mkuu ni njia ip ya kuondoa sumu mwilini inayo tokana na kutumia dawa za Mseto kwa mda mrefu na antibiotics? kama dawa za typhod na UT????
Kuna supplements za aina mbalimbali huweza kuondoa sumu kwa hara sana,supplements hizi ni gharama kiasi.Lakini kwa kuwa hapa siko kibiashara,nitakushauri utumie vyakula tu kuondoa sumu.
1.Kunywa juisi ya green leafy vegetables(juisi ya mboga mbichi za majani) kama celery na spinach glasi 1 kwa siku.
2.Kunywa juisi ya matunda yenye mchanganyiko wa karoti,parachichi,apple na stafeli glasi moja kwa siku.
3.Pendelea kutumia chai ya tangawizi kila siku asubuhi.
4.Kunywa maji safi na salama angalau lita 2 kwa siku.
5.Kunywa glasi moja ya maji vuguvugu yaliyochanganywa na limao 1 kila siku alfajiri baada ya kuamka na kabla hujala chochote.Hata ukifanya hivi angalau mara 3/4 kwa wiki inatosha.
Kuna vyakula vingi sana vinavyoweza kufanya kazi hiyo,lakini nimekuwekea baadhi tu.Pia pendelea kufanya mazoezi kama vile kukimbia taratibu mpaka jasho litoke angalau mara 3 kwa wiki.Medical system haziwezi kuwashauri watu kufanya hivi kwa kuwa watakosa wateja wa kununua dawa zao.
Huu ni ushauri wa bure kwa kila mtu.Ukitaka kujua ukweli huu,basi fanya kwa vitendo haya ninayosema yote halafu jilinganishe afya yako kabla na baada ya kuanza utaratibu huu baada ya mwezi mmoja.