Mtumishi wa Umma wa Kwanza Aliyezaliwa Siku ya Uhuru Kustaafu Mwaka Huu Desemba

Mtumishi wa Umma wa Kwanza Aliyezaliwa Siku ya Uhuru Kustaafu Mwaka Huu Desemba

eliakeem

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2009
Posts
17,214
Reaction score
15,853
Kwanza niwapongeze kwa shughuli za ujenzi wa Taifa. Nipende tu kuwakumbusha ya kuwa Nchi yetu sasa inaanza kukomaa na kuwa pevu. Nasema hivyo kwa sababu miaka yote tumekuwa tukishuhudia wastaafu ambao walikuwa wamezaliwa kipindi cha ukoloni. Yaani kabla ya uhuru wa Tanganyika.

Lakini sasa mwaka huu na kuendelea tutashuhudia wastaafu ambao wamezaliwa ndani ya kipindi cha uhuru. Heko baba wa Taifa na wengine wengi waliopigania na kuhangaikia uhuru mpaka kupatikana. Sasa matunda tumeyaona. Sasa wameanza kuwa watu wazima na hata wanazeeka.😀😀😀

Hivyo tunaanza kupata wahenga waliozaliwa kipindi cha uhuru. Tunaomba nao wawe na hekima na busara ili kuendelea kutupa misemo yenye kufundisha jamii, kama vile wahenga waliozaliwa kabla ya uhuru walivyotuachia hazina kubwa ya misemo. Mfano mimi binafsi napenda sana ule msemo "Asiye sikia la mkuu ..."

Mwisho niwatakie siku njema na pia kuendelea kupokea wahenga wapya. Yaani wastaafu waliozaliwa kipindi cha uhuru.

Uhuru hoyee!
 
  • Thanks
Reactions: RMC
Akili zingine Ni za kichawa kweli,Nani alikuambia kusitafu Hadi uwe unamiaka 60 ? He Ukisitafu unamiaka 55?
 
Akili zingine Ni za kichawa kweli,Nani alikuambia kusitafu Hadi uwe unamiaka 60 ? He Ukisitafu unamiaka 55?

Yaa inawezekana ukawa sahihi. Lkn hiyo siyo ya lazima. Tunaita premature retirement.
 
Kuanzia mwaka huu watumishi wengi waliozaliwa baada ya uhuru wataanza kustaafu kwa lazima.

Hivyo sherehe za uhuru mwaka huu ni za kipekee kwa namna hiyo.
 
  • Thanks
Reactions: RMC
Sasa wastaafu wote kuanzia Disemba ni wale waliozaliwa ndani ya uhuru kulelewa na kusoma ndani ya uhuru.
 
Back
Top Bottom