Muda wa ajira kwa baadhi ya kada za Serikalini uwe mfupi

Muda wa ajira kwa baadhi ya kada za Serikalini uwe mfupi

RingaRinga

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2015
Posts
1,047
Reaction score
521
Tatizo la ajira serikalini limekuwa sugu sana.
Ajira ni mojawapo ya keki ya taifa inayofaa kufaidiwa na wote wanaostahili.
Sasa nashangazwa na utaratibu wa serikali wa kuwang'ang'ania watumishi wa serikali hadi watimize umri wa miaka 60 ya kuzaliwa.
Kuna baadhi ya kada kwa kuzingatia wingi wa mahitaji na udogo wa athari ya kustafu mapema zinafaa kurekebishiwa umri wa kustaafu.
Ntataja moja tu,

UALIMU WA SHULE ZA MSINGI

Kada hii ina wahitimu wengi sana ukilinganisha na kada yoyote. Lakini pia haina athari kubwa ikiwa watumishi wake watastaafu kwa hiari au lazima kwa umri wa miaka 45.
Hii itawapa fursa pia kutumia walichochuma kuwekeza kny ufugaji, kilimo au mambo mengine wakiwa bado na nguvu.

Sheria ya pension irekebishwe ili hao watakaohiari kutoka wakiwa na umri huo iwahusu.
Makato yao ya pensheni yanaweza kuwa makubwa ili yawasaidie wakati wowote watakapostaafu, ni swala la makubaliano tu.
Liwe ni chaguo la ama uende na mkataba wa sasa au huo mpya.
Lakini nafasi za ajira zitolewe nyingi kny mikataba ya muda mfupi.
Sidhani kwa hali ya sasa kwa vijana waliosubiri kuajiriwa kwa miaka 5 au zaidi haitawafaa.
Wengine wanalazimika kujitolea kwa kulipwa laki mbili kwa mwezi bila increment wala nyongeza.
Hii itasaidia kundi kubwa lililoko nje kuajiriwa kwa idadi kubwa kuliko ilivyo sasa.
Muda wa kusubiri ajira utakuwa mdogo ukilinganisha na sasa.
 
Kupunguza tatizo la ajira ni kuzipa misuli sector binafsi na sio kupunguza ambao wameajiriwa .


Mtu mmoja makini akiwezeshwa anaweza akawaajiri watu 100.

Usifikirie kuhusu mtu Ku retire at the age of 45

Maana mshahara wa Mwalimu hauzidi 500K-2M Kwa 99% sasa unafikiri anabidi ajiandae vipi kustaafu .

Sector binafsi ndo zinaweza kubadilisha maisha ya watz
 
Tatizo la ajira serikalini limekuwa sugu sana.
Ajira ni mojawapo ya keki ya taifa inayofaa kufaidiwa na wote wanaostahili.
Sasa nashangazwa na utaratibu wa serikali wa kuwang'ang'ania watumishi wa serikali hadi watimize umri wa miaka 60 ya kuzaliwa.
Kuna baadhi ya kada kwa kuzingatia wingi wa mahitaji na udogo wa athari ya kustafu mapema zinafaa kurekebishiwa umri wa kustaafu.
Ntataja moja tu,

UALIMU WA SHULE ZA MSINGI

Kada hii ina wahitimu wengi sana ukilinganisha na kada yoyote. Lakini pia haina athari kubwa ikiwa watumishi wake watastaafu kwa hiari au lazima kwa umri wa miaka 45.
Hii itawapa fursa pia kutumia walichochuma kuwekeza kny ufugaji, kilimo au mambo mengine wakiwa bado na nguvu.

Sheria ya pension irekebishwe ili hao watakaohiari kutoka wakiwa na umri huo iwahusu.
Makato yao ya pensheni yanaweza kuwa makubwa ili yawasaidie wakati wowote watakapostaafu, ni swala la makubaliano tu.
Liwe ni chaguo la ama uende na mkataba wa sasa au huo mpya.
Lakini nafasi za ajira zitolewe nyingi kny mikataba ya muda mfupi.
Sidhani kwa hali ya sasa kwa vijana waliosubiri kuajiriwa kwa miaka 5 au zaidi haitawafaa.
Wengine wanalazimika kujitolea kwa kulipwa laki mbili kwa mwezi bila increment wala nyongeza.
Hii itasaidia kundi kubwa lililoko nje kuajiriwa kwa idadi kubwa kuliko ilivyo sasa.
Muda wa kusubiri ajira utakuwa mdogo ukilinganisha na sasa.
Ungekuwa wewe umeajiriwa ungekuja na mawazo haya? Huyo mtu unayemzungumzia hapo kaa ukijua wengi wanawatoto na wanamikopo ambayo imewafikisha hapo.Unachotakiwa kujua ni kutambua nafasi yako na kutumia akili yako kupambana, ukiwa na mentality ya keki ya taifa, hata ya kwako ya birthday italiwa!!!
 
labda tuseme mda wa kustaafu kwa lazima ushushwe hadi 45
 
Ukipata nafasi ya kuajiriwa utakuja kufuta h mada yako
 
Hao walimu uluowataja zaidi ya 90% wamezaliwa 1980 kuja 1998.

Wapo Hadi 2040......

So kuanzia 2035 uaona taasisi kibao za umma Zina vibabu na vibibi ......
 
Back
Top Bottom