naam amezungumzia waislam kuchukua juhudi katika kusoma na sio kuendelea kulalama/
kwa kweli amekuwa jasiri kusema ukweli ambao unatakiwa ufahamike waislamu tuliowengi, kuwa hakuna free lunch
"Huu ni muda mwafaka kwa waislamu kuanza kujikita na kukazania zaidi suala la elimu, na si kubaki kulialia pekee kuomba kuchaguliwa na kupewa vyeo serikalini, hivyo tuchangamke tusiendelee kubaki nyuma tupige hatua kama wenzetu," alisema Mufti.
source: mjengwa.blogspot.com
Huyu sheikh Mufti tunamjua kwamba ni moja ya idara ya serikali inayowakilisha mtazamo wa serikali kuhusu waislamu. wewe pamoja na mufti nawaomba niwaulize :-
a. Utaendeleza shule kwa michango ya waumini? Ni kiasi gani unataka walipe kama waislamu kuchangia elimu ya watoto wao?
b. Kodi na vifaa vya endeshaji pesa utazipata wapi?
c. Uwezo wa kifedha kwa waislamu wengi unajulikana ni wa kusikitisha kama sio kuhuzunika (Kwa ufupi wengi ni maskini) sasa hizo pesa za ujenzi wazitoe wapi wakaibe???
d. Sawa tunaweza kupata ufadhili wa kujenga shule kutoka kwa waarabu au matajiri wa kiislamu nchini? Ila kama ilivyo misikiti mingi Tanzania kuendesha misikiti na mashule sio kama kuiendesha nyumba yako Mtu wa Pwani ni kwamba inahitajika a stable working capital kuhakikisha msikiti au shule inaendeshwa kwa umakini.
Hivyo ijapokuwa umesoma fikiria vilevile waislamu hawalalamiki kama wajinga bali to promote fairness na equality the government needs to subsidies them. MOU ya Kanisa na Serikali ndio iliyoleta shule nyingi za wakristo, kama mnakumbuka shule za seminari ziliibuka kama uyoga miaka ya 90s. Sasa jiulize kwanini, siamini na kwasababu najua kuwa si michango ya waumini pekee imechangia kukua kwa hizi shule bali na kwa msaada wa serikali pia.
Nyerere anachukiwa na waislamu kwasababu mojawapo ya sababu alichangia kwa kiasi kikubwa kuvunjika kwa EAMWS. EAMWS ilikuwa ni jumuiya yenye kuwaunganisha waislamu sunni, shia, ismailiya na wengineo kwa lengo la kuwaendeleza waislamu kielimu. Kumbuka kipindi kile waislamu wengi walikuwa ni wafanyabiashara ya kilimo, utumwa, meli waliona kuna haja ya jumuiya ya kiislamu nayo iendelee kielimu. Hivyo basi wakawa wameanzisha jumuiya hiyo kuleta maendeleo kwa waislamu. Vilevile kumbuka kipindi cha miaka 1945 wakoloni walikuwa wakifanya kazi kwa kupitia missionaries kusambaza dini na elimu. Waislamu walikuwa wanatakiwa kubadili dini ili waweze kusoma shule za wamisionaries (kama huamini waulize watu kutoka Tanga babu zao na bibi zao watakuambia ndio maana Tanga utakuta mtu mdogo wake muislamu kaka mkristo na kuendelea).
EAMWS ilikuja kama mbadala wa wamisionaries kwani ilikuwa na network Tanzania nzima kupitia waalimu wa vyuo,tariqa na jumuiya za kiithnasheri ambao walitapakaa Tanzania nzima. Hivyo wakaweka mikakati ya kuwa na elimu ya kidunia na ya kidini ili kuwanyanyua waislamu ambao wengi walikuwa hawapati huduma kutoka shule za missionaries. Mikakati hii ilifanikiwa na mwaka 1964 Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan Bin Ameir Al-Shirazi alienda Lebanon, Egypt, Iraq, Syria na kufanikiwa kupata grant ya karibu pound milion 55 za kiegypt wakati ule kuja kuanzisha CHUO KIKUU cha kwanza Tanzania. Ilipofikia hapo Nyerere akaona ni tishio na vilevile tishio kwa wakristo kwa vile waislamu wataanzisha chuo kikuu.
Hivyo basi tunaifahamu wengine vizuri Bakwata na ni bora tu tuiache itangaze inavyojisikia ila inajulikana kama taasisi ya serikali kwani akina Sheikh Abdallah Chaurembo, Sheikh Adam Nasibu, na wengineo wengi kwa msaada wa serikali (kwani serikali iliwaona ni waislamu walioelimika mpaka wakasifiwa katika magazeti ya Uhuru na Radio Tanzania) ndio walioshiriki kuiua hii jumuiya.
Hivyo Mtu Pwani soma historia vizuri kwani through history you can define your future. Usifikirie waislamu wanalalamika tu kama wendawazimu, chunguza kwanza.