Mtwara: Askari Polisi mmoja kati watuhumiwa wa mauaji ya mfanyabiashara alikutwa mahabusu akiwa amejinyonga tarehe 22 Jan 2022

Mtwara: Askari Polisi mmoja kati watuhumiwa wa mauaji ya mfanyabiashara alikutwa mahabusu akiwa amejinyonga tarehe 22 Jan 2022

bievinii

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2021
Posts
712
Reaction score
736
Askari mmoja Kati waliokuwa wakituhumiwa kufanya mauaji ya mfanyabiashara kijana alijinyonga

====

Askari huyo alijinyonga Januari 22 mwaka huu 2022 kwa kutumia tambala la kudekia akiwa mahabusu ya kituo cha polisi wilaya ya Mtwara.

Katika taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mtwara ACP Mark Njera, alikiri kuwa askari wake saba wanaotuhumiwa kutekeleza mauaji ya kijana Mussa Hamisi (25), mkazi wa kijiji cha Ruponda wilaya ya Nachingwea mkoani humo aliyekuwa akiwadai askari hao zaidi ya shilingi milioni 33.7 wameshafikishwa mahakamani

Imeelezwa kuwa tukio la mauaji ya kijana huyo walilitekeleza Januari 5, 2022 na mwili wa marehemu waliutupa katika kitongoji cha Majengo, kijiji cha Hiari wilayani Mtwara.

Waliofikishwa Mahakamani Januari 25, 2022 ni:

1. Mrakibu wa Polisi Gilbert Kalanje -Mkuu wa Upelelezi wa wilaya ya Mtwara,

2. Mrakibu Msaidizi wa Polisi Charles Onyango - Mkuu wa Kituo cha Polisi Mtwara,

3. Mrakibu wa Polisi Msaidizi Nicholaus Kisinza - Mkuu wa Kikosi cha Intelejensia ya Jinai mkoa wa Mtwara,

4. Mkaguzi wa Polisi John Msuya Mganga - Mkuu wa Zahanati ya Polisi Mtwara,

5. Mkaguzi wa Polisi Msaidizi Marco Mbuta,

6. Mkaguzi wa Polisi Shirazi Mkupa na

7. Koplo Salimu Juma Mbalu.

Kuhusu mauaji ya mfanyabiashara, soma Mtwara: Maafisa Saba(7) wa Polisi wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya Kijana aliyekuwa akiwadai zaidi ya Tsh milioni 33.7 (Januari 25, 2022)


FB_IMG_16431767572068268.jpg

 
1643179324122.png

Afisa wa Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara, Mrakibu Msaidizi wa Polisi, Greyson Mahembe ambaye ni miongoni mwa maafisa saba wa jeshi hilo waliofunguliwa mashtaka ya mauaji ya mfanyabiashara amejinyonga kwa tambala la kudekia akiwa mahabusu ya kituo cha polisi wilaya ya Mtwara.

Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara liliwakamata na kuwafikisha mahakamani Maafisa wa Polisi saba kwa tuhuma za mauaji ya Mussa Hamisi Hamisi (25) mkazi wa Kijiji cha Ruponda wilayani Nachingwea Mkoani Lindi aliyekuwa akiwadai askari hao zaidi ya Sh milioni 33.7.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara, ACP Marck Njera ilisema mauaji hayo yalifanyika Januari 5, 2022 na mwili wa marehemu ulitupwa kitongoji cha Majengo kijiji cha Hiari Wilayani Mtwara.

Habari Leo

- Mtwara: Maafisa Saba(7) wa Polisi wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya Kijana aliyekuwa akiwadai zaidi ya Tsh milioni 33.7
 
Afisa wa Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara, ACP Greyson Mahembe ambaye ni miongoni mwa maafisa saba wa jeshi hilo waliofunguliwa mashtaka ya mauaji ya mfanyabiashara amejinyonga kwa tambala la kudekia akiwa mahabusu ya kituo cha polisi wilaya ya Mtwara...
Wameamua kumuondoa ili kupoteza ushahidi wakubwa wao wasitajwe
 
Hivi tambaza la deki kweli tambaa la deki hebu fikiria tena tambaa la nini la deki

Sasa ukirudi kwenye kesi ya Zombe na wenzake kuna askari mmoja naye alijinyonga hivyo hivyo

Kuna kitu hapo kuna kitu huenda huyo jamaa ndio anajua siri zote

Bila ya kuwekwa tume huru ya uchunguzi kama ile ya Zombe kuna mtu ataangushiwa Zigo la dhambi hapo
 
Tambala za deki zinaweza kuwemo sello za wao police Hadi simu wanaruhusiwa kutumia
 
Askari mmoja Kati ya wale 7 waliokuwa wakituhumiwa kufanya mauaji ya mfanyabiashara kijana ajinyonga

--
Afisa wa Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara, Mrakibu Msaidizi wa Polisi, Greyson Mahembe ambaye ni miongoni mwa maafisa saba wa jeshi hilo
Hakuna tena kesi hapo
 
Hivi tambaza la deki kweli tambaa la deki hebu fikiria tena tambaa la nini la deki

Sasa ukirudi kwenye kesi ya Zombe na wenzake kuna askari mmoja naye alijinyonga hivyo hivyo

Kuna kitu hapo kuna kitu huenda huyo jamaa ndio anajua siri zote

Bila ya kuwekwa tume huru ya uchunguzi kama ile ya Zombe kuna mtu ataangushiwa Zigo la dhambi hapo
Maadamu damu imelipa damu imebalance.zombi hayupo sawa.
Vihela vyenyewe mbuzi si wazame porini madini tele yamejaa.
Ukishaua mtu umewasha bluetooth on popote unanuka
 
Back
Top Bottom