Mtuhumiwa wa Bangi alalamika kufutiwa kesi mara 5 bila kuachiwa kwa miaka 8

Mtuhumiwa wa Bangi alalamika kufutiwa kesi mara 5 bila kuachiwa kwa miaka 8

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Hassan Banda anayedaiwa kukutwa na Bangi mwaka 2016, ameiomba Mahakama ya Kisutu imrudishe Mahabusu za Polisi kwa sababu mpaka sasa amewekwa Gerezani bila hukumu kwa kile kinachodaiwa ni "Upelelezi Haujakamilika".

Banda amesema, licha ya Rais Samia kuagiza kufutwa kwa kesi zisizokuwa na msingi, kesi yake imeshafutwa mara 5 lakini amekuwa akifunguliwa mashtaka upya, pia alishaandika barua ya kuingia makubaliano ya 'Plea Bargain' lakini hajapata majibu.

Mahakama imekubaliana na hoja za Banda na kuueleza upande wa Mashtaka kama hautakuwa na jibu la kuridhisha itamwachia huru mtuhumiwa huyo. Kesi itarejea tena Februari 21, 2023.

================

MSHITAKIWA Hassan Banda anayedaiwa kukutwa na bangi, ameiomba mahakama arudishwe katika kituo cha polisi hadi pale upelelezi utakapokamilika, kwa sababu mpaka sasa yuko gerezani kwa kile kinachodaiwa upelelezi haujakamilika.

Aidha, amedai kuwa hivi karibuni, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan alitaka kesi zisizokuwa na msingi zifutwe kwa sababu kesi yake hadi sasa imefutwa mara tano na kufunguliwa upya kwa madai kwamba upelelezi bado.

Banda alidai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Evodia Kyaruzi, wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kutajwa. Wakili wa Serikali, Monica Ndakidemi, alidai kuwa upelelezi haujakamilika.

Alidai kuwa faili bado liko kituo cha polisi na kwamba limerudishwa kwa ajili ya marekebisho ya kiupelelezi, hivyo akaomba tarehe ya kutajwa.

"Kesi yangu ina mwaka wa nane tangu Agosti, 2016 nilipokamatwa. Kila siku majibu ni yale yale ya upande wa mashtaka kuwa upelelezi bado haujakamilika.

"Nimekaa gerezani muda mrefu hadi naumwa mgongo, macho na pumu. Pia niliandika barua ya kuingia makubaliano 'plea bargaining' lakini sijapata. Nimechoka kukaa gerezani, naomba mahakama inirudishe polisi hadi upelelezi utakapokamilika ndiyo niletwe mahakamani," alidai.

Pia alidai kuwa kesi yake imeshafutwa mara tano na kufunguliwa upya kwa mashtaka yale yale huku familia na ndugu wakiwa wanamtegemea, hivyo akaomba aonane na kiongozi wa waendesha mashtaka mahakamani hapa, Grace Mwanga, ili amsaidie.

Baada ya mshtakiwa huyo kudai hayo, Hakimu Kyaruzi alisema hoja zilizotolewa ni za msingi kwa hiyo tarehe ijayo kama upande wa mashtaka hautakuwa na jibu la kuridhisha mahakama itamruhusu aonane na Mwanga.

Akijibu hoja za mshtakiwa, Wakili Ndakidemi alidai kuwa alichokidai ni cha kweli, kwa hiyo atajitahidi kuwasiliana na uongozi wa polisi ili kurudisha faili kesi iendelee.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 21 kwa ajili ya kutajwa na kuangalia hatua za faili zilipofikia.

Inadaiwa kuwa Agosti 25, 2016 mshtakiwa akiwa eneo la Mbezi Kibanda cha Mkaa wilayani Ubungo, alikutwa na bangi.

NIPASHE
 
Hassan Banda anayedaiwa kukutwa na Bangi mwaka 2026, ameiomba Mahakama ya Kisutu imrudishe Mahabusu za Polisi kwa sababu mpaka sasa amewekwa Gerezani bila hukumu kwa kile kinachodaiwa ni "Upelelezi Haujakamilika".

Banda amesema, licha ya Rais Samia kuagiza kufutwa kwa kesi zisizokuwa na msingi, kesi yake imeshafutwa mara 5 lakini amekuwa akifunguliwa mashtaka upya, pia alishaandika barua ya kuingia makubaliano ya 'Plea Bargain' lakini hajapata majibu.

Mahakama imekubaliana na hoja za Banda na kuueleza upande wa Mashtaka kama hautakuwa na jibu la kuridhisha itamwachia huru mtuhumiwa huyo. Kesi itarejea tena Februari 21, 2023.

================

MSHITAKIWA Hassan Banda anayedaiwa kukutwa na bangi, ameiomba mahakama arudishwe katika kituo cha polisi hadi pale upelelezi utakapokamilika, kwa sababu mpaka sasa yuko gerezani kwa kile kinachodaiwa upelelezi haujakamilika.

Aidha, amedai kuwa hivi karibuni, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan alitaka kesi zisizokuwa na msingi zifutwe kwa sababu kesi yake hadi sasa imefutwa mara tano na kufunguliwa upya kwa madai kwamba upelelezi bado.

Banda alidai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Evodia Kyaruzi, wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kutajwa. Wakili wa Serikali, Monica Ndakidemi, alidai kuwa upelelezi haujakamilika.

Alidai kuwa faili bado liko kituo cha polisi na kwamba limerudishwa kwa ajili ya marekebisho ya kiupelelezi, hivyo akaomba tarehe ya kutajwa.

"Kesi yangu ina mwaka wa nane tangu Agosti, 2016 nilipokamatwa. Kila siku majibu ni yale yale ya upande wa mashtaka kuwa upelelezi bado haujakamilika.

"Nimekaa gerezani muda mrefu hadi naumwa mgongo, macho na pumu. Pia niliandika barua ya kuingia makubaliano 'plea bargaining' lakini sijapata. Nimechoka kukaa gerezani, naomba mahakama inirudishe polisi hadi upelelezi utakapokamilika ndiyo niletwe mahakamani," alidai.

Pia alidai kuwa kesi yake imeshafutwa mara tano na kufunguliwa upya kwa mashtaka yale yale huku familia na ndugu wakiwa wanamtegemea, hivyo akaomba aonane na kiongozi wa waendesha mashtaka mahakamani hapa, Grace Mwanga, ili amsaidie.

Baada ya mshtakiwa huyo kudai hayo, Hakimu Kyaruzi alisema hoja zilizotolewa ni za msingi kwa hiyo tarehe ijayo kama upande wa mashtaka hautakuwa na jibu la kuridhisha mahakama itamruhusu aonane na Mwanga.

Akijibu hoja za mshtakiwa, Wakili Ndakidemi alidai kuwa alichokidai ni cha kweli, kwa hiyo atajitahidi kuwasiliana na uongozi wa polisi ili kurudisha faili kesi iendelee.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 21 kwa ajili ya kutajwa na kuangalia hatua za faili zilipofikia.

Inadaiwa kuwa Agosti 25, 2016 mshtakiwa akiwa eneo la Mbezi Kibanda cha Mkaa wilayani Ubungo, alikutwa na bangi.

NIPASHE
2026 tumefika lini?
 
Hassan Banda anayedaiwa kukutwa na Bangi mwaka 2016, ameiomba Mahakama ya Kisutu imrudishe Mahabusu za Polisi kwa sababu mpaka sasa amewekwa Gerezani bila hukumu kwa kile kinachodaiwa ni "Upelelezi Haujakamilika".

Banda amesema, licha ya Rais Samia kuagiza kufutwa kwa kesi zisizokuwa na msingi, kesi yake imeshafutwa mara 5 lakini amekuwa akifunguliwa mashtaka upya, pia alishaandika barua ya kuingia makubaliano ya 'Plea Bargain' lakini hajapata majibu.

Mahakama imekubaliana na hoja za Banda na kuueleza upande wa Mashtaka kama hautakuwa na jibu la kuridhisha itamwachia huru mtuhumiwa huyo. Kesi itarejea tena Februari 21, 2023.

================

MSHITAKIWA Hassan Banda anayedaiwa kukutwa na bangi, ameiomba mahakama arudishwe katika kituo cha polisi hadi pale upelelezi utakapokamilika, kwa sababu mpaka sasa yuko gerezani kwa kile kinachodaiwa upelelezi haujakamilika.

Aidha, amedai kuwa hivi karibuni, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan alitaka kesi zisizokuwa na msingi zifutwe kwa sababu kesi yake hadi sasa imefutwa mara tano na kufunguliwa upya kwa madai kwamba upelelezi bado.

