Mufti amuombea msamaha ustadhi aliyechapa viboko watoto wadogo bila huruma

Mufti amuombea msamaha ustadhi aliyechapa viboko watoto wadogo bila huruma

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Sheikh Mkuu na Mufti wa Tanzania, Sheikh Dkt. Abubakar Zuber Bin Ally ametumia mashindano ya kusoma na kuhifadhi Qur-an Tukufu kumuombea msamaha mwalimu wa Madrasa, Mussa Bashiri, aliefikishwa mahakamani akikabiliwa na mashtaka ya kuwafanyia ukatili wa kuwachapa viboko watoto wawili wenye umri wa miaka 6 na 9 na kuwasababishia madhara.

"kiukweli nilisikia kuna mwalimu wa madrasa amefikishwa mahakamani kwa kosa la kuchapa watoto wa madrasa hivyo nitumie nafasi hii kuwaomba wazazi na umma wa Watanzania msameheni tuchukulie alipitiwa lakini nitoe wito kwa walimu wote kuacha kuwa wakali kwa watoto wa madrasa hata hivyo sisi kama mabaraza la Waislamu tumekuwa tukitoa semina kwa walimu kuhusu namna yakuwafundisha watoto wetu"~Abubakar zuber mufti wa Tanzania
1740310921881.png
 
Iyo kikubwa zaidi safi sana sheikh hana hatia kama hutaki mwanao kuchapwa basi mtafutie sheikh afundishwe nyumbani huku akiwa anaangalia tv
 
Kosa lake lipo pale pale hakuna msamaha hapo,tusiendekezee vitendo hivyo kwa kigezo Cha msamaha
 
Kosa lake lipo pale pale hakuna msamaha hapo,tusiendekezee vitendo hivyo kwa kigezo Cha msamaha
Kwaiyo akipigwa shule iko pw akipigwa na sheikh ndo mnakuja juu sheikh yupo sawa anapambania dini ya mungu na mungu yupo naye sawa toto lako lichelewe madrasa kwakuangalia tv alafu unataka asipigwe
 
Back
Top Bottom