Mtwara: Mapambano ya Polisi na Jambazi mwenye silaha; Raia ameuwawa, askari amepigwa risasi

Mtwara: Mapambano ya Polisi na Jambazi mwenye silaha; Raia ameuwawa, askari amepigwa risasi

GAZETI

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2011
Posts
5,286
Reaction score
6,736
Wakuu jioni hii hapa Newala(Mtwara) limetokea tukio la Jambazi mwenye silaha kuvamia kituo cha mafuta Kiduni na kupora fedha. Wakati anaondoka eneo la tukio kaua Raia mmoja, hata hivyo wananchi wenye hasira walimfuatilia jambazi huyu ambaye alishindwa kutoroka baada ya mtu mwenye pikipiki ambaye anasadikiwa kuwa ni mwenzake kuwahi kukimbia baada ya kuona mazingira yameshakuwa magumu.

Mpaka hivi sasa bado polisi wako msituni wakimsaka jambazi huyo ambaye anaonekana kuwa na ujuzi wa hali ya juu katika kutumia silaha, askari mmoja ameshapigwa risasi eneo la makalio na amekimbizwa hospitali, pia kuna tetesi kuwa askari wawili wameuwawa.

RAIA KUUWAWA: Hili ni la uhakika kwani nimeiona maiti kwa macho yangu

ASKARI KUPIGWA RISASI: Huyu aliyejeruhiwa nimemuona kwa macho yangu akikimbizwa, hospitali pia namfahamu ni dereva wa gari za polisi.

Sina uhakika na habari za kuuwawa kwa polisi ingawa zinazungumzwa sana na watu mbalimbali.

Tuwaombee mungu askari wetu wapate ushindi katika mpambano huo mgumu ukizingatia uwa kuna hali ya mvua na giza

Wakuu hakuna umeme nitarejea baadae kama kutakuwa na taarifa za uhakika.
 
Kwani kila anaekuwapo eneo la tukio lazima hawe na camera au kifaa chakupigia picha
 
Jambazi mmopja kuwashinda maaskari wengi ni uzembe mkubwa. Ovaaa!
 
ikumbukwe hata jambazi anaweza kuwa ni askari mzuri ila aliyekiuka maadili ya kazi
 
Dah! RIP raia, pole askari uliyejeruhiwa 0713! sijajua kivipi hilo jambazi limetarget ma------ au ulikuwa unasanda?
 
Nasisi raia tukiona sehem kunamatukio tusipende kukimbilia
 
poleni sana huko mtwara. huyo jambazi labda ni mmoja kati ya wale waungwana waliokamatwa wakipata mafunzo ya kikomandoo na cd za al-shabaab..
 
Kwa kuwasaidia Polisi, hao majambazi wapo nyuma yenu ndio maana wameweza kuwapiga risasi za makalio
 
Jambazi mmopja kuwashinda maaskari wengi ni uzembe mkubwa. Ovaaa!

Mkuu sijui kama utakumbuka tukio la ujambazi wa hela za nmb 2006 mataa ya Ubungo. Majambazi watatu kama sikosei walikuwa wanajeshi. Silaha kubwa za kivita na risasi zilivaliwa kama mkanda. Ukikutana na jambazi kama huyo hata muwe askari kumi ataweza kuwamaliza.

Yule traffic aliyejitahidi kupambana nao alupandishwa cheo na akapewa ofa ya kusoma ili apande zaidi. Nikikumbuka mkasa huu najiona wa kumshkuru sana Mungu maana wanafamilia yangu walikumbana nao.
 
poleni sana huko mtwara. Huyo jambazi labda ni mmoja kati ya wale waungwana waliokamatwa wakipata mafunzo ya kikomandoo na cd za al-shabaab..

Nilijua tu yataishia huko!
 
Huyo afande inaonyesha ni muoga alikuwa anakimbia mapambano ndio maana akapigwa risasi ya
 
Ni uhakika na wameshamuua mkuu wa upelelezi aitwaye Nurdin. Na bado wako at large majirani wasaidie taarifa.
 
Upolisi mgumu sana.

Ukiwa polisi maisha yako unakuwa umyaweka rehani kulinda wananchi na mali zao, lakini hao hao leo wanakuchukia na kukuona kama adui, majambazi nao wanakuchukia na kila kukicha viongozi wa chadema wanakuita mtu mbaya.

Poleni wafiwa
 
Back
Top Bottom