Banda alidai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Evodia Kyaruzi, wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kutajwa. Wakili wa Serikali, Monica Ndakidemi, alidai kuwa upelelezi haujakamilika.

Alidai kuwa faili bado liko kituo cha polisi na kwamba limerudishwa kwa ajili ya marekebisho ya kiupelelezi, hivyo akaomba tarehe ya kutajwa.

"Kesi yangu ina mwaka wa nane tangu Agosti, 2016 nilipokamatwa. Kila siku majibu ni yale yale ya upande wa mashtaka kuwa upelelezi bado haujakamilika.

"Nimekaa gerezani muda mrefu hadi naumwa mgongo, macho na pumu. Pia niliandika barua ya kuingia makubaliano 'plea bargaining' lakini sijapata. Nimechoka kukaa gerezani, naomba mahakama inirudishe polisi hadi upelelezi utakapokamilika ndiyo niletwe mahakamani," alidai.

Pia alidai kuwa kesi yake imeshafutwa mara tano na kufunguliwa upya kwa mashtaka yale yale huku familia na ndugu wakiwa wanamtegemea, hivyo akaomba aonane na kiongozi wa waendesha mashtaka mahakamani hapa, Grace Mwanga, ili amsaidie.

Baada ya mshtakiwa huyo kudai hayo, Hakimu Kyaruzi alisema hoja zilizotolewa ni za msingi kwa hiyo tarehe ijayo kama upande wa mashtaka hautakuwa na jibu la kuridhisha mahakama itamruhusu aonane na Mwanga.

Akijibu hoja za mshtakiwa, Wakili Ndakidemi alidai kuwa alichokidai ni cha kweli, kwa hiyo atajitahidi kuwasiliana na uongozi wa polisi ili kurudisha faili kesi iendelee.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 21 kwa ajili ya kutajwa na kuangalia hatua za faili zilipofikia.

Inadaiwa kuwa Agosti 25, 2016 mshtakiwa akiwa eneo la Mbezi Kibanda cha Mkaa wilayani Ubungo, alikutwa na bangi.

NIPASHE
WaTz na mifumo yetu tuwe na utu! Miaka 8, kuna ushahidi gani mpya utakaoibuka, zaidi ya kusahau hata yaliyotokea? Wanasheria wanafanya mambo kama hawajasoma?!
 
Utakuta watoto wadogo wanaolala kwenye sebule za shemeji zao wanabeza mapigano ya katiba mpya.


Qumerniner zao
We zoba unadhani nchi zenye katiba bora haya hayapo

USSR
 
Huyo hakimu evodia kyaruzi namjua personally, alikua hakimu mahakama ya wilaya kahama! Ndo akahamishiwa huku, aisee huyo dada hachukui rushwa hata Senti mia yaani yupo straight tuliwahi kupata msala tukataka kumpa kibunda alitufukuza kama mbwa


Kuja uliza ma secretary yaani hata wao hawampendi Kila michongo wakimpa anawatolea nje, huyo dada kiboko
 
Hassan Banda anayedaiwa kukutwa na Bangi mwaka 2016, ameiomba Mahakama ya Kisutu imrudishe Mahabusu za Polisi kwa sababu mpaka sasa amewekwa Gerezani bila hukumu kwa kile kinachodaiwa ni "Upelelezi Haujakamilika".

Banda amesema, licha ya Rais Samia kuagiza kufutwa kwa kesi zisizokuwa na msingi, kesi yake imeshafutwa mara 5 lakini amekuwa akifunguliwa mashtaka upya, pia alishaandika barua ya kuingia makubaliano ya 'Plea Bargain' lakini hajapata majibu.

Mahakama imekubaliana na hoja za Banda na kuueleza upande wa Mashtaka kama hautakuwa na jibu la kuridhisha itamwachia huru mtuhumiwa huyo. Kesi itarejea tena Februari 21, 2023.

================

MSHITAKIWA Hassan Banda anayedaiwa kukutwa na bangi, ameiomba mahakama arudishwe katika kituo cha polisi hadi pale upelelezi utakapokamilika, kwa sababu mpaka sasa yuko gerezani kwa kile kinachodaiwa upelelezi haujakamilika.

