida sana na mabeki na makipa wa wakati ule hawakua na viwango vyovyote, no offsides.. Saivi beki anakuchezea offside trick which means mshambuliaji anatumia akili mingi sana aweze kufunga. Akina Pele walikua wanajifungia tu kama rede
kwamba??
 
Anao anao nyingiii! Hivi pele angekabwa na mabeki wa aina ya Frank Libouf, Marceil Desaily, Nigal de Jong Javier Mascherano and a like angefunga migoli yote hayo? Pele mwenyewe hamfikii Maradona. Kwanza kule kushindwa tu kucheza ulaya kumesha mpunguzia credit. Ona. Ronaldo kwa mfano. Kacheza vilabu vikubwa ulaya. Sportin Lisbon, Man united, na sasa Real Madrid. Maradona yeye kasukuma ngozi pale Barcelona, napoli, na sevila. Messi ingawa anachezea barca, bd ni moja ya club kubwa barani ulaya na duniani kwa ujumla.
 
Anao anao nyingiii! Hivi pele angekabwa na mabeki wa aina ya Frank Libouf, Marceil Desaily, Nigal de Jong Javier Mascherano and a like angefunga migoli yote hayo? Pele mwenyewe hamfikii Maradona. Kwanza kule kushindwa tu kucheza ulaya kumesha mpunguzia credit. Ona. Ronaldo kwa mfano. Kacheza vilabu vikubwa ulaya. Sportin Lisbon, Man united, na sasa Real Madrid. Maradona yeye kasukuma ngozi pale Barcelona, napoli, na sevila. Messi ingawa anachezea barca, bd ni moja ya club kubwa barani ulaya na duniani kwa ujumla.
Mkuu hebu nenda you tube uone clips za pele kwanza,kisha ndo urudi ku comment
 
Mkuu unachekesha sana!hakuna anayemfikia pele kwa ku dribble,kufunga,chenga na pasi

Hahahahaha acha kuchekesha mkuu.. Pele alikua hakabwi na pia mabeki wa wakati ule ni wazembe. Hivi ushaona Messi anavyotembea na vijiji?? Unaona jinsi ambavyo kavunja karibia kila aina ya record?? Ushaona anayoyafanya Ronaldo?? Ukiangalia clip za Pele alafu uje ulinganishe na za kina Ronaldo utacheka sana
 
Mkuu hebu nenda you tube uone clips za pele kwanza,kisha ndo urudi ku comment

ukitaka skills, pele hamfikii Dinho, Zizou, hata Jay jay Okocha. Sema kila zama na kitabu chake. Muhameid Ally, angepambana na Tyson asingetoka salama. Zama zake zilipita akaja Tyson. Kwangu Tyson mkali zaidi kuliko Ally.
 
ukitaka skills, pele hamfikii Dinho, Zizou, hata Jay jay Okocha. Sema kila zama na kitabu chake. Muhameid Ally, angepambana na Tyson asingetoka salama. Zama zake zilipita akaja Tyson. Kwangu Tyson mkali zaidi kuliko Ally.

Hivi mkuu uliona ile tik tak aliyofunga Pele wanayomsifia?? Utacheka ufe, mtu yupo ndani ya boksi anabetua mpira anapiga danadana moja anapiga tik tak golii.. Wakati wote huo mabeki wanashangaa tu na kipa nae lofa sana.

Ile tik tak hawezi kuifananisha na ile aliyopiga Rooney dhidi ya Man City
 
Wachezaji bora duniani ni zidane na dinho,haijawahi na haitowahi kutokea kama wao
 
Anao anao nyingiii! Hivi pele angekabwa na mabeki wa aina ya Frank Libouf, Marceil Desaily, Nigal de Jong Javier Mascherano and a like angefunga migoli yote hayo? Pele mwenyewe hamfikii Maradona. Kwanza kule kushindwa tu kucheza ulaya kumesha mpunguzia credit. Ona. Ronaldo kwa mfano. Kacheza vilabu vikubwa ulaya. Sportin Lisbon, Man united, na sasa Real Madrid. Maradona yeye kasukuma ngozi pale Barcelona, napoli, na sevila. Messi ingawa anachezea barca, bd ni moja ya club kubwa barani ulaya na duniani kwa ujumla.

Nimeisha kuambia hakucheza Ulaya kwa sheria ya bunge la Brazil siyo kwa kujipendea, taja shara za serikali Tanzania, mnyama twiga, madini ya almasi kwa Brazil nyara kama hizo alikuwa ni King Pele.
 
Mambo ya baba ake Edo yanakujaje hapa?
Unamuonya kama nani?
Unataka kila MTU afikiri sawa?
Kuna wengine wanáamini ngasa ni zaidi ya mmessi!
hilo kosa unalomlaumia hapo juu ndio hilohilo unalomfanyia yeye. Naye mwache atoe fikra zake kwa kadri anavyojisikia, madhali havunji sheria.
 
Sasa Ronaldo na Messi wake wachezaji hawa niliowataja hapo juu hawawafikii hata nusu, Ronaldo hamfikii kabisa Kassim Manara kwa kila kitu iwe stamina au ball control wachezaji hao wamecheza miaka ya 70 na 80 mwanzoni, sasa kama hao hawawafikii itakuwaje Eddo awalinganishe na King Pele?

