Muhimu kufahamika katika wasifu wa Julius Nyerere

Muhimu kufahamika katika wasifu wa Julius Nyerere

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Nikijibu maswali niliyopokea kuhusu kitabu cha wasifu wa Mwalimu Nyerere:

Abdul Katalango kuwa na ustahamilivu kwani kazi yeyote ya mikono ya binadamu haiwezi kukosa kasoro.

Hawa waandishi ni wa ngazi za juu sana katika kiwango chochote kile na jamii itanufaika sana kwa kazi hii yao.

Kuna mengi wameyaeleza ya Mwalimu mimi sikuwa nayajua lakini yapo mengi yamewapita na huu ni ubinadamu.

Nimekuwa narashiarashia Vol. 1 ya kitabu kinamueleza Mwalimu alivyofika Dar es Salaam 1952 aliikuta TAA katika hali gani ya siasa.

Bahati mbaya TAA Political Subcommitee (Kamati Ndogo ya Siasa) iliyoundwa 1950 iliyokuwa inashauriwa na Earle Seaton haikutajwa.

Wajumbe wake walikuwa Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdulwahid Sykes, Hamza Mwapachu, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, Steven Mhando na John Rupia.

Kitabu kinaeleza kuwa Nyerere alipofika Dar es Salaam aliikuta TAA imeshikiliwa na Sykes watatu Abdul na wadogo zake wawili si kuwa ilikuwa chini ya uongozi wa vijana wasomi akina Mwapachu, Kyaruzi na wazee wenye sauti katika wenyeji wa Dar es Salaam kama Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na Sheikh Said Chaurembo.

Ukiacha kuunganisha nguvu hizi mbili mengi ya huko mbele hayataeleweka.

Umuhimu wa Kamati hii na wajumbe wake uko katika matayarisho ya kutengeneza mapendekezo ya katiba ya Tanganyika kazi iliyoletwa na Gavana Twining mwaka wa 1949 na baada ya kushindikana kukubaliwa mapendekezo haya ndipo juhudi zikapamba moto kuunda kuitia nguvu TAA majimboni na kuunda TANU.

Sasa huyu Earle Seaton jina lake hapo halipo lakini ndiye aliyekuwa akiwashauri vipi TAA iitambuke serikali ipeleke nguvu zake UNO kwenye Baraza la Udhamini wa Nchi zilizokuwa chini ya utawala wa Waingereza kwa kudai uchaguzi wa "One Man One Vote."

Elewa kuwa hii ni 1950 na Mwalimu hajafika Dar es Salaam.

Moto ulikuwa unafukuta na serikali kujihami ikawa inawaondoa viongozi wa TAA Dar es Salaam kuwapeleka majimboni kuidhoofisha TAA.

Huu ni mfano mmoja tu.

Antar Sangali kuna vitu naviona vinatoa ladha kubwa katika historia ya Mwalimu kwa vipi juu ya ugeni aliokuwanao Dar es Salaam aliweza kwa haraka kuingiliana na watu na katika akautumia uhusiano huu kukubalika na kuijenga TANU kwanza Dar es Salaam kisha nchi nzima.

Kitabu kinasema Nyerere aliishi nyumbani kwa Ally Sykes Mtaa wa Kipata.

Nyerere angeliishi Kipata angejuana na baba yangu hapa kwa kuwa baba yangu alikuwa kapanga nyumba ya Liwali wa Songea Sheikh Abdallah Simba nyumba inayokabiliana na nyumba ya Kleist Sykes ambayo Ally Sykes ndiyo akiishi na mkewe Bi. Zainab.

Ingekuwa hivi baba yangu, Said Salum Abdallah angemjulia Nyerere nyumbani kwa Ally Sykes.

Baba yangu kakutana na Nyerere nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu.

Kama urafiki Nyerere rafiki yake, mwenzake na msiri wake alikuwa Abdul na kwa kauli yake amesema katika hotuba ya kuaga Ukumbi wa Diamond kuwa Kasella Bantu ndiye aliyempeleka kwa Abdul.

Nini umuhimu wa nyumba hii?

Nyumba hii ndipo kulipokuwa na kituo cha harakati zote za Waafrika Dar es Salaam dhidi ya ukoloni toka wakati Kleist Sykes yu hai.

Nyerere kajuana na watu wengi nyumba hii wanachama wa kawaida wa TAA na viongozi.

Ukimtoa Nyerere nyumba hii ya Mtaa wa Aggrey ukampeleka Kipata kwa Ally Sykes unapoteza historia kubwa ya Mwalimu.