Aidha, amedai kuwa hivi karibuni, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan alitaka kesi zisizokuwa na msingi zifutwe kwa sababu kesi yake hadi sasa imefutwa mara tano na kufunguliwa upya kwa madai kwamba upelelezi bado.

Banda alidai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Evodia Kyaruzi, wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kutajwa. Wakili wa Serikali, Monica Ndakidemi, alidai kuwa upelelezi haujakamilika.

Alidai kuwa faili bado liko kituo cha polisi na kwamba limerudishwa kwa ajili ya marekebisho ya kiupelelezi, hivyo akaomba tarehe ya kutajwa.

"Kesi yangu ina mwaka wa nane tangu Agosti, 2016 nilipokamatwa. Kila siku majibu ni yale yale ya upande wa mashtaka kuwa upelelezi bado haujakamilika.

"Nimekaa gerezani muda mrefu hadi naumwa mgongo, macho na pumu. Pia niliandika barua ya kuingia makubaliano 'plea bargaining' lakini sijapata. Nimechoka kukaa gerezani, naomba mahakama inirudishe polisi hadi upelelezi utakapokamilika ndiyo niletwe mahakamani," alidai.

Pia alidai kuwa kesi yake imeshafutwa mara tano na kufunguliwa upya kwa mashtaka yale yale huku familia na ndugu wakiwa wanamtegemea, hivyo akaomba aonane na kiongozi wa waendesha mashtaka mahakamani hapa, Grace Mwanga, ili amsaidie.

Baada ya mshtakiwa huyo kudai hayo, Hakimu Kyaruzi alisema hoja zilizotolewa ni za msingi kwa hiyo tarehe ijayo kama upande wa mashtaka hautakuwa na jibu la kuridhisha mahakama itamruhusu aonane na Mwanga.

Akijibu hoja za mshtakiwa, Wakili Ndakidemi alidai kuwa alichokidai ni cha kweli, kwa hiyo atajitahidi kuwasiliana na uongozi wa polisi ili kurudisha faili kesi iendelee.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 21 kwa ajili ya kutajwa na kuangalia hatua za faili zilipofikia.

Inadaiwa kuwa Agosti 25, 2016 mshtakiwa akiwa eneo la Mbezi Kibanda cha Mkaa wilayani Ubungo, alikutwa na bangi.

NIPASHE
kuna POLISI atakuwa anatembea na mke wa huyu jamaa!
 
WaTz na mifumo yetu tuwe na utu! Miaka 8, kuna ushahidi gani mpya utakaoibuka, zaidi ya kusahau hata yaliyotokea? Wanasheria wanafanya mambo kama hawajasoma?!
Sio vizuri kabisa kumweka mtu ndani miaka 8 kisa ganja na ushahidi usiwepo.. wakati mwingine tutumie utu na best judgement tu
 
Huyo hakimu evodia kyaruzi namjua personally, alikua hakimu mahakama ya wilaya kahama! Ndo akahamishiwa huku, aisee huyo dada hachukui rushwa hata Senti mia yaani yupo straight tuliwahi kupata msala tukataka kumpa kibunda alitufukuza kama mbwa


Kuja uliza ma secretary yaani hata wao hawampendi Kila michongo wakimpa anawatolea nje, huyo dada kiboko

Yule Dada anafaa apewe ujaji ni mwadilifu sana hata mimi habari zake nilipata sehemu yaani bora ukaombe akusaidie bila hela ukimpa hela umeharibu kila kitu, hachukui rushwa kabisa anashangaza wengi
 
mimi nikisema kwamba nikikuta Polisi anapigana na Nyoka ni nitamsaidia nyoka muwe mnanielewa.

yaani Polisi anaweza akaamua akukomoe tu basi.

hawa Watu sijui wameumbwa na Mungu huyu huyu aliyetuumba sisi ?🤔

Polisi popote ulipo hebu imagine wewe ingekua ndiye Hassan Banda
 
mimi nikisema kwamba nikikuta Polisi anapigana na Nyoka ni nitamsaidia nyoka muwe mnanielewa.

yaani Polisi anaweza akaamua akukomoe tu basi.

hawa Watu sijui wameumbwa na Mungu huyu huyu aliyetuumba sisi ?🤔

Polisi popote ulipo hebu imagine wewe ingekua ndiye Hassan Banda
exactly
 
Back
Top Bottom