Waungwana naogopa mno ninapoona kuwa nasi JF tuna Tabia ya kutojali mambo yanayohusu maisha ya wenzetu.Utofauti wa Msomi na yule asiyeenda shule ni Ustaarabu na kujua ku-value Utu wa mwenzake.Suala la Mtafaruku wa Zanzibar tunaliangalia kwa upeo Mdogo,Kutakuja tokea matatizo ambayo tunaweza kabisa kuyatafutia Ufumbuzi Leo!.Viongozi wetu wana tabia ya kutojali kwa yale mambo wasioyapenda,Wameweza kuwakana Vijana huko Ukraine wakati Vigezo vyote vimeonyesha kuwa wao ndio waliwapa Go ahead ya kwenda kutafuta Elimu Huko.Leo wanapuuzia Muafaka(II) Kati yao na Chama cha CUF,Hii ni Hatari na linaweza kusababisha vifo!!!
Kwa wale mtakaokuwa na kumbukumbu nzuri,mtakumbuka kuwa Hotuba
ya kwanza ya JK Bungeni ile 30/Desemba/2005 ,alisema atatumia nguvu zake zote kumaliza matatizo ya Zanzibar!,Kama kawaida kaingia (Ikulu) madarakani na jukumu la Matatizo hayo kampa Kingunge na Makamba,Watu hawa hawapendi mabadiliko,wanataka kuona CCM ndio yenye kuongoza Daima,hata kama inakosa Ridhaa ya wananchi,wameshindwa kujenga mazingira ya Chama hichi kupendwa Pemba na Unguja,na ndiyo hiyo iliyoleta Mtafaruku wa kuuliwa watu kule Pemba (Enzi za Mkapa).Muafaka (I) Ulimalizika bila makubaliano,na huu Muafaka(II)Unaonekana unafikia ukingoni bila maamuzi ya maana!,Hali hii itakwenda hivi mpaka lini?.
Siku Muungwana JK alipomchagua Makamba kuwa Katibu Mkuu wa CCM alisema amemchagua ili akajibu mapigo ya Wapinzani!,Makamba anajibu mapigo kwa kiswahili cha mtaani,Uwezo wake wa kujadili mambo kwa kina ni Mdogo,yeye ni mtendaji zaidi kama askari polisi ,lakini sio Negotiator!!,Kwa Mtazamo wangu Mzee Mangula alikuwa mtu mwenye akili ya kuweza kuzungumza na kutatua matatizo kwa majadiliano lakini sio huyu Makamba!.Sasa tunarudishwa nyuma,na tunarudisha hali ya wenzetu Wazanzibari nyuma pia,kwa sababu wao ndio waathirika zaidi!.Muafaka huu umezungumzwa kwa miezi 8 bila kufikia makubaliano!,Nafikiri sasa ni muda Muafaka kwa jumuiya ya Kimataifa kuingilia kati kabla hali haijakuwa mbaya zaidi!.
Wanaoumia hapa sio Seif,Lipumba au hao CCM,wanaopata matatizo ni raia wa kawaida,kwani sehemu kama Pemba ambayo haina uwakilishi wa CCM imeachwa hata katika miradi ya Maendeleo.Waungwana Tuujali Utanzania wetu kuliko Itikadi za Vyama vyetu!!Balaa hili la CCM na CUF litaleta Mmomonyoko Mkubwa kwenye Muungano!,wale mnaomshauri JK,p/se mwambieni aende huko Zanzibar na kulifanyia kazi hili kwa Uwazi!!!Suala liwe Utanzania wake na sio Itikadi zake za Uccm!!
Ni Imani yangu kuwa tutalijadili hili kwa uwazi hapa tukijali UTAIFA wetu.Tuweke TAIFA mbele kabla ya Itikadi zetu za Vyama!.