Ata hao uliwataja hawawafikii kina Yungi Mwanansare, Abushir, Sebwana, John Lyimo



 
Hata ww na Eddo hamfanani.. Tatzo la nyinyi wazee wenzangu wa zamani mna shida sana mnapenda kujiona nyinyi enzi zenu ni bora sana.. Binafsi namkubali sana Eddo tafakuri zake

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
umejitahidi kueleza, lakini hata wewe uko biased, huwezi kusema ronaldo ni mbio tuu.

chuki zake tu ka base kwenye kuponda tu nao wana mazuri yao mm mwenyewe simuelewi pele wala maradona sijwakuta na sikuwahi kuwaona imebaki historia saivi ni mess na ronaldo tu hao hadi mtupe historia na video zao tukimaliza darasa kila wik end tunakwenda kuwangalia live mess,ronaldo,costa.falcao na wengine kizazi kipya hiki tunashukuru kwa history
 
Pele hakuwa na uwezo kama anavyopambwa na wazungu hasa waingereza
unakumbuka goli la mkono wa mungu achana na goli analochukua wachezaji watano na kufunga goli zuri kabisa Huyo ndio maradona
we zamani wachezaji waliokuwa wanacheza mpaka wastaafu kazi zao ndio wacheze mpira mtu ana miaka 40 bado anacheza mpira wapi na wapi ??

Pele alikuwa kama forward wa chandimu harudi nyuma mpira ukianza yeye yupo golini kama beki kumbe ndio forward wao wa kutegemewa shame...!!

Refa anaingia uwanjani amevaa suti huku ana siga mkononi eti ndio mchezaji awe bora halafu anafimbo
huu ni upuuzi na wendawazimu kukubali kwamba Pele ni zaidi ya messi unahitaji akili kubwa kunishauri nikakubali ila nitakusikiliza

Modern football hautumii nguvu sana kama wazee wa zilipendwa ni akili zaidi ndio maana wachezaji ni wenye maumbo madogo madogo tu.

Siku hizi mpira unafundishwa darasani unatulia zamani mtu amelewa anaingia uwanjani ndio maana siku hizi watu wanawekeza kwenye mpira

wazee wa zamani mlikuwa mnasikiliza mpira sisi tunaangalia

Messi ndiye mchezaji bora wa mpira wa miguu wa muda wote
 
Niliyoyaona kwenye sakata lote hili:
1. Waandishi wetu kuandika sio wanachokiamini, ispokua wanachoamini kitawafanya waonekane kuwa mahiri mbele ya wasomaji. Kwa hivyo ni lazima waandike maoni yaliyo kinyume na mawazo ya wefngi (against the general public opinion) hata kama wao wenyewe ni sehemu ya hao wengi.
2. Waandishi wetu kununua ihasni (favour) kwa watu mashuhuri kwa kupitia kalamu zao. Hufanya hivyo kwa kuwasifu watu hao mashuhuri, au mambo yanayohusiana nao, au kuwakebehi (sio kukosoa) wapinzani wa hao watu mashuhuri au mambo yanayohusiana nao.
3. Waandishi wetu kutumia kalamu zao kuendekeza visa na visasi vyao dhidi ya mahasimu wao, hata kama uhasama wenyewe ni tofauti tu ya timu wanazozipendelea.
4. Sisi wasomaji kushindwa kutofautisha baina ya maoni na hukumu, hivyo kuamini kila aliyeandika makala yanayounga mkono ushabiki wetu kwa swala fulani hawawezi kuwa wamekosea na kila wanaokebehi (sio kukosoa) swala tunalolishabikia hawawezi kuwa sahihi.
5. Sisi wasomaji kutaka waandishi wawe na mawazo yaliyo sawa na yetu kwa 100%.
6. Waandishi kutotanabahisha misimamo na maslahi yao kwenye jambo wanaloliandikia, ili wasomaji tutafsiri makala na maoni yao kwa mujibu wa misimamo na maslahi hayo.
7. Wapenzi wa soka, hasa waandishi na wasomaji kun'gan'gania bila ya kuyumba kwenye mojawapo ya dhana mbili kuu. Kizazi cha sasa kinatawaliwa na dhana ya 'kipya kinyemi' bila ya kujua kuwa kinaweza kikawa ni kidonda pia. Kizazi cha kale kinatawaliwa na dhana ya 'vya kale ni dhahabu' bila ya kujali kwamba baadhi ya dhahabu zinaweza kuwa feki.

Kwa msingi huo, mtu pekee awezaye kutoa maoni yasiyofungamana juu ya wachezaji hawa ni yale anayeishi kwenye sayari nyengine, au wa sayari hii asiyejua chochote kuhusu kabumbu. Wageni hao wa soka baadaye wawekwe darasani kuelimishwa kuhusu mchezo huo, waoneshwe uchezaji na wachezaji wazuri wa mchezo huo zama hizo na hizi wasiokuwa hao wanaobishaniwa. Baadaye ndio waoneshwe uchezaji wa wanaobishaniwa na kutakiwa watoe maoni yao.
 
messi akili nyingi ww

acha poteza muda huyu pelle unaye mtetea hapo amesha kili messi ni level nyingine

Messi ana command mpira yule mguu mmoja kma ana miguu mia
 
Mtoa hoja is just living in a stone age era,scientifically soccer ime-undergo lots of changes for the better,kitambo kulikuwa na talents tu but now people can be trained to bend like Beckham or rooney.Soccer sasa ni biashara.
 
Back
Top Bottom