MUGALU: Persona Non Grata

Umejificha kwa ID bandia halafu unakazana umecheza mpira ,nani anakujua hapa? Kama vipi jitambulishe wewe ni nani weka na picha tutakufahamu tu.
Hii ni platform ya kutambulishana au kutoa maoni ?
Kwanini usijitambulishe wewe kwanza alaf uniambie na mimi nijitambulishe ?
Alaf mbona kama umepatwa na Jazba kidogo nini tatizo ?

Jibu tafadhari.
 
Sijawahi ona mshambuliaji wa hovyo kama mugalu!!!!dakika zote 90 anafanya kazi ya kutafuna big G na kubutua mpira nje!aende yanga ndio kunamfaa kwa wacongo wenzie
 
Mtamkataa huyo dube muda mwalimu
 
Dube hana kiwango cha kucheza Simba, muacheni aendelee kuimprove huko Azam

Bahati mbaya yenu mnaompendekeza Dube labda mmemuona katika mechi hizo za akina Yanga, Gwambina etc ila jamaa ni wa kawaida sana

Kuhusu Mugalu, Kocha anakaa na wachezaji muda mwingi zaidi kuanzia mazoezini mpaka kwenye mechi ila sisi mashabk tunamuona mchezaji ktk muda wa mechi tu tena dakika zisizozidi 90,,,,sasa hiki sio kipimo sahihi cha kusema eti Kagere ni bora zaidi ya Mugalu
 
Hii ni platform ya kutambulishana au kutoa maoni ?
Kwanini usijitambulishe wewe kwanza alaf uniambie na mimi nijitambulishe ?
Alaf mbona kama umepatwa na Jazba kidogo nini tatizo ?

Jibu tafadhari.
Mimi sina ninachotakiwa kuprove,wewe umedai ulicheza mpira ,ili tukuamini kwamba ulicheza mpira inabidi uthibitishe.Katika sheria na kanuni ,ukitoa madai fulani inabidi uthibishe kwa ushahidi.Mimi sidaiwi ushahidi kwakuwa sija assert chochote .Thibitisha madai yako kwamba ulicheza mpira.
 
Unazijua Sheria za Jamiiforum ?
Na Kanuni zake?
Au ndio unaingia mjini wakati huu ?
 
Mwalimu hawezi kumchukua mwanafunzi anayejibu maswali mengi darasani akamuacha mwenye trend nzuri ya kuongoza mitihani ya mihula /katikati au mwisho wa mwaka.

Ni sawa na jamii inasema X ni mwizi na mzazi wa X anasema X si mwizi mbona anasali/anaswali sana.

Kwenye mazoezi inawezekana anafanya vyema ila kwenye kuyatumia aliyojifunza hawezi,HATUFAI
 
Mtamkataa huyo dube muda mwalimu
Prince Dube hadi sasa ndiye mfungaji bora wa ligi yetu ya VPL.
Pia hao mastraika wa Simba msimu huu hawajawahi kuifunga Yanga ktk mechi ya VPL, Dube kaifunga.
Kumbuka goli la kuisawazishia Yanga lilifungwa na Beki Onyango na sio Straiker wa Simba.
Dube anayafanya hayo Mambo akitokea Majeruhi ya kuvunjika mkono ktk mechi ya kwanza na Yanga.
Ina maana hajacheza mechi nyingi na timu yake la sasa hivi angekuwa na magoli mengi zaidi.
Mi naenda kwa vigezo vya takwimu za uwanjani.
Kwa wecheza mpira wanamjua Price Dube ni nani.
 
Dube laini sana mdau utarudi tena hapa kuleta malalamiko
 
Tunataka mchezaji wa kuonyesha uwezo caf na sio ligi ya ridhaa
 
Dube laini sana mdau utarudi tena hapa kuleta malalamiko
Dube laini...!
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Laini kivipi hebu fafanua.
Au unataka acheze pira Gwalide la Prison na Atipolo....!
Pila la kisasa ni la kunyumbulika braza.
Ukiwa mgumu unavunjika nyonga.

Unamkumbuka mchezaji aliyeingia Sub kwa Kaizer Chief siku ya mechi
na Simba kwa Mkapa ?
Alivoguza tu mpira akashikwa na Msuli akatolewa nje kimoja.
Shauri ya Ugumu
 
Weee nae mbona unaongea utopolo sasa ata uyo kocha akikaa na mchezaji anampima vipi kiwango chake kama sio uwanjani ndani ya hizo dakika 90

Kila mchezaji anapimwa uwanjani ndani ya dakika 90 ambazo mashabiki ndo wanaziona sio mazoezi au kwenye vyumba vya kubadili nguo
 
Mugalu tulisema mapema sana kwamba hajui kufunga lakini alipata watetezi kwamba anakaa na mpira,
Kazi za kukaa ni mipira awaachie akina Miquisson na Chama yeye afunge magoli,
Kingine Simba inabidi wapate beki wa kuwasaidia Kapombe na Tshabalala pale wanapochoka
 
Ndugu usidanganyike kwenye mashindano ya club bingwa afrika mpaka sasa hakuna namba 9 kafunga goli tatu ,anayeongoza ni winga anazo goli NNE na namba 9 wazuri wote wanazo 2 ,nimaloze kusema club bingwa afrika ni ngumu kwa namba 9 wote
 
Itakuwa ni kwer umechez mpira umeongea point
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…