Muafaka CCM na CUF, pande mbili za shilingi!

Muafaka CCM na CUF, pande mbili za shilingi!

Profesa Lipumba, CUF wanatafuta ufalme gani?

Chama cha Wananchi (CUF), kupitia kwa mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba, juzi kilitoa tamko kali la kushutumu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuhusu mwenendo wa mazungumzo ya mwafaka.

Mwenyekiti huyo alizungumza maneno mengi mno, hata akafikia wakati wa kuomba msaada wa jumuiya ya kimataifa, katika kuhakikisha kuwa mazungumzo ya mwafaka yanazaa matunda mazuri.

CUF wanaamini kuwa CCM ndio wanaokwamisha mwafaka huo, kwa maelezo kwamba wamefanya ghiliba kwa uhadaa ulimwengu.

Kwanza ni vema tukasema kwamba sisi hatufungamani na upande wowote katika suala hili, ilimradi tu pande zote- CUF na CCM - wanachotaka ni kuona Tanzania inaendelea kuwa nchi ya amani.

Kauli za Profesa Lipumba, si tu kwamba zinaamsha hisia za vurugu miongoni mwa wafuasi wa vyama hivyo, lakini ni kauli iliyojikita zaidi katika utashi wa propaganda za kisiasa.

Pengine CUF wanajua kwamba baada ya kuwepo mwafaka, hawatakuwa na jingine la kuwafanya wasikike.

Tunasema hivyo kwa sababu kwa muda wenyewe wa mazungumzo bado haujaisha. Profesa Lipumba kasema zimebaki siku saba. Ndiyo, siku hizo ni nyingi. Hata kama ingekuwa imebaki siku moja, bado siku hiyo ni muhimu.

Ndiyo maana tunaamini kuwa kabla ya kiongozi huyo kuzomoka na kuanza kutoa maneno ya kuwatisha wananchi, angesubiri kwanza aone hadi siku ya mwisho, kitu gani kitakuwa kimefanywa na CCM.

Profesa Lipumba amezungumza maneno makali, akitaka umma uamini kuwa Zanzibar ni kama Darfur.

Kwa kauli zake za kuomba msaada wa kimataifa, anataka kuonyesha kwamba Zanzibar sasa watu hata hawasaidiani chumvi. Hii si kweli.

Kwa kusema kwamba Rais Jakaya Kikwete amekuwa akitoa ulaghai, hasa kwenye hotuba yake ya Desemba, mwaka juzi, huko ni mkumvunja moyo kiongozi huyo aliyeapa kusimamia kidete upatikanaji mwafaka wa kudumu Zanzibar.

Kwa yeyote atakayesikiliza kauli ya Profesa Lipumba ya jana, atagundua kwamba hizi ni propaganda za kisiasa anazoeneza.

Hakuna anayezuia propaganda hizo, lakini zinapokuwa na mwelekeo wa kujenga au kuamsha hisia za chuki miongoni mwa Wanzanzibar na Watanzania kwa ujumla, hapo tutapinga.

Ni ukweli ulio wazi kwamba Zanzibar yapo matatizo ya kisiasa, lakini matatizo haya si ya kutisha kama Profesa Lipumba na chama chake wanavyotangaza.

Mazungumzo ya Mwafaka yanahitaji ustahimilivu, kuaminiana na kuweka mbele zaidi, maslahi ya nchi na wananchi.

Kwa hili tunapenda kumwambia Profesa Lipumba kwamba asilikuze mno. Mara zote Watanzania wamemaliza tofauti zao kwa njia ya mazungumzo. Kwa kuwa nia ya kumaliza matatizo ya Zanzibar ipo, na imeanza kuonyeshwa na viongozi wetu wa vyama viwili, basi tusubiri.

Kama Darfur wanakuja kwetu kutafututa mwafaka, hilo CUF hawalioni? kama kungekuwa na vita anyohubiri Lipumba, nani angekuja kuendesha vikao vya mwafaka hapa? Chonde Profesa Lipumba.

Maoni ya Mhariri: Mtanzania Agosti 8.
 
My blames are on CCM! Wanatumia mwafaka kujinufaisha kisiasa na si kuwanufaisha Wazanzibari na Watanzania. My questions are:-

1. Hivi mazungumzo gani ambayo huwa hayana deadlines?
2. Hivi Mwafaka wa kwanza uliotokana na uchaguzi wa 1995 na kusimamiwa na Jumuiya ya Madola chini ya usuluhishi wa chifu Anyouku nani aliyeuvuruga?/Hakuutekeleza? Na kwa nini hakuutekeleza? Mimi naamini ni CCM.

Am standing to be corrected. Nina mashaka makubwa sana kuwa kwa ujinga huu wa hawa Watawalw wetu, wanayachezea maisha yetu Watanzania tena kwa faida zao binafsi.Matokeo yake wanawapa hao CUF loophole ya kuanzisha kauli za ajabu-ajabu tena (nakumbuka ile ya Jino-kwa jina na Mapanga sha-sha-sha)

Ukweli kwangu ni dhahiri na hata Waangalizi wa Kimataifa walisema wazi kuwa Zanzibar uchaguzi haukuwa huru na haki na matokeo ya uchaguzi ni kielelezo kuwa bila CUF kushirikishwa kwenye uongozi wa Visiwa vya Zanzibar, Zanzibar itatawalika kwa Msaada wa Tanganyika tu au Majeshi toka nje!

Kisa cha hayo yote madaraka! Inauma sana!
 
Profesa Lipumba, CUF wanatafuta ufalme gani?

Chama cha Wananchi (CUF), kupitia kwa mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba, juzi kilitoa tamko kali la kushutumu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuhusu mwenendo wa mazungumzo ya mwafaka.

Mwenyekiti huyo alizungumza maneno mengi mno, hata akafikia wakati wa kuomba msaada wa jumuiya ya kimataifa, katika kuhakikisha kuwa mazungumzo ya mwafaka yanazaa matunda mazuri.

CUF wanaamini kuwa CCM ndio wanaokwamisha mwafaka huo, kwa maelezo kwamba wamefanya ghiliba kwa uhadaa ulimwengu.

Kwanza ni vema tukasema kwamba sisi hatufungamani na upande wowote katika suala hili, ilimradi tu pande zote- CUF na CCM - wanachotaka ni kuona Tanzania inaendelea kuwa nchi ya amani.

Kauli za Profesa Lipumba, si tu kwamba zinaamsha hisia za vurugu miongoni mwa wafuasi wa vyama hivyo, lakini ni kauli iliyojikita zaidi katika utashi wa propaganda za kisiasa.

Pengine CUF wanajua kwamba baada ya kuwepo mwafaka, hawatakuwa na jingine la kuwafanya wasikike.

Tunasema hivyo kwa sababu kwa muda wenyewe wa mazungumzo bado haujaisha. Profesa Lipumba kasema zimebaki siku saba. Ndiyo, siku hizo ni nyingi. Hata kama ingekuwa imebaki siku moja, bado siku hiyo ni muhimu.

Ndiyo maana tunaamini kuwa kabla ya kiongozi huyo kuzomoka na kuanza kutoa maneno ya kuwatisha wananchi, angesubiri kwanza aone hadi siku ya mwisho, kitu gani kitakuwa kimefanywa na CCM.

Profesa Lipumba amezungumza maneno makali, akitaka umma uamini kuwa Zanzibar ni kama Darfur.

Kwa kauli zake za kuomba msaada wa kimataifa, anataka kuonyesha kwamba Zanzibar sasa watu hata hawasaidiani chumvi. Hii si kweli.

Kwa kusema kwamba Rais Jakaya Kikwete amekuwa akitoa ulaghai, hasa kwenye hotuba yake ya Desemba, mwaka juzi, huko ni mkumvunja moyo kiongozi huyo aliyeapa kusimamia kidete upatikanaji mwafaka wa kudumu Zanzibar.

Kwa yeyote atakayesikiliza kauli ya Profesa Lipumba ya jana, atagundua kwamba hizi ni propaganda za kisiasa anazoeneza.

Hakuna anayezuia propaganda hizo, lakini zinapokuwa na mwelekeo wa kujenga au kuamsha hisia za chuki miongoni mwa Wanzanzibar na Watanzania kwa ujumla, hapo tutapinga.

Ni ukweli ulio wazi kwamba Zanzibar yapo matatizo ya kisiasa, lakini matatizo haya si ya kutisha kama Profesa Lipumba na chama chake wanavyotangaza.

Mazungumzo ya Mwafaka yanahitaji ustahimilivu, kuaminiana na kuweka mbele zaidi, maslahi ya nchi na wananchi.

Kwa hili tunapenda kumwambia Profesa Lipumba kwamba asilikuze mno. Mara zote Watanzania wamemaliza tofauti zao kwa njia ya mazungumzo. Kwa kuwa nia ya kumaliza matatizo ya Zanzibar ipo, na imeanza kuonyeshwa na viongozi wetu wa vyama viwili, basi tusubiri.

Kama Darfur wanakuja kwetu kutafututa mwafaka, hilo CUF hawalioni? kama kungekuwa na vita anyohubiri Lipumba, nani angekuja kuendesha vikao vya mwafaka hapa? Chonde Profesa Lipumba.

Maoni ya Mhariri: Mtanzania Agosti 8.

mhariri tumekuelewa ulipoegemea, na hujawa neutral kabisa katika kuhariiri hii habari, au mwenzetu akina Lowassa weshakupatia nofu, au ndio haya waliosema ndugu zetu wa kenya kuwa Rais arambwa miguu na waandishi wa habari tz na mimi nnaongezea kumbe na CCM pia imemiliki vyombo vingi vya habari
 
Nyie KAFU sijui CAFU na Nyie SISIEM ......CCM Jamani wekeni mambo wazi...Mna tu koroga!! Hivi hamjui Kwamba Kuna Mechi Ya Msumbiji Na Tanzania Hivi karibuni!! Tume jiandaa Vipi!!


Basi Kafu Iwe Msumbiji alafu CCM iwe Tanzania..Basi atakae shinda siku hiyo Ndio Mshind Milele..au Mna semaje!!


Ha- Ha!! Punguzeni Makerere!!
 
Kwa sababu mavichwa yenu yanadhani mpaka mtu wa nje ndio anaweza kuwasaidia kupatana haya Marekani wamesema rudini basu kwenye kikao basi.


Mareakani yawaonya wanaovuruga muafaka
*Balozi ahimiza mazungumzo yahitimishwe


*Asema serikali ya Mseto ni suala la msingi

*Asema amani ya Tanzania inatikiswa

Na Andrew Msechu

SUALA la muafaka wa kisiasa visiwani Zanzibar ambao upo katika hali ya kulegalega, limechukua sura mpya baada ya Balozi wa Marekani Tanzania kuonya watu wanaotaka kuuvuruga.

Akizungumza mara baada ya mkutano wake na waandishi wa habari katika ubalozi huo, balozi huyo, Michael Ratzer, alisema ni vema Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF) vikafikia makubaliano katika mazungumzo hayo yaliyodumu kwa miezi minane sasa.

Alisema ni muhimu maridhiano baina ya pande mbili hizo yakafikiwa haraka kabla hali kisiwani humo haijawa mbaya na akasisitiza kuwa kuna umuhimu wa kuunda serikali ya mseto ili kumaliza mizozo ya kisiasa visiwani humo.

Hatua hiyo imekuja huku kukiwa na utata baina ya pande mbili zinazoshiriki mazungumzo hayo, CUF na CCM, ambapo wakati CUF wamekuwa wakilalamikia mizengwe na kuibuliwa kwa madai mapya nje ya mazungumzo ya vyama hivyo, CCM wamekuwa wakidai kuwa CUF ndiyo wanaogomea kuendelea na mazungumzo hayo.

Hata hivyo, mwanzoni mwa wiki hii CUF walitoa msimamo wao wa kutoendelea na mazungumzo hayo na kuomba msaada wa jumuiya ya kimataifa kuingilia ili kuhakikisha hali ya kisiasa inatengemaa visiwani Zanzibar.

