Muhogo: Kuongeza thamani ya bidhaa na bei ya mkulima

Muhogo: Kuongeza thamani ya bidhaa na bei ya mkulima

Kigoma Independent

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2017
Posts
3,519
Reaction score
2,055
Muhogo ni zao la chakula na biashara lakini siku za hivi karibuni limeonekana kushamiri sana katika uwanda wa biashara kwa kusaidiana na kushirikiana na mashirika mbalimbali ili kupendeleza mnyororo wa thamani hasa kwa wakulima wadogowadogo.

Mashirika ya MVIWATA (Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania) na VECO (Vredeseilanden-Belgium NGO) yanashirikiana katika kuimarisha usalama wa kipato cha chakula miongoni mwa wakulima wadogowadogo. Mashirika haya yameanzisha mnyororo wa thamani kwa uzalishaji wa zao la muhogo.

Uchunguzi wa zao la muhogo kama kipaumbele ulifanywa na wakulima wa muhogo wenyewe. Shughuli muhimu ni pamoja na uimarishaji na uendelezaji wa asasi za biashara za wakulima na kuziunganisha kwenye soko. Pia midahalo mbalimbali imekuwa ikiandaliwa ili kuhakikisha kuna kuwepo na ushiriki wa wadau wengi kwenye mnyororo wa thamani hususani kwenye zao la muhogo kwa wakulima wadogowadogo nchini Tanzania.

Kwahiyo wale wote ambao ni wakulima wadogowadogo wa zao la muhogo na pia ambao wana malengo ya kufanya ukulima wa zao la muhogo mnapenda kushauriwa ili kushirikiana katika kulngaeza ufanisi na mnyororo wa thamani katika zao la muhogo nchini Tanzania kwa kilimo chenye tija na faida kemukemu kupitia ushirikiano ambao utapatikana kutoka mashirika mbalimbali nchini na nje ya nchi.
 
Mnyororo wa thamani maana yake nini?
 
Mnyororo wa thamani maana yake nini?
"Mnyororo wa thamani "pia ujulikana Kama (value chain creation):Ni mtiririko wa shughuri zote zinazofanywa katika uzalishaji hadi kumfikia mlaji.Mtiririko huu ujumuisha shughuri mbalimbali hadi kufika kwa mlaji ambe ni mtumiaji wa mwisho wa bidhaa au zao lililozalishwa.Kila kazi inayofanywa kutimiza mzunguko mzima huongeza thamani ya zao au bidhaa husika.Kwamfano;
✓Uzalishaji.
✓Usafirishaji.
✓Usindikaji.
✓Uhifadhi.
✓Upangaji wa madaraja.
✓kufungasha na,
✓masoko.
 
" kupendeleza mnyororo wa thamani hasa kwa wakulima wadogowadogo......."

"mashirika haya yameanzisha mnyororo wa thamani kwa uzalishaji wa zao la muhogo......"

Sijaelewa hicho kilichoanzishwa na kinachopendelezwa ni nini?

Ni kitu kipya, hakijawahi kuwepo!
 
" kupendeleza mnyororo wa thamani hasa kwa wakulima wadogowadogo......."

"mashirika haya yameanzisha mnyororo wa thamani kwa uzalishaji wa zao la muhogo......"

Sijaelewa hicho kilichoanzishwa na kinachopendelezwa ni nini?

Ni kitu kipya, hakijawahi kuwepo!
Sio kitu kipya bali Ni kama kiunganishi Cha bidhaa/mazao ambayo wakulima wadogowadogo wanazalisha Kama vile;
✓jatropha(mibomo kaburi).
✓mafuta ya alizeti.
✓kaa wa kwenye tope.
✓muhogo.
✓mkonge.
✓pamba.
Na hii inatokana na kuwepo na wakulima lakini hawana fursa za masoko,usafirishaji nakadharika,kwa hiyo mashirika mbalimbali kama Agriculture non sector actors fund (ANSAF) ili kuinua mbinu mbadala ya kuwainua wakulima wadogowadogo ili kuinua wigo mpana wa kunufaika na kilimo tija Chao wenyewe.
 
Sio kitu kipya bali Ni kama kiunganishi Cha bidhaa/mazao ambayo wakulima wadogowadogo wanazalisha Kama vile;
✓jatropha(mibomo kaburi).
✓mafuta ya alizeti.
✓kaa wa kwenye tope.
✓muhogo.
✓mkonge.
✓pamba.
Na hii inatokana na kuwepo na wakulima lakini hawana fursa za masoko,usafirishaji nakadharika,kwa hiyo mashirika mbalimbali kama Agriculture non sector actors fund (ANSAF) ili kuinua mbinu mbadala ya kuwainua wakulima wadogowadogo ili kuinua wigo mpana wa kunufaika na kilimo tija Chao wenyewe.
Unaweza kuongelea muhogo pekee ili nipate kuelewa fursa hasa IPO wapi kwani nimekuwa nikiliepuka hill zao!
 