Nyerere hakupata kuishi nyumba moja na Ally Sykes Mtaa wa Kipata.

Nyumba ya Ally Sykes umaarufu wake ni kuwa pale ndipo ilipokuwa, "printing press," ya kuchapa mikaratasi ya "uchochezi,"dhidi ya serikali kazi hiyo akiifanya kwa siri yeye mwenyewe Ally Sykes.

Kwa wakati ule nyumba ya Abdul ilikuwa nyumba ya kisasa yenye vikorombwezo vyote.

Ilikuwa nyumba mbili katika moja.

Nyumba kubwa mlango mkubwa unaelekea Mtaa wa Stanley na nyumba ndogo Mtaa wa Sikukuu.

Hii nyumba ndogo ndiyo akiishi Abbas Sykes na ndiyo akaondolewa pale na kaka yake kumpisha Nyerere mwaka wa 1955 baada ya Mwalimu kuacha kazi.

Mipango yote ya TANU ikifanyika nyumba hii.

Katika nyumba hii ndipo Mama Maria alipojuana na Bi. Mwamvua bint Mrisho mke wa Abdul Sykes na wakawa mashoga wakubwa.

Antar Sangali Ni muhimu mno mchango wa Earle Seaton ukafahamika toka mwanzo ili itakapokuja kuelezwa ilikuwaje Japhet Kirilo akawa mmoja kati ya watu 17 waliounda TANU ijulikane kuwa yeye ndiyo Mtanganyika wa kwanza kuzungumza UNO mwaka wa 1952 kufuatilia kwa Wameru kupeleka madai ya kudhulumiwa ardhi yao na Wazungu na Earle Seaton ndiye aliyetayarisha ile "petition," kupitia Meru Citizens Union.

Hapa utamuona Seaton akitoka kuisaidia TAA Makao Makao Makuu kuandika waraka kwa Gavana Edward Twining anakuja kuwasaidia Wameru kutengeneza "petition," kudai haki yao UNO.

Hili la kwanza.

Pili utakuja kujua nafasi ya Mzanzibar, Sheikh Hassan bin Ameir ambae alikuwa sheikh na mwanasiasa pia pale patakapozuka mgongano baina yake na Julius Nyerere mara tu baada ya uhuru kupatikana ikabidi Sheikh Hassan bin Ameir akamatwe na kufukuzwa Tanganyika akarudishwa kwao Zanzibar.

Sheikh Hassan bin Ameir ana historia kubwa kwa Nyerere binafsi, TANU na katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Huyu kushoto ni Earle Seaton yuko na Mwalimu Nyerere hapa ni baada ya uhuru.

Seaton alikuwa Wakili kutoka Bermuda akifanya shughuli zake Moshi na alikuwa rafiki wa Abdul Sykes.

Abdul ndiye aliyemtia TAA 1950 kwa mlango wa nyuma kama mshauri kuhusu Mandate Territories.

Pucha:Ally Sykes na Julius Nyerere

Kulia Lawi Sijaona, Abdul Sykes, Julius Nyerere na Dossa Aziz tafrija ya kumuaga Nyerere safari ya pili Ukumbi wa Arnautoglo UNO 1957. Picha hii alinipa Kleist Sykes.

Kulia Abdulwahid Sykes na mkewe Bi. Mwamvua bint Mrisho kwenye Garden Party Government House sasa Ikulu, 1950s. Hawa ndiyo walimpokea Julius Nyerere 1952 na 1955 alipoacha kazi wakamkaribisha nyumbani kwao yeye na Mama Maria.

Screenshot_20200510-010735.jpg
Screenshot_20200506-071411.jpg
20200510_075821.jpg

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio kwamba ugeni wake ulileta ladha kwa kuhusiana na watu vizuri

LA HASHA,

Mwl Nyerere alikuwa msomi na mwenye Akili nzuri (cognitively) na pia alikuwa na kipaji cha Uongozi (Talented in Leadership) jambo ambalo wafia dini kama wewe Mohamed Said hutaki kuukubali.

Alipofika DSM alikuta wazee wa kiswahili kama wewe na hao wenzio uliowataja ambao hawakuwa na Uwezo mkubwa kama Mwalimu J.K Nyerere.

Walikuwa na Elimu Akhera tu ya kumuabudu Mwenyezi Mungu kisha warudi kucheza bao na kukaa vibarazani kupiga soga.

Nyerere alikuwa Mbeba Maono ya Taifa hili.

Haya uliyoyaandika ni UONGO MTUPU.

Umeandika kidini kwakuwa wewe ni Mfia dini na HUMPENDI NYERERE.

Tunakufahamu Mohamed Said



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio kwamba ugeni wake ulileta ladha kwa kuhusiana na watu vizuri

LA HASHA,

Mwl Nyerere alikuwa msomi na mwenye Akili nzuri (cognitively) na pia alikuwa na kipaji cha Uongozi (Talented in Leadership) jambo ambalo wafia dini kama wewe Mohamed Said hutaki kuukubali.

Alipofika DSM alikuta wazee wa kiswahili kama wewe na hao wenzio uliowataja ambao hawakuwa na Uwezo mkubwa kama Mwalimu J.K Nyerere.

Walikuwa na Elimu Akhera tu ya kumuabudu Mwenyezi Mungu kisha warudi kucheza bao na kukaa vibarazani kupiga soga.

Nyerere alikuwa Mbeba Maono ya Taifa hili.

Haya uliyoyaandika ni UONGO MTUPU.

Umeandika kidini kwakuwa wewe ni Mfia dini na HUMPENDI NYERERE.

Tunakufahamu Mohamed Said



Sent using Jamii Forums mobile app
Azare..
Umeghadhibika unakuja na lugha kali kuwakashifu wazee wangu.

Eleza tu mawazo yako tukusome.

Hakika Mwalimu alikuwa na uwezo mkubwa sana hili sijasema mie aliyesema hayo ni Hamza Mwapachu akimwambia Abdul kuwa ni lazima Nyerere aingizwe katika nafasi ya President wa TAA katika mkutano wa 1953 na 1954 waunde TANU.

Mimi sina sababu ya kusema uongo.

Kisome kitabu uone nimenukuliwa mara ngapi katika kumueleza Mwalimu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swali binafsi kidogo...

Katika tafiti za kuandika kitabu au vitabu hivi waliwahi kukuomba mchango wowote kuhusu walichokuwa wanaandika?
 
Azare..
Umeghadhibika unakuja na lugha kali kuwakashifu wazee wangu.

Eleza tu mawazo yako tukusome.

Hakika Mwalimu alikuwa na uwezo mkubwa sana hili sijasema mie aliyesema hayo ni Hamza Mwapachu akimwambia Abdul kuwa ni lazima Nyerere aingizwe katika nafasi ya President wa TAA katika mkutano wa 1953 na 1954 waunde TANU.

Mimi sina sababu ya kusema uongo.

Kisome kitabu uone nimenukuliwa mara ngapi katika kumueleza Mwalimu.

Sent using Jamii Forums mobile app


Huyo (Azarel) yeye ndiye mfia dini.
 
Swali binafsi kidogo...

Katika tafiti za kuandika kitabu au vitabu hivi waliwahi kukuomba mchango wowote kuhusu walichokuwa wanaandika?
Mtama,
Walikukuja kunihoji mara mbili:

"Ndugu Mohamed,
Salaam kutoka Dar es Salaam. Tunatumai uko mzima. Tuna furaha kukujulisha kuwa kile kitabu cha wasifu wa Mwalimu Nyerere tulokuwa tunakiandika sasa kimeshachapishwa. Ndugu Mohamed, ulitoa mchango muhimu kwenye mchakato wa utafiti, na hivyo tuna furaha kubwa kukutunukia nakala ya kitabu. Ikiwa utapenda kukifuata kitabu kupitia kijana wako hapo TPH mtaa wa Samora, unaweza kufanya hivyo. La sivyo, tunaomba anuani ya kukutumia nakala yako. Tunatoa shukrani zetu tena na kukutakia kila la kheri."
Prof Issa Shivji
Prof Saida Yahya-Othman
Dr Ng’wanza Kamata

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtama,
Walikukuja kunihoji mara mbili:

"Ndugu Mohamed,
Salaam kutoka Dar es Salaam. Tunatumai uko mzima. Tuna furaha kukujulisha kuwa kile kitabu cha wasifu wa Mwalimu Nyerere tulokuwa tunakiandika sasa kimeshachapishwa. Ndugu Mohamed, ulitoa mchango muhimu kwenye mchakato wa utafiti, na hivyo tuna furaha kubwa kukutunukia nakala ya kitabu. Ikiwa utapenda kukifuata kitabu kupitia kijana wako hapo TPH mtaa wa Samora, unaweza kufanya hivyo. La sivyo, tunaomba anuani ya kukutumia nakala yako. Tunatoa shukrani zetu tena na kukutakia kila la kheri."
Prof Issa Shivji
Prof Saida Yahya-Othman
Dr Ng’wanza Kamata

Sent using Jamii Forums mobile app
Vizuri kama walikuja, ningesikitika kama wasingepita kwako. Vipi, kuna chochote walijifunza au chukua kutoka kwako? Kuna ulilojifunza kutoka kwao?
 