CUF wanadai kuwa pamoja na jitihada zao za kumwandikia Rais Jakaya Kikwete, kutaka aingilie kati mvurugano uliojitokeza katika mazungumzo, Rais amekaa kimya, jambo ambalo wamelitafsiri kuwa ameukataa wito wao.

CUF wanasema itakapofika Agosti 15, mazungumzo hayo yatakuwa yamekufa rasmi na kwamba viongozi watatoa mlolongo wa mazungumzo hayo na viongozi wa CCM tangu yalipoanza Januari mwaka huu.

Awali akiwakaribisha wanafunzi waliokuja kujitolea kwa ajili ya kusaidia kutoa huduma za jamii na kujifunza hali ilivyo katika maeneo ya Karagwe na Pemba, Balozi Retzer, alisema ingawa Tanzania imekuwa na historia ya kuwa kisiwa cha amani, bado imekuwa ikikutana na matukio ya uvunjaji amani, ikiwamo matukio ya kisiasa.

"Kwa sasa tatizo linaloonekana kuwepo ni suala zima la kisiasa Zanzibar, tatizo hili bado halijapatiwa ufumbuzi, lakini tuna matumaini kuwa serikali ya CCM na uongozi wa Chama cha CUF watafikia makubaliano kupitia mpango unaoendelea kabla ya tarehe ya mwisho waliyojiwekea, ambayo ni Agosti 15," alisema Retzer.

Akitoa ufafanuzi juu ya njia nzuri inayoweza kutumiwa kumaliza matatizo hayo mara baada ya mkutano huo, Balozi Retzer alisema kutokana na hali halisi ya matokeo ya uchaguzi ambao umekuwa ukivigonganisha vyama hivyo viwili, ni jambo zuri iwapo utakuwepo uwezekano wa serikali ya mseto, ikiwa ni njia muhimu kumaliza matatizo yaliyopo.

"Unapokuwa na uchaguzi ambao unavigawanya vyama viwili kwa uwiano unaokaribiana wa uwakilishi, ni vyema kuhakikisha kuwa watu wote wanapata nafasi ya uwakilishi serikalini, suala la serikali ya mseto inayounganisha pande hizo ni muhimu, hii inaonyesha umoja wa kitaifa," alisema.

Aliongeza kuwa ni vizuri inapofikia hatua kama hiyo kuungana kwa ajili ya maslahi ya wananchi wa maeneo mawili yenye uwakilishi kwa serikali kuhusisha na kuingiza watu wa upinzani.

Alitoa mfano wa namna ambavyo vyama viwili vya kisiasa nchini Marekani vyama vya Republican na Democrat, ambavyo mara kadhaa vimekuwa vikijikuta vikigawana matokeo kwa asilimia zinazokaribiana hivyo kwa kujali maslahi ya wananchi hulazimika kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa.

Alisema ni vema kuangalia uwezekano huo wa kuungana na kujumuisha uwakilishi wa sehemu hizo mbili zenye mgongano ili kulinda maslahi ya wananchi waliopiga kura bila kujali itikadi.

Hata hivyo alisisitiza kuwa anaamini kuwa pande hizo mbili zitamaliza tofauti zilizojitokeza na kufikia maelewano mapema.

Wanafunzi hao 26 waliokaribishwa na balozi huyo nchini jana wanatarajiwa kufanya kazi za kujitolea katika maeneo ya Pemba na Karagwe kwa ushirikiano na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Marekani ni nchi pekee duniani ambayo ilikataa kuyatambua matokeo ya uchaguzi kisiwani Zanzibar mwaka 2005, ikisema kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za uchaguzi.

Hata hivyo, mazungumzo ya kutafuta muafaka baina ya vyama hivyo viwili yaliyoanza Januari mwaka huu, yalilegeza msimamo wa nchi hiyo dhidi ya uchaguzi wa Zanzibar kiasi kwamba Rais George Bush, alimkaribisha kwa mazungumzo Rais Jakaya Kikwete jijini New York mapema mwaka huu.
 