Ni kweli usemavyo,hii Ni kutokana hasa na sera ambayo ilitolewa na waziri wetu mkuu Mheshimiwa Majaliwa Kassimu Majaliwa ya kuzuia uuzaji na usafirishaji wa muhogo nje ya nchi(EXPORT BAN POLICY) hususani nchi jirani Kama vile Uganda,Rwanda na Burundi ko ikapelekea kudhoofisha soko la muhogo nchini,lakini sasa hivi kumekuwepo na asasi mbalimbali za kiraia na kibinafsi na pia serikali ya Tanzania Kama vile kituo Cha utafiti cha mikocheni(MARI) ili kuweza kuimarisha soko la muhogo pamoja na mbegu Bora za muhogo Kama vile batobato na matekwenya ambazo Ni Bora katika ukuaji na kustahimiri magonjwa mbalimbali na pia,siku za hivi karibuni tahasisi mbalimbali pamoja na serikali kwa ujumla zimejaribu kuingia ubia na serikali ya China kuhusu kukuza na Kuongeza soko la muhogo nchini,hasahasa kwa kutumia Kuongeza mnyororo wa thamani (VALUE CHAIN CREATION) Kama usindikaji na uboreshwaji wa miundombinu na nyenzo katika soko la muhogo,Ko China imeweka mpango mkakati ambao umeipa thamani pamoja na soko zao la muhogo nchini,ko kwa sasa zao la muhogo liko na soko pana ndani na nje ya nchi.Kwa mfano,VCD,ZAFFIDE,VECO, ANSAF, MVIWATA,DADP's,RLDC,SHF&TASU ambazo ziko msitari wa mbele kupigania masoko ya mazao mbalimbali nchini na sio tu zao la muhogo.
 
".....kituo Cha utafiti cha mikocheni(MARI) ili kuweza kuimarisha soko la muhogo pamoja na mbegu Bora za muhogo Kama vile batobato na matekwenya ambazo Ni Bora katika ukuaji na kustahimiri magonjwa mbalimbali..."
Hizo mbegu za batobato na matekwenya zinatoa wastani tani ngapi kwa ekari nikiweka mche mmoja kwa mita moja mraba?
 
".....kituo Cha utafiti cha mikocheni(MARI) ili kuweza kuimarisha soko la muhogo pamoja na mbegu Bora za muhogo Kama vile batobato na matekwenya ambazo Ni Bora katika ukuaji na kustahimiri magonjwa mbalimbali..."
Hizo mbegu za batobato na matekwenya zinatoa wastani tani ngapi kwa ekari nikiweka mche mmoja kwa mita moja mraba?
Zinaweza kutoa Tani (10-20) kwa hekari ukiweka mche mmoja kwa mita moja mraba.
 
muhogo ni zao la chakula na biashara,lakini siku za hivi karibuni limeonekana kushamiri Sana katika uwanda wa biashara kwa kusaidiana na kushirikiana na mashirika mbalimbali ili kupendeleza mnyororo wa thamani hasa kwa wakulima wadogowadogo.
Mashirika ya MVIWATA(mtandao wa vikundi vya wakulima Tanzania) na VECO(vredeseilanden-Belgium NGO) yanashirikiana katika kuimarisha usalama wa kipato Cha chakula miongoni mwa wakulima wadogowadogo.mashirika haya yameanzisha mnyororo wa thamani kwa uzalishaji wa zao la muhogo.Uchunguzi wa zao la muhogo Kama kipaumbele ulifanywa na wakulima wa muhogo wenyewe.Shughuli muhimu ni pamoja na uimarishaji na uendelezaji wa asasi za biashara za wakulima,na kuziunganisha kwenye soko.Pia midahalo mbalimbali imekuwa ikiandaliwa ili kuhakikisha Kuna kuwepo na ushiriki wa wadau wengi kwenye mnyororo wa thamani hususani kwenye zao la muhogo kwa wakulima wadogowadogo nchini Tanzania.
ko wale wote ambao ni wakulima wadogowadogo wa zao la muhogo na pia ambao wanamalengo ya kufanya ukulima wa zao la muhogo mnapenda kushauriwa ili kushirikiana katika kulngaeza ufanisi na mnyororo wa thamani katika zao la muhogo nchini Tanzania kwa kilimo chenye tija na faida kemukemu kupitia ushirikiano ambao utapatikana kutoka mashirika mbalimbali nchini na nje ya nchi.
kimsingi sijakupata vizuri, nivyema ukanielewesha kwakua mimi ni mkulima wa mihogo na mpaka sasa nahangaika na soko la uhakika hasa huku mkoani Tanga, nimejitahidi kutafuta soko la wachina nimeshindwa kuwapata, hivyo vyama na taasisi ulizotaja bila shaka havina miguu kutoa taarifa ama kuwafikia wakulima kila mahali kwakua hawajulikani ofisi zao zilipo... hivyo nahitaji msaada wako katika hili.
 
kimsingi sijakupata vizuri, nivyema ukanielewesha kwakua mimi ni mkulima wa mihogo na mpaka sasa nahangaika na soko la uhakika hasa huku mkoani Tanga, nimejitahidi kutafuta soko la wachina nimeshindwa kuwapata, hivyo vyama na taasisi ulizotaja bila shaka havina miguu kutoa taarifa ama kuwafikia wakulima kila mahali kwakua hawajulikani ofisi zao zilipo... hivyo nahitaji msaada wako katika hili.
Mkuu naomba tuwasiliane ili tujadili pamoja, maana msimu huu ninataka kuanza na ekari 20. Ili nijue soko hasa .. 0753142011
 
Mimi nina muhogo ekari tano natafuta soko mwenzangu ana ekari 50, wote hatujui tuuze wapi naomba ufunguke,vinginevyo tunaona hakuna mawasiliano kati ya wakulima na watalaam na viongozi,wanasiasa na kwa ujumla tunasoma tu kwenye magazeti soko liko China.
 
Mimi nina muhogo ekari tano natafuta soko mwenzangu ana ekari 50, wote hatujui tuuze wapi naomba ufunguke,vinginevyo tunaona hakuna mawasiliano kati ya wakulima na watalaam na viongozi,wanasiasa na kwa ujumla tunasoma tu kwenye magazeti soko liko China.

Kama kuna biashara kichaa siku hizi basi ni kilimo!!

Wanasema kila leo masoko yapo, nenda huko Mviwata uone watakavