Ni muda tu ndio unawapa kiburi ukichanganya na vyeo. Wanadhani wamejificha sana na pengine wanadhani wayafanyayo hayajulikani.
Kwanza hakuna jambo baya na zuri kama system. Matendo huhifadhiwa na kuwekwa rikodi. System inaendeshwa na binadamu ambao ni dhaifu vile vile.
Hawa viongozi wetu iwe kwa MAKUSUDI AU KWA BAHATI MBAYA WANAFUMBIA MACHO malalamiko tena mengine yapo kisheria na kikatiba.
Iweje leo watawala hawana habari kabisa kwamba watumishi hawajapewa stahiki zao za kisheria za kupandishwa madaraja na mishahara kila baada ya muda kwa zaidi ya miaka 3 hivi.
Iweje leo watawala kwa zaidi ya miaka minne wamezuiya mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa na maandamano halali ambayo yapo kisheria na kikatiba kama si kiburi tu na hadaa ya muda?
Iweje leo watawala wanafumbia macho wavurugaji wa haki za wananchi kwenye Chaguzi mbali mbali za marudio na ule wa Mitaa bila kuulizwa lolote kama si kiburi tu na kuhadaliwa na vyeo na muda?
Iweje leo serikali iamuwe kujitoa kwenye ile itifaki za uwazi na ukaguzi kwenye jumuiya ya kimataifa kama si nia ovu na kutaka isiwajibike? na sasa kuna huo mpango wa kutaka kujitoa kwenye Haki za Binadamu kwenye Umoja wa Afrika? iweje kama si kiburi tu na nia mbaya?
Iweje srikali itumie nguvu za chama kutunga sheria ya kudhibiti habari, na kupata habari na kutumia kisingizio cha sheria hizo zilizotungwa kwa nia mbaya kudhibiti wakosoaji kama si kiburi cha watawala wakati wanajuwa KATIBA imetoa ruhusa ya kupata habari?
Kwamba kinachoendelea cha kuwatesa na kuwasumbuwa wapinzani wasifanye siasa na kukipendelea chama cha CCM wazi wazi bila kuchukuliwa hatua watendaji, kuwatesa kwa kuwakamata kupitia Polisi na Mamlaka za kiserikali nyengine eti iwe si kiburi na kuhadaliwa na muda tu ?
WASICHOJIFUNZA WATAWALA.
Hawajifunzi kwamba wao sio wa kwanza kufanya haya na kwamba wakati utawaumbuwa. Hawajifunzi somo la wakati na vyeo kuwa ni la kupita na muda utawaacha mkono baadae.
Hawajifunzi kuwa walikuwepo waliofanya haya kabla yao na historia iliwahukumu na leo tunasoma kwenye vitabu uchafu wa aina hio.
Hawajifunzi kuwa mwanadamu ana ukomo wa uvumilivu na ikifika huko hata hio sytem inayowapa kiburi huwageuka na kuanza kuwashughulikia.
Hawajifunzi kuwa Taifa linalindwa na KILA MMOJA WETU na sio system pekee yenye wajibu na uwezo wa kuilinda nchi. Nchi inalindwa na umoja wetu na mshikamano hili wanalijuwa kweli ?
Hawajifunzi kuwa nchi za wenzetu zilifanya makosa kama haya, watawala walidharau na kuyadogosha makosa yao, walijisahau kuwa makosa madogo ndio huzaa makosa makubwa na chuki hupandikizwa kwa kudharau na baadae huonekana kuwa mazoeya. Watawala hawajui kuwa watu wameumizwa kwa hii miaka minne na wana chuki wamezifundika kwenye nafsi zao. Wao wanahadaiwa na vyeo wakidhani watu wamesahau?
MWISHO.
Watawala mnayo nafasi ya kujifunza na mnayo nafasi ya kurekebisha bado. Kadiri siku zinavyokwenda ndio level ya ongezeko la tatizo inakuwa itafika wakati kujirekebisha kwenu itakuwa vigumu. Tambueni wanaoumia ni binadamu vile vile
Watawala tambuweni Watanzania wana vipaumbele vya kudumu vya umoja na mshikamano , Kamwe msithubutu kucheza na maeneo ambayo yatamongonyoa tunu hizo. Jitafakarini kama haya yanayofanywa na AWAMU YA TANO yanawakikishia WATANZANIA uwepo wa tunu hizo. Wataalamu wetu wa USALAMA fanyeni tafiti.
Tulipofika sipo mahali salama na kamwe msijaribu amani yetu kwa udhaifu wenu wa kutoona uhalisia.
MAAJABU
Maajabu ya awamu ya TANO ni kule kudhani kwamba yote yanayofanyika kwamba wananchi hawayajui, Dunia haijuwi, wasomi hawajui na kwamba eti wamejifungia kama kisiwa kwa hio watendayo eti hayajulikani.
Haya maajabu yasingemuweka Hitler kwenye kumbukumbu leo kwa uwezo aliokuwa nao.
Rejeeni makosa ya wakati na vyeo muone yalivyowagharimu waliopita kabla yenu.
Wakati wa kujirekebisha ni sasa.
Kishada.
Kwanza hakuna jambo baya na zuri kama system. Matendo huhifadhiwa na kuwekwa rikodi. System inaendeshwa na binadamu ambao ni dhaifu vile vile.
Hawa viongozi wetu iwe kwa MAKUSUDI AU KWA BAHATI MBAYA WANAFUMBIA MACHO malalamiko tena mengine yapo kisheria na kikatiba.
Iweje leo watawala hawana habari kabisa kwamba watumishi hawajapewa stahiki zao za kisheria za kupandishwa madaraja na mishahara kila baada ya muda kwa zaidi ya miaka 3 hivi.
Iweje leo watawala kwa zaidi ya miaka minne wamezuiya mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa na maandamano halali ambayo yapo kisheria na kikatiba kama si kiburi tu na hadaa ya muda?
Iweje leo watawala wanafumbia macho wavurugaji wa haki za wananchi kwenye Chaguzi mbali mbali za marudio na ule wa Mitaa bila kuulizwa lolote kama si kiburi tu na kuhadaliwa na vyeo na muda?
Iweje leo serikali iamuwe kujitoa kwenye ile itifaki za uwazi na ukaguzi kwenye jumuiya ya kimataifa kama si nia ovu na kutaka isiwajibike? na sasa kuna huo mpango wa kutaka kujitoa kwenye Haki za Binadamu kwenye Umoja wa Afrika? iweje kama si kiburi tu na nia mbaya?
Iweje srikali itumie nguvu za chama kutunga sheria ya kudhibiti habari, na kupata habari na kutumia kisingizio cha sheria hizo zilizotungwa kwa nia mbaya kudhibiti wakosoaji kama si kiburi cha watawala wakati wanajuwa KATIBA imetoa ruhusa ya kupata habari?
Kwamba kinachoendelea cha kuwatesa na kuwasumbuwa wapinzani wasifanye siasa na kukipendelea chama cha CCM wazi wazi bila kuchukuliwa hatua watendaji, kuwatesa kwa kuwakamata kupitia Polisi na Mamlaka za kiserikali nyengine eti iwe si kiburi na kuhadaliwa na muda tu ?
WASICHOJIFUNZA WATAWALA.
Hawajifunzi kwamba wao sio wa kwanza kufanya haya na kwamba wakati utawaumbuwa. Hawajifunzi somo la wakati na vyeo kuwa ni la kupita na muda utawaacha mkono baadae.
Hawajifunzi kuwa walikuwepo waliofanya haya kabla yao na historia iliwahukumu na leo tunasoma kwenye vitabu uchafu wa aina hio.
Hawajifunzi kuwa mwanadamu ana ukomo wa uvumilivu na ikifika huko hata hio sytem inayowapa kiburi huwageuka na kuanza kuwashughulikia.
Hawajifunzi kuwa Taifa linalindwa na KILA MMOJA WETU na sio system pekee yenye wajibu na uwezo wa kuilinda nchi. Nchi inalindwa na umoja wetu na mshikamano hili wanalijuwa kweli ?
Hawajifunzi kuwa nchi za wenzetu zilifanya makosa kama haya, watawala walidharau na kuyadogosha makosa yao, walijisahau kuwa makosa madogo ndio huzaa makosa makubwa na chuki hupandikizwa kwa kudharau na baadae huonekana kuwa mazoeya. Watawala hawajui kuwa watu wameumizwa kwa hii miaka minne na wana chuki wamezifundika kwenye nafsi zao. Wao wanahadaiwa na vyeo wakidhani watu wamesahau?
MWISHO.
Watawala mnayo nafasi ya kujifunza na mnayo nafasi ya kurekebisha bado. Kadiri siku zinavyokwenda ndio level ya ongezeko la tatizo inakuwa itafika wakati kujirekebisha kwenu itakuwa vigumu. Tambueni wanaoumia ni binadamu vile vile
Watawala tambuweni Watanzania wana vipaumbele vya kudumu vya umoja na mshikamano , Kamwe msithubutu kucheza na maeneo ambayo yatamongonyoa tunu hizo. Jitafakarini kama haya yanayofanywa na AWAMU YA TANO yanawakikishia WATANZANIA uwepo wa tunu hizo. Wataalamu wetu wa USALAMA fanyeni tafiti.
Tulipofika sipo mahali salama na kamwe msijaribu amani yetu kwa udhaifu wenu wa kutoona uhalisia.
MAAJABU
Maajabu ya awamu ya TANO ni kule kudhani kwamba yote yanayofanyika kwamba wananchi hawayajui, Dunia haijuwi, wasomi hawajui na kwamba eti wamejifungia kama kisiwa kwa hio watendayo eti hayajulikani.
Haya maajabu yasingemuweka Hitler kwenye kumbukumbu leo kwa uwezo aliokuwa nao.
Rejeeni makosa ya wakati na vyeo muone yalivyowagharimu waliopita kabla yenu.
Wakati wa kujirekebisha ni sasa.
Kishada.