Na Andrew Msechu

SUALA la muafaka wa kisiasa visiwani Zanzibar ambao upo katika hali ya kulegalega, limechukua sura mpya baada ya Balozi wa Marekani Tanzania kuonya watu wanaotaka kuuvuruga.

Akizungumza mara baada ya mkutano wake na waandishi wa habari katika ubalozi huo, balozi huyo, Michael Ratzer, alisema ni vema Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF) vikafikia makubaliano katika mazungumzo hayo yaliyodumu kwa miezi minane sasa.

Alisema ni muhimu maridhiano baina ya pande mbili hizo yakafikiwa haraka kabla hali kisiwani humo haijawa mbaya na akasisitiza kuwa kuna umuhimu wa kuunda serikali ya mseto ili kumaliza mizozo ya kisiasa visiwani humo.

Hatua hiyo imekuja huku kukiwa na utata baina ya pande mbili zinazoshiriki mazungumzo hayo, CUF na CCM, ambapo wakati CUF wamekuwa wakilalamikia mizengwe na kuibuliwa kwa madai mapya nje ya mazungumzo ya vyama hivyo, CCM wamekuwa wakidai kuwa CUF ndiyo wanaogomea kuendelea na mazungumzo hayo.

Hata hivyo, mwanzoni mwa wiki hii CUF walitoa msimamo wao wa kutoendelea na mazungumzo hayo na kuomba msaada wa jumuiya ya kimataifa kuingilia ili kuhakikisha hali ya kisiasa inatengemaa visiwani Zanzibar.

CUF wanadai kuwa pamoja na jitihada zao za kumwandikia Rais Jakaya Kikwete, kutaka aingilie kati mvurugano uliojitokeza katika mazungumzo, Rais amekaa kimya, jambo ambalo wamelitafsiri kuwa ameukataa wito wao.

CUF wanasema itakapofika Agosti 15, mazungumzo hayo yatakuwa yamekufa rasmi na kwamba viongozi watatoa mlolongo wa mazungumzo hayo na viongozi wa CCM tangu yalipoanza Januari mwaka huu.

Awali akiwakaribisha wanafunzi waliokuja kujitolea kwa ajili ya kusaidia kutoa huduma za jamii na kujifunza hali ilivyo katika maeneo ya Karagwe na Pemba, Balozi Retzer, alisema ingawa Tanzania imekuwa na historia ya kuwa kisiwa cha amani, bado imekuwa ikikutana na matukio ya uvunjaji amani, ikiwamo matukio ya kisiasa.

"Kwa sasa tatizo linaloonekana kuwepo ni suala zima la kisiasa Zanzibar, tatizo hili bado halijapatiwa ufumbuzi, lakini tuna matumaini kuwa serikali ya CCM na uongozi wa Chama cha CUF watafikia makubaliano kupitia mpango unaoendelea kabla ya tarehe ya mwisho waliyojiwekea, ambayo ni Agosti 15," alisema Retzer.

Akitoa ufafanuzi juu ya njia nzuri inayoweza kutumiwa kumaliza matatizo hayo mara baada ya mkutano huo, Balozi Retzer alisema kutokana na hali halisi ya matokeo ya uchaguzi ambao umekuwa ukivigonganisha vyama hivyo viwili, ni jambo zuri iwapo utakuwepo uwezekano wa serikali ya mseto, ikiwa ni njia muhimu kumaliza matatizo yaliyopo.

"Unapokuwa na uchaguzi ambao unavigawanya vyama viwili kwa uwiano unaokaribiana wa uwakilishi, ni vyema kuhakikisha kuwa watu wote wanapata nafasi ya uwakilishi serikalini, suala la serikali ya mseto inayounganisha pande hizo ni muhimu, hii inaonyesha umoja wa kitaifa,” alisema.

Aliongeza kuwa ni vizuri inapofikia hatua kama hiyo kuungana kwa ajili ya maslahi ya wananchi wa maeneo mawili yenye uwakilishi kwa serikali kuhusisha na kuingiza watu wa upinzani.

Alitoa mfano wa namna ambavyo vyama viwili vya kisiasa nchini Marekani vyama vya Republican na Democrat, ambavyo mara kadhaa vimekuwa vikijikuta vikigawana matokeo kwa asilimia zinazokaribiana hivyo kwa kujali maslahi ya wananchi hulazimika kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa.

Alisema ni vema kuangalia uwezekano huo wa kuungana na kujumuisha uwakilishi wa sehemu hizo mbili zenye mgongano ili kulinda maslahi ya wananchi waliopiga kura bila kujali itikadi.

Hata hivyo alisisitiza kuwa anaamini kuwa pande hizo mbili zitamaliza tofauti zilizojitokeza na kufikia maelewano mapema.

Wanafunzi hao 26 waliokaribishwa na balozi huyo nchini jana wanatarajiwa kufanya kazi za kujitolea katika maeneo ya Pemba na Karagwe kwa ushirikiano na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Marekani ni nchi pekee duniani ambayo ilikataa kuyatambua matokeo ya uchaguzi kisiwani Zanzibar mwaka 2005, ikisema kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za uchaguzi.

Hata hivyo, mazungumzo ya kutafuta muafaka baina ya vyama hivyo viwili yaliyoanza Januari mwaka huu, yalilegeza msimamo wa nchi hiyo dhidi ya uchaguzi wa Zanzibar kiasi kwamba Rais George Bush, alimkaribisha kwa mazungumzo Rais Jakaya Kikwete jijini New York mapema mwaka huu.

..is this linked to war on terror?just wondering,real!
 
ewe mola hakika unamjua mwenye nia njema na zanzibar na unamjua mwenye nia mbaya na zanzibar,mfedheheshe na mpe laana kila mwenye nia ya kuleta machafuko zanzibar,na umjaalie asifanikiwe na ufisadi wake, na mpe nguvu anaeitakia mema zanzibar,na umdhihirishe watu wamjue.amin.inshallah mungu atatunusuru na kila balaa. after all fainali kaburini
 
Jembajemba, na Under_age,

Maneno ya Mwanagenzi yana ukweli ambao wengi whawaukubali lakini dio hivyo!

Inawezekana Maalim Seif katofautiana na Profesa? Maalim yuko wapi? Kama yeye ni kiongozi wa timu ya CUF katika mazungumzo haya nadhani ingefaa azungumze yeye kama alivyodai Makamba. Inawezekana Maalim siku hizi karidhika kwani SMZ inamtunza! Kwa hiyo hana haraka kama wenzie

Hivi huyu mtu alikuwa akitafuta muakafaka na CCM kwa ajili gani hasa?.. majuzi tu wajumbe wa mikutano hiyo walianza kujitenga na yeye bado alikuwa upande wa ku - support mazungumzo zaidi, why?..

Sasa haya ndio maneno na nadhani sasa hivi mtanielewa naposema kwamba Seif Sharrif sii kiongozi mzuri mwenye kuitakia mema Zanzibar!.
 
"Every gun that is made, every warship that is launched, every rocket fired signifies in the final sense a theft from those who hunger and are not fed, those who are cold and not clothed" – Eisenhower
 
Mnyamwezi Lipumba amebebeshwa mzigo mzito, pamoja na kwamba wanyamwezi ni hodari wa kubeba mizigo mizito lakini huu muda si mrefu Mnyamwezi ataushindwa.

CUF chama cha kitaifa chenye focus kubwa Zanzibar... yenye 2.8% ya Watanzania wote...

Sitashangaa mambo yasipoenda vizuri Lipumba akapigwa chini kama akina James Mapala.
 
Muafaka wa nini wakati sera zao ziko tofauti? CCM wawe CUF au CUF kuwa CCM? Toka mwanzo sikuona dalili ya suluhu kwani CUF inaongozwa na viongozi waliowahi kuwa ndani ya CCM na wanajua kuichachafya, je CCM itakubali kuwasikiliza wakati wanawaona kama waasi. Ukweli CUF ni chama kizuri kijijenge bila kutegemea CCM na wananchi tutawaunga mkono. Wafanye kazi ili baadhi ya wanCCM wa ndani bara(Tanganyika) wajiunge nao ili upinzani huko pia uwe kama Zenji na ndipo demokrasia ya kweli itpatikana na miafaka itakoma
 
Msavila,

Ndugu yangu kwanza tuwaogope CCM kama ndio watawala!..
Hawa jamaa wamepandikizia kila chama wanafiki wake ambao utawaona wakisha shtukiwa tu hurudi nyumbani. Hizi mbegu chafu zimepandikizwa kila chama na usidhani kama kuna ushindani kichama sasa hivi labda baadaye baada ya muundo mpya wa Katiba. Hakuna kipya na wala hapatakuwa na kipya kama Katiba mbovu bado itaendelea kukumbatiwa.
Viongozi wote wa vyama vya Upinzani wanaweza kuwa na nia nzuri lakini tukumbuke kuwa CCM sii mchezo mdogo. Matumaini yangu makubwa ni ktk kizazi hiki kipya ambacho mmeweza kuonyesha mengi mazito ambayo sijawahi kuyasikia toka kwa wazee wetu.
Nchi imejawa na hofu kubwa ktk kizazi hiki na hakika ni muungano pekee ambao unaweza kurudisha hadhi ya nchi yetu.
Jana Usiku mzima nilikaa nikiyasoma mahojiano ya Nyerere ambayo Mzee Mwanakijiji aliyaweka ktk moja ya mada zetu. Nikamsikitikia sana marehemu baba wa Taifa kama angeweza kuitupia jicho Tanzania ya leo na ile alokuwa akiizungumzia, yaani tofauti kabisa hasa pale aliposhupalia kuwa Azimio la Arusha haliwezoi kufa!
Ndio maaana Kingunge alipiga kelele mwaka jana wakati Mbowe aliposema anataka kufuata nyayo za baba wa Taifa, akidai kuwa Mbowe hamjui Nyerere wala hawezi kulingana nae!..
Kwa kuisoma hotuba ile niligundua mengi mazito ambayo CCM leo hii haitaki kabisa yawe historia ya taifa letu. Na ni kati yao hao hao wana CCM ambao humpaka mavi mwalimu kiasi kwamba leo hii kuna baadhi yetu tunaamini kila ninaloandikwa kubadilisha historia.
 
haya tena jamani kesho ndio 15/aug siku ya mwisho ya maongezi,sijui kutakuwa na nn ...........YANGU MACHO TU.
 
Tamko gani hilo na deadline ni kesho!Au tunataka kuonyeshana Ubabe sasa!Nani mwenye nguvu?.Kwa mtindo huu hatutofika salama,kwa sababu tunashindwa kuziba ufa mdogo na sioni uwezo wa kujenga Ukuta.
 
JK awasihi CUF wasivunje mazungumzo
Asema muafaka ni kwa maslahi ya taifa
NA MWANDISHI WETU (Uhuru)
RAIS Jakaya Kikwete amewasihi viongozi na wanachama wa CUF wasikubali mazungumzo ya kutafuta muafaka wa kisiasa Zanzibar yavunjike.
Katika taarifa aliyoitoa jana kwenye vyombo vya habari, Rais Kikwete alisema gharama ya kuvunjika kwa mazungumzo hayo ni mbaya.
"Nawasihi wenzetu wa CUF tuungane kuhakikisha tunafanikiwa. Tusikubali mazungumzo yavunjike kwani gharama ya kuvunjika kwa mazungumzo haya ni mbaya na haina maslahi kwa taifa letu na watu wake. Itahatarisha amani na utulivu wa nchi yetu," alisema Rais Kikwete.
Alisema ni muhimu kwa CCM na CUF kuendelea kuzungumza ili kupata ufumbuzi wa tatizo, la sivyo nchi itarudi kwenye uhasama, shutuma zisizoisha, kubaguana, kutozikana, kutosalimiana na kuchekeana.
"Tunazungumza kwa sababu tuna tatizo tunalolitafutia ufumbuzi. Kuacha kuzungumza si jawabu kwani tutakuwa tunaacha kulipatia ufumbuzi tatizo linalotusibu sote. Tutarudi kule tulikokuwa, yaani kwenye uhasama, shutuma zisizoisha, kubaguana, kutozikana na hata kutosalimiana au kuchekeana," alionya Rais Kikwete.
Alisema iwapo jawabu la tatizo halitapatikana kwa mazungumzo kuvunjika kutakuwa na muendelezo wa utamaduni mbaya wa kuzifanya tofauti za kisiasa kuwa ni chanzo cha uadui, chuki na hivyo kuhatarisha amani, utulivu na umoja wa taifa.
"Sisi wa upande wa CCM, hatudhani kama tumefikia mahali pa kusema kuwa mambo yameshindikana na hivyo mazungumzo yavunjike," alisema.
Alisisitiza: "Hatujafikia hatua hiyo hata kidogo. Ni maoni yangu na ya Chama Cha Mapinduzi kuwa, tuendelee kuzungumza na kila upande uboreshe hoja zake za kuushawishi upande mwingine."
Alisema ukomo wa mazungumzo utokane na ridhaa CUF na CCM kwa kuridhika kuwa, ajenda zote zimepata nafasi ya kujadiliwa kwa kina, na kuelewana.
Alisema kinyume na hivyo, ni kuahirisha tatizo litakalojitokeza baadaye na kudhuru taifa siku za usoni.
"Tunafanya yote hayo ili kujihakikishia amani, utulivu, mshikamano na umoja wa taifa letu na watu wake vinaendelea kuwepo daima dumu," alisema.
Chimbuko la mazungumzo hayo, ni ahadi aliyoitoa Rais Kikwete alipolihutubia Bunge, Desemba 30, 2005.
"Niliahidi kuwa, nitakuwa tayari kuchukua hatua za kutafuta ufumbuzi wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar. Kwa ajili hiyo, nilielezea nia yangu ya kusaidia kuanzisha na kuwezesha mjadala juu ya mustakabali wa kisiasa Zanzibar," alisema Rais Kikwete.
Alisema ahadi hiyo aliitoa kwa dhati akiamini hakuna tofauti zozote za kisiasa na kijamii ambazo haziwezi kumalizwa kwa mazungumzo.
Rais Kikwete alisema kwamba kamati ya mazungumzo ya muafaka inayohusisha wajumbe kutoka vyama hivyo, ilikaa Februari mosi mwaka huu na kutengeneza ajenda ya pamoja ya mazungumzo.
Alitaja mambo matano ambayo yalikuwa katika ajenda hiyo kuwa ni uchaguzi mkuu wa Zanzibar wa Oktoba 30, 2005 na taathira zake, usawa na haki katika kuendesha siasa na masuala ya utawala ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Mambo mengine aliyataja kuwa ni njia za kuimarisha mazingira ya maelewano ya kisiasa na uendeshaji wa uchaguzi huru na wa haki Zanzibar na utaratibu wa kutekeleza programu ya utekelezaji wa makubaliano yatakayofikiwa katika mazungumzo hayo.
Alisema tangu mazungumzo yaanze Januari mwaka huu, kamati imefanya vikao 12 na kutumia siku 43 za mazungumzo, wakati makatibu wakuu wa vyama hivyo wamekutana mara mbili kutafuta ufumbuzi wa yale mambo yaliyohitaji kufanywa nao.
Alifafanua kwamba, walikubaliana mazungumzo ya msingi yatafanywa na kamati, lakini pale ambapo kamati itakwama, makatibu wakuu wataingilia kati kutoa mwongozo.
Alisema tangu wameanza mazungumzo, makatibu wakuu wamekutana mara mbili na hiyo ni dalili kwamba mambo yanakwenda vizuri.
Rais Kikwete alisema kati ya ajenda tano; tayari tatu pande zote mbili zimefikia maelewano mazuri na kuzitaja kuwa ni usawa na haki katika kuendesha siasa, masuala ya utawala ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na njia za kuimarisha mazingira ya maelewano ya kisiasa na uendeshaji wa uchaguzi huru na wa haki Zanzibar.
Taarifa kamili ya Rais Kikwete, kuhusiana na mazungumzo ya muafaka kati ya CCM na CUF iko ukurasa wa 10
 
Back
Top Bottom