Teamanaconda
JF-Expert Member
- Jun 21, 2013
- 602
- 564
Ahsante sana kiongozi,umenipa somo ambalo hapo kabla nilikuwa silijuhi,ubarikiwe sanaMadhehebu ni mafundisho, maadili na matendo ya ibada yaliyo ya msingi katika dini fulani. Ni makundi ndani ya dini fulani ambayo yanatofautiana bila ya kuvunja umoja wa msingi. Madhehebu mbalimbali ya dini ileile yanaweza kushindana hata kupigana vita. Kwa kifupi madhehebu ni mapokeo ya ufahamu kunako dini husika. Wakati alipoishi
Yesu Kristo, dini ya Uyahudi ilikuwa na madhehebu yaliyoshindana sana, hasa Masadukayo, Mafarisayo na Waeseni lakini wote walibakia kuwa ni dini ya uyahudi japokuwa walikuwa wanatofautiana kwa mengi.
Wafuasi wa dini ya Ukristo, kutokana na wingi wao katika urefu wa historia na upana wa jiografia, wamegawanyika katika madhehebu mengi, kuanzia Kanisa Katoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki hadi makundi elfu kadhaa ya Uprotestanti na ushirika wa Anglikana na yanazidi kuongezeka siku kwa siku lakini wote wanabakia katika njia kuu ya UKristo ispokuwa mapokezi yao yametofautiana kwa baadhi ya vitu.
Sasa katika uislamu kuna mikondo mitatu mikubwa ambayo ni Sunni-Waljamaa, Shia na Wahabiyya ambao ni Answar Sunna. Shia ndani yao wamegawanyika katika makundi mengi zaidi.
Sunni-waljamaa kuna madhehebu au madhhab manne yanayokubaliwa rasmi. Wahabiyya wao walianza kujiita Answar Sunna' ni dhehebu ndani ya Sunni lililo vuka mipaka katika sheria za dini. Sunni wote wanafanya Mawlid ispokuwa hao 'Wahabiyya au Answar sunna' ambao kwasasa nao wamegawanyika ndani yake kuna dhehebu la 'Salafy Swaleh' ambalo lina misimamo mikali zaidi na sheria zao ni kali zaidi wao wanajihusisha na mambo ya itikadi zaidi (Tawhid).
Kwa hivyo Mawlid hupingwa na Wahabiya na sio Sunni.
Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app