Asilimia kubwa ya wabunifu wa zamani walifanya vitu kimakosa ndipo kukagundukika kitu kipya mfano tuchukulie ugali watu zamani walikuwa wanakula nafaka kwa kutafuna ila siku moja dogo kaona kuliko nitafune pora nipondeponde nibwie tu jumla hapo wakagundua unga siku nyingine dogo kashindwa kubwia unga akaona bora aweke maji ili anywe kwa wingi hapo ukagundulika msukulu au unga uliowekwa maji siku nyingine kwenye baridi kali maji hayanyweki ule uji mbichi haunyweki pia,dogo akaona auweke jikoni upate moto ili anywe ukapatikana uji siku nyingine wazazi wapo shamba dogo kaambiwa apike uji akazidisha unga kupeleka shamba kala fimbo za kutosha lakini walikula kwa shida baadae wakazoea ukatokea ugali huu mfano ndivyo pombe nayo ilivyogunduliwa hawakujua ninini lakini kama ni matunda yalichumwa leo wakala yakabaki yakachachuka kesho walivyokula wakaona mbona yapo hivi ni fikra zangu tu