Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,336
- 4,731
Tukio hilo limetokea katika kitongoji cha Kwamagome kilichopo ndani ya halmashauri ya mji Handeni majira ya saa kumi na mbili jioni, huku Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Blasius Chatanda akithibisha kutokea kwa tukio hilo na kusema Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha tukio hilo.
Chanzo: ITV
=========
Akizungumza akiwa hospitali ya wilaya Handeni, baba mzazi wa mmoja wa majeruhi Waziri Mhina amesema tukio hilo limetokea jioni ambapo mtoto wake wa miaka sita Hossein Mhina, amekatwa sehemu ya uso na kuumia vibaya huku akivuja damu nyingi.
Aidha majeruhi wengine katika tukio ni Mwaliko Sadiki amekatwa mkono wa kushoto, Mgaza Waziri mkono wa kulia na Kabelwa Zuberi aliyekatwa maeneo ya tumboni, ambapo wote walifikishwa hospitali ila Yasin Athuman alifariki hapo hapo baada ya kukatwa mkono na mguu.
Mtuhumiwa wa tukio hilo Ramadhani Abdi naye alishambuliwa na wananchi wenye hasira kali na amelazwa hospitali akiwa chini ya ulinzi wa polisi.