Vizuri kama walikuja, ningesikitika kama wasingepita kwako. Vipi, kuna chochote walijifunza au chukua kutoka kwako? Kuna ulilojifunza kutoka kwao?
Mtama...
Katika kitabu wamenitaja sana katika habari zinazomuhusu Mwalimu hasa kuingiliana kwake na watu wa Dar es Salaam na Maktaba yangu imeorodhoshwa katika kitabu kama Maktaba ambayo ina taarifa za Mwalimu.

Mimi sasa najifunza mengi kuhusu Mwalimu katika hiki kitabu na kama uonavyo kuna baadhi ya mambo nimeyaweka hapo juu katika bandiko langu.
 
Huyo (Azarel) yeye ndiye mfia dini/QUOTE]
Mokaze,
Hii historia ya TANU niliyoiandika katika kitabu cha Abdul Sykes ina kawaida ya kumpa mtu mshtuko.
Azarel kapata mshtuko katika mengi kwani mambo ambayo hata kwa mbali hakupata kuyafikiri.

Kubwa kabisa ni kuwa hakupata hata siku moja kusikia kuwa Nyerere alipata kujadiliwa atiwe katika uongozi wa TAA na waliomjadili pia hakupata hata siku moja kuwasikia wakitajwa katika historia ya TANU.

Hakupata kumsikia Earle Seaton wala hakupata kuisikia TAA Political Subcommittee ambayo mmoja wa wajumbe alikuwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir.

Hakupata kusikia.
Si kosa lake sasa keshajifunza na anaijua historia nyingine si ile historia rasmi.
 
Mtama...
Katika kitabu wamenitaja sana katika habari zinazomuhusu Mwalimu hasa kuingiliana kwake na watu wa Dar es Salaam na Maktaba yangu imeorodhoshwa katika kitabu kama Maktaba ambayo ina taarifa za Mwalimu.

Mimi sasa najifunza mengi kuhusu Mwalimu katika hiki kitabu na kama uonavyo kuna baadhi ya mambo nimeyaweka hapo juu katika bandiko langu.
Vizuri, nashukuru kama umekuwa na mchango kwenye maandiko haya. Hata kama hawajaweka kila kitu lakini ninaamini tutakachopata kitakuwa si haba. Historia ni historia, iwe mbaya au nzuri ni historia. Inapaswa kuandikwa kwa usahihi muhimu tu ni ushahidi.

Watu watajadili mengi kuhusu mazuri au mabaya ya Nyerere lakini naamini tusipindishe historia, iwe nzuri au mbaya, isipindishwe. Watu waje kuitazama wenyewe, na kuijadili kama ilivyo
 
Azare..
Umeghadhibika unakuja na lugha kali kuwakashifu wazee wangu.

Eleza tu mawazo yako tukusome.

Hakika Mwalimu alikuwa na uwezo mkubwa sana hili sijasema mie aliyesema hayo ni Hamza Mwapachu akimwambia Abdul kuwa ni lazima Nyerere aingizwe katika nafasi ya President wa TAA katika mkutano wa 1953 na 1954 waunde TANU.

Mimi sina sababu ya kusema uongo.

Kisome kitabu uone nimenukuliwa mara ngapi katika kumueleza Mwalimu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijawakashifu, nimesema ukweli kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya umeshayaandika sana, nimeshasoma kitabu chako mwaka 2013 na nilinunua kwa pesa yangu kutoka msikitini nikiwa DSM na nilishakuambia hilo hapahapa...labda wewe huna kumbukumbu

Ninaposema wewe ni mdini Nina uhakika na hilo kutokana na baadhi ya kurasa katika baadhi ya vitabu vyako...ningekuwa nipo karibu navyo ningeviscreeshort nikuoneshe na uongo wako pia.

Pia nimeshasikia mjadala wako ukihojiwa na Azam TV kuna mengi ya uongo uliyoyasema na kusema kuwa ulifanya utafiti.

Uongo ni dhambi na huu mwezi mtukufu kwenu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom