Afrika mashariki wote wamekubaliana kuwa mwezi ukionekana popote katika hizi nchi 3 basi wafunge na kufungua pamoja.
Hiyo taarifa haipo ndugu yangu kuwa Kenya au Uganda mwezi umeandama.
UK kwa nini tuufuate mwezi wao?
Ikiwa hii ni hoja yafaa kufahamu kuwa ibada za kiislamu ni za kimaumbile. Zinafuata maumbile ya mwezi na jua kwa maana ya nyakati.
Vipi napo kwenye nyakati za swala inatubidi tufuate mwenendo wa Jua la UK? Kwamba kule ikiwa adhuhur tutangaziwe sisi tuswali adhuhur pia
Unajua haki si kumwangalia mtu!
Haki ni kile anachokisema ni sahihi?
Inawezekana mtu akazungumza ukweli lakini haiondoi kuwa ana sifa ya uongo.
Bakwata ni wazunguaji kwenye mambo mengi tu!
Lakini kwenye suala la mwezi wanavyolisimamia ndivyo kwenye vitabu vya fiqh limeandikwa hivyo hivyo kama wanavyolisimamia.
Hivyo rai yangu, tusome dini na tuache mkumbo.
Kwa sababu kwenye mahakama ya Allah atusimamishwa wewe kama wewe na kuhukumiwa wewe kama wewe.