Mtu kujitangaza kaokoka ama watu kumsemea kaokoka ni undumilakuwili, matendo yake ya mafichoni na fikra zake haviwezi kuonekana kirahisi.

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Mimi nimeokoka sikuhizi, Fulani kaokoka baada ya kutoka jela, fulani kaokoka baada ya kuponea chupu chupu ajali, n.k, ni kauli ambazo nikizisikia namrefer mhusika moja kwa moja na ndumilakuwili.

Kuokoka huwa ni siri ya mtu binafsi na Mwenyezi Mungu, kwamba yeye anatenda, kufikiri, kunena, n.k yanayompendeza Mungu bila kupretend bali kwa moyo mweupe kabisa

Kitu cha kwanza kabisa kusema flani kaokoka ni undumilakuwili, kuokoka ni ndani ya moyo kuzidi machoni, kuna matendo yake yanayoonekana mbele yetu lakini kuna matendo yake ya siri huko chumbani, kuna fikra zake anazifikiria ndani ya kichwa chake hatuwezi kuziona, kuna maneno anayonena kwa masikio yetu tunaweza kuyasikia lakini hatujui kama kayamaanisha, n.k.

Kitu cha pili kujinadi kaokoka ni undumilakuwili, Kuokoka na kuacha madhambi ni process sio kitu cha siku moja , hata siku ya leo unaweza kuamua kwamba umeacha dhambi lakini wanadamu huwa tuna kawaida ya kurelapse kurudi kwenye dhambi zilizotukolea kuzifanya, ni kama vile mtu aliezoea pombe ama madawa mengine ya kulevya anaweza kuacha leo lakini kesho akarudia, inawezekana ila sio rahisi kuacha na ni wachache huwa wanaweza.

Kitu cha pili kujinadi ama kumnadi fulani kaokoka ni undumilakuwili, watu wakirudi kwenye dhambi wanakaa kimya, kwanini kusiwe na kujitangaza kwamba kashindwa kuokoka, hapa ndipo unafki wa haya mambo yalipo, tunasikia tu watu wanaokoka lakini wanakuwa wazito kujitangaza wamerudi kwenye madhambi, wanapenda sifa ya kuonekana wameokoka lakini hawapendi uwajibikaji wanapotoka nje ya mstari.

machoni mtu mnamuona kaokoka yupo kupeleka mahitaji kwa nyumba za watoto yatima, kila jumapili anagudhuria kanisani, ni mshauri kwa vijana waliopotea njia, n.k. lakini vyote hivi ni vile mnavyoviona kwa macho yenu tu na sio picha kamil

lakini ni mtu huyo huyo ni mzinzi wa kubadilisha wake za watu kimya kimya, usiku nyumbani kwake huwa anautwika analewa tila lila, smartphone yake imejaa oicha na video za uchi, ni mtu wa visasi vya mauaji, kanisani anaenda kiushahidi, n.k.
 
dunia unafiki hii mkuu ,MTU anajitangazia kaokoka ili kujitaftia huruma ya jamii
 
Kumewahi kuwa na manabii kibao walioenenda katika njia zinazopendeza lakini hakuna hata moja aliejinadi kaokoka
Aaaah , kuokoka mpaka hekima ya MUNGU imulike njia zako Mimi nilivyojua huu mfumo nimekabidhi MUNGU maisha yangu.

Maana unapokuwa unaukataa uzinzi basi ndo mnara unasoma 5G na kushobokewa na wanawake wa kila aina sasa bila hekima ya MUNGU huwezi kutoboa.
 
Kuokoka na kuacha madhambi ni process, sio kitu cha siku moja.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Dini imeletwa na wahuni, ili kutucheleweshea maendeleo yetu,
 
Kuokoka na kuacha madhambi ni process, sio kitu cha siku moja.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
Dhambi ni kama madawa ya kulevya na pombe, kuiacha sio uamuzi wa siku moja tu, na kuna muda ili mtu aziache inabidi aumie, mfano mtu muongo inabidi akubali kudhalilika kwamba vitu alivyodanganya hana, Muuaji inabidi akakiri kwa familia ya mtu aliemuua na awe tayari kwenda jela, n.k.
 
Kwakweli sio kazi rahisi
 
Nifah
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…