Muhimbili: Mgonjwa Aliyeacha Deni na Kupata Bima Hatotibiwa kwa Bima, Bali kwa Malipo ya Fedha Taslimu

Nani kasema bima itumike kulipa deni la nyuma.

Hoja ya msingi ni utu. Deni liendelee kuwa deni hadi pale atakapo pona alilipe.

Na bima itumike kwasasa ili aendelee na tiba.

Inahitaji degree kujua hili

Umesema mwenyewe hapa πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡
 
System lazima igome, huwezi badili category wakati una deni.
Ndugu bima si mali ya Muhimbili.

Mgonjwa hadaiwi na bima.

Bima ni mfumo wa malipo ambapo Muhimbili italipwa kutokana na kutoa huduma.

Hali ilivyo, muhimbili hawamwambia alipe deni.

Bali wanaokataa malipo kwa matibabu ya sasa kupitia bima.

How comes mgonjwa yuko na bima lkn Muhimbili wanahitaji cash ili atibiwe.

Ongea kama mtanzania unajua haki ya kodi unayotumia inapaswa kurudi kwa watz wenzio wasio na uwezo ktk mambo gani ya msingi.

Mwenge?
Goli la mama?
Kuwanunulia condom na mafuta vilainishi na kuwapa tiba ya bure waratibu?
Kutoa tiketi za bure kwa washabiki wa mpira.?
Kutoa mabilioni ya pesa kuwapa viongozi wa dini?
Kununua maV8?
Kupeleka nje ya nchi (tour) wasanii na kuwapa mikopo?
Kuwalipia wagonjwa wote wanaokata rufaa ya uhai wao ktk hospitali za rufaa?
Kutengeza mabango nchi nzima.?
Kukopa pesa nje na kupita madeni ya zamani.? List ni ndefu
 
Bima sio kwaajili ya kulipa madeni unayodaiwa huko nyuma.

Clear madeni yako na upate huduma. Kumbukumbu na record zako za matibabu zipo.

Huna haja kuja kupotosha wala kujaribu utapeli kwenye mambo obvious.

Sio vizuri na sio sawa kujaribu kufanya wema na ukarimu wa matabibu wa hospitali ya Muhimbili kuwa ukatili.

Hii maana yake ni kwamba, matabibu wa hospitali ya Muhimbili wasingemtibu wakati huo huyo mgonjwa hana pesa ya matibabu, nadhani mtoa hoja ungekuja hapa na upotoshaji mwingine wenye sura nyingine wa kiwango cha juu zaidi.

Ni muhimu kua na shukrani kwa hata kidogo tu.
Gentleman, hata hiyo bima aliyonayo mgonjwa wako hivi sasa, bilashaka yoyote ni ushauri kutoka kwa matabibu wa hospitali ya Muhimbili. Kuwa muungwana, kua na shukrani tafadhali gentleman.

Tuwape maua yao kwa hospitality waliyonayo wazalendo hawa kwa wagonjwa wetu mbalimbali.

Friends, ladies and gentlemen,
Simulizi ya muungwana mtoa hoja inamaanisha jinsi gani matabibu wa hospitali ya Muhimbili wanavyothamini afya na uhai wa waTanzania, na kwamba mgonjwa wake mtoa hoja alikua akitibiwa hata pale alipokua hana pesa kwa ahadi ya kuja kulipa baadae.

Ama kwa hakika ubinadamu kazi.
Na shukran ya punda ni mateke. Mateke kwa hospital ya Muhimbili diyo haya sasa πŸ’

Mungu Ibariki Tanzania
 
Hayo unayotaka yanafanyika Kanisan ndugu! This world is Brutal Mdogo wangu, na haswa kwa wanaume, ukijua hayo ujue upo vitani, Pambana!
Sasa kwanini serikali wanapeleka pesa makabisani bila kuombwa.

Na kuacha wajibu wa kuwapa haki raia wake za msingi.

Kumbuka kama ilivyo haki kwa raia kupiga kura. Ni hivyo hivyo ni haki kwa raia kutibiwa, kupata elimu nk.

Kwanini kifungu gani cha katiba serikali isiyo na dini inaamua kuzitunuku taasisi za dini pesa.

Na wewe unataka wagonjwa waende kanisani kutafuta haki yao ya kutibiwa.

My poor country people
 
Ndugu elewa.

Kuna njia mbili za kuchangia huduma za matibabu Muhimbili.

1. Cash
2. Bima.

Muhimbili hawahamuamuru mgonjwa alipe deni la nyuma.

Na mgonjwa hajataka kulipa deni la nyuma kwa kutumia bima.

Hoja ni kwamba mgonjwa pamoja na deni aliyonalo ana haki ya kupewa option yyt kuendelea na tiba.

Muhimbili ni hospitali ya Ummah. Lkn kwasasa zinaendeshwa kama provate.


Mgonjwa kutoka jamii masikini anawekewa vikwazo kama kwamba yuko private hospital.

Mgonjwa ana haki ya kuandaa na tiba kwa kuchangia kupitia bima, na sio kama sera ya sasa kuwa mgonjwa bora afe lkn kama hana cash hatopata tiba ktk hospitali inayoendeshwa kupitia kodi yake.

My poor country people try to understand your rights

Vaa mikoba ya mgonjwa.

Pesa ya kuwalipia watz masikini ipo lkn iko missuse.

Naamini Magufuli huko aliko anawalilia watz masikini.

Na anajutia maamuzi mengine makubwa aliyoyafa
 
Viongozi wanathibitisha ule usemi mwenye shida hamjui mwenye njaa.

Wao wanalipiwa kila kitu, kula, kulala, mavazi, malazi, makazi, umeme, maji, posho, mishahara minono na bado humo humo WANATUIBIA.

Hawajui kula na vipofu.
 

Tofautisha:

#fact
#Truth
#Right thing

Mwenye Mamlaka ndo anaamua!
 
Hilo tuongee na yule aliyekuwa anajigaragaza kwenye matope
 
Pole sana kwa huyo mgonjwa na pole sana kwako kwa maumivu uyapatayo.

Masikini wa kipato na akili ambao ndio waathirika wakubwa wa mfumo ovu na hovyo wa CCM ndio wanakuwa chawa wakubwa wa CCM na viongozi wake.

CCM si chama cha siasa tena,ni genge la unyang'anyi wa rasilimali za Mtanzania kwa mgongo wa siasa.
 
Mkurugenzi wa MNH ni Prof. Janabi.

Je umewahi kufikiri kuwa ana moyo unaodunda kama sisi? Serikali inajifaidisha kupitia afya za Watanzania

Hatuna serikali bali wauaji
 
Lipeni deni achani kumbwelambwela hapa,

ingekua hana haki angetibiwa kipindi chote alichotibiwa? ama matabibu wa hospitali ya Muhimbili wangekua hawafahamu hilo wangemtibu kweli for hatakama hamna shukran kwa hilio?

nivae viatu vya gonjwa gani, nimemuuguza baba yangu mzazi ocean road tangu 2008 ameaga dunia Dec 2019 akiwa anatibiwa kwa bima, na expenses kidogo nje ya bima tulishirikiana na ndugu jamaa na marafiki kuzikabili..

My father was very free,
As whole familie tupo kazini, akijiskia vibaya wala hatusumbui, anakwenda hospital mwenyewe baadae kabisa akiona hawa jamaa wameshatoka makazini, ndiyo ana tuarifu vijanaa wake, kwamba yupo amelazwa hospitali Fulani. Hiyo ni faida ya Bima ya afya.

Kwa huyo mgonjwa wenu, kwakua nyinyi ndugu, jamaa, na marafiki zake mpo hai na mna uwezo. There is no escape root or room hata mtie huruma namna gani gentleman .

Jikusanyeni, jichangeni muende mkacleare deni la nyuma la mgonjwa, na aweze kupata huduma. Otherwise mnamfedhehesha sana na kwakweli mnamkatisha tamaa sana.

Kumbuka,
Mifumo inasomana sasa hivi, huwezi kuposha wala kudanganya chochote gentleman.

Sijui uende hospitali ya Amana, temeke ama mwananyamala au wapi utakapoona inafaa, through system utaonekana tu. Na status ya ugonjwa na madeni yako itajulikana tu.

Hakuna haja ya kuja kuonyesha fahari kwenye msiba kwa kutoa rambirambi ya milion 10, wakati laki8 ulikua mbishi mlalamishi.

Hiyo ni useless na completely nonsense πŸ’
 
Hiko unachotaka kifanyike wewe ni FRAUD.

Naomba nikueleweshe jambo moja, mgonjwa huwa anakuwa na namba moja tu ya file popote pale anapotibiwa, iwe dispensary, kituo cha fya, au hospitali.

Maisha yako yote utatibiwa kwa namba ileile, uwe unatumia cash au bima. Kama ulikuwa unatibiwa kwa cash, siku ukipata bima basi watachange category kwenye system then unaendelea na matibabu and viceversa.

Sasa huwa kuna exceptions, kama mgonjwa uliondoka ukiwa na deni, system itaendelea kusoma unadaiwa kwa miaka yotee. Na kama ulikuwa unatumia cash, system haitakubali kubadili category mpaka ulipe hilo deni kwanza.

Unachotaka kifanyike wewe hakiwezekani, na kama ingekuwa ivo basi wengi wangekuwa wanakimbia na madeni, kisha wakirudi wanafungua namba mpya ya file wanaendelea kutibiwa, which is FRAUD.

Hivyo siyo kwamba wamekataa bima, la hasha. Bali sheria haziruhusu kufanya ivo, na wakifanya ivo unavyotaka wewe akija CAG lazima waliwe kichwa.
 
Nimekuelewa kuwa una uchungu,una hoja nzuri na ni vema ukaiwasilisha kwa waziri wa afya,badala ya kumtuhumu Mama kuwa hajali wanyonge.
 
CCM ni sawa na ukoo wa Omari All Bongo wa Gabini
 
Kwani we mzee unatakaje, unataka deni lipotee? Akishatibiwa na Bima deni la nyuma je? Au unataka Bima ilipe deni la nyuma?

Ndugu wachenge walipe deni la zamani alafu mgonjwa asajiliwe kama mgonjwa wa Bima
 
Tofautisha:

#fact
#Truth
#Right thing

Mwenye Mamlaka ndo anaamua!
Hii ni shida ya kutojua haki na mipaka ya watendaji wa serikali.

Serikali ni sisi wananchi ktk nchi inayojipambanuabnibya kdemokrasia. Watendaji wa serikali hufanya kazi kwa mahitaji, ustawi wa wanachlkn kuna utawala wa Kleptocracy.

Bila ya shaka aina hii ya kiumbe wa mfano wako unathibitisha tunatawaliwa na mfumo wa Kleptocracy
 

Tofautisha:

#fact
#Truth
#Right thing

Mwenye Mamlaka ndo anaamua

Naona roho ya Mtikila ndani yako, Pambana Kaka, sisi wito wetu ni kutafuta Pesa ya halali na amani, Asante!
 
Kwani we mzee unatakaje, unataka deni lipotee? Akishatibiwa na Bima deni la nyuma je? Au unataka Bima ilipe deni la nyuma?

Ndugu wachenge walipe deni la zamani alafu mgonjwa asajiliwe kama mgonjwa wa Bima
Mgonjwa atibiwe. Ndio kazi ya kodi. Kazi ya kodi si kwa faida ya watumishi wa serikali pekee.

Akishapona atalipa deni.

Iweje mama Samia anadai wagonjwa madeni wanaofata wapate tiba.

Utu huu kujifunza wapi.

Vp mzee Janabi mnakubali kuongiza taasisi kwa kudhulumu wanaolipa mshahara.

Kiongozi muadilifu hujiuzulu.

Roho yangu inaniambia serikali kuna wahalifu wengi walijivika nguzi ya kondoo.

Nilitarajia kilemba ni alama ya utu na huruma.
 
Nimekuelewa kuwa una uchungu,una hoja nzuri na ni vema ukaiwasilisha kwa waziri wa afya,badala ya kumtuhumu Mama kuwa hajali wanyonge.
Mkuu wa Mkoa alisema, akikosea mama ni sawa Uislamu umetukanwa.

Ni kweli ushungi ilipaswa kuwa ni alama ya utu, huruma na mfano kwa jamii.

Ni bahati mbaya serikali yake inafanya kazi sawa na itikadi ya serikali. Wao hawana dini.

Nimewaelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…