Mtwara: Askari Polisi mmoja kati watuhumiwa wa mauaji ya mfanyabiashara alikutwa mahabusu akiwa amejinyonga tarehe 22 Jan 2022

Labda aliingia chooni au ni zam yake kudek na akijitafakari hajaua na pengine anaona famili yake itamuangaliaje na huku kesi aliangalia kabisa haiishi salama akaona bora atangulie akafanye kesi na Mungu huko
 
Dunia imeisha Maafisa wazito wa Polisi.
Wana amua kumwua raia kwa ajiri ya Milioni 33.
Hapo wakigawana kila Polisi anapata shilingi milioni 4 tu.

Afisa Mzima wa Polisi anaua raia kwa shilingi milioni 4.

Kama afisa wa Polisi anauwa mtu kwa milion 4, Private wa Polisi si atauwa mtu hata kwa kutaka kuiba Laki moja.

Hii ni fedheha kubwa kwa Jeshi la Polisi na hasa kwa
MAAFISA WAKE KUHUSIKA KATIKA MATUKIO YA UJAMBAZI WA KUUA MA KUPORA RAIA MALI ZAO.

Jamii ifahamu kuwa.

[emoji117]Tendo lolote Ovu ukimfanyia Binadamu mwenzako ni lazima litajulikane.
Usijidanganye kufikiri kuwa kuna uwezo wa kuto julikana.
Kwakuwa Mungu yupo na hiyo ni moja ya kazi yake.
Kuuweka uovu wa Mwanadamu hadharani ili sheria ichukue mkondo.
Huwezi kuua kiumbe cha Mungu na ukabaki salama.
Chukueni mfano wa Kijana aliyemchoma Mkewe na Mkaa Kigamboni.
Watoto walioua Wazazi wao kwa Siri Arusha na Moshi wote wametiwa nguvuni.

Tambua kuwa ukitenda uovu wowote uwe tayari kwa ghalama utakazo zipata kwakuwa ni lazima utajulikana.

Kwaherini.

Kwangu mimi Milioni 4 ni bajeti a kunywea bia tu, at least nimejibana sana kwa miezi mitatu.
Siwezi kumtukana hata mtu kwa ujira wa milioni 4

Najiheshimu na kuheshimu watu wote .
 
Mfumo wa ukamataji unawaruhusu polisi kutekeleza mauaji. Sheria ya kuwa na kibari cha ukamataji haina nguvu Tanzania.
 
Wote walikuwa wamelala usingizi wa PONOOOOO
 
Kumbe mhehe, ni kawaida.
 
Upo sahihi, chumba wamo wote, mmoja ajinyonge!
Mahabusu wa Mauaji huwezi waweka wote sehemu moja, watapangana namna gani ya kujitetea. Hao askari waliwekwa mahabusu tofauti, Mkuu wa Kituo akiwekwa LILUNGU, Aliyejiua akiwekwa Kituoni hapo polisi, OC CID alipelekwa Nachingwea nk nk. Ila kupata picha halisi ya kesi kama hizo watuhumiwa wanatenganishwa kwa umbali mkubwa tu na hakuna uwezekano wa wao kukutana mpaka mahakani. Ni possible kujiua. Kama ameawa basi kwa namna yoyote OCD, RPC na RCO watahusika tu.
 
Lakini hata hapo mtwara si kuna watu wengine? Au ndiyo alipewa kachumba kapekeyake na tambala la dekio likiwepo? Hapo kuna kitu kimejificha.
 
Lakini hata hapo mtwara si kuna watu wengine? Au ndiyo alipewa kachumba kapekeyake na tambala la dekio likiwepo? Hapo kuna kitu kimejificha.
Wauaji hawachanagamini na mahabusu wengine.
 
mara nyingi matambala ya kudekia huwa yanachaguliwa makuukuu yale yaliyochoka[emoji848][emoji848]
 
Huyu ndiye mwenye siri nzito ya sakata zima ebu tuwekeeni picha ya hilo tambala la deki alilotumia kujinyongea
Siku zote tambala huwa na majimaji ivyo kulifanya kuoza, sidhani kama linaweza kuhimili zaidi ya kilo 60 za mtu mzima, cha kujiuliza, je alikuwa peke yake? Kwanini awe peke yake?
 
Ebu jaribu kutumia tambala la deki uje utupe mrejesho.
Unapoambiwa tambala la deki unapata picha gani?
Napata picha ni nguo kuukuu ambayo napita picha haina uwezo wa kumbeba mtu mzima tena askari ikamnyonga
 
Mleta habari huyo mtu alijinyonga au amejinyonga.
Alikutwa au amekutwa!!
 


Leo zimetoka taarifa za mmoja kati polisi waliotuhumiwa kuua mfanyabiashara,kujiua lockup. Taarifa zinaeleza mahabusu huyu alijinyonga kwa kutumia dekio.

Napingana na hizi taarifa. Kwa uelewa wangu na mazingira nayoyajua mahabusu ni ngumu sana mtu kujinyonga. Kwanza hakuna uwezekano wa uwepo wa kitu cha kujinyongea. Pili hata kama mahabusu atatumia nguo zake bado uwepo wa mahabusu wengine kunaondoka uwezekano huo.

Natilia mashaka ripoti ya polisi. Kabla hatujasema kujinyonga kwa mchongo tunawataka polisi watoke tena watueleze kwa kina mtuhumiwa huyu amejinyongaje nyongaje.Tofauti na hapo tutaamini kuna syndicate.

Mods msiunge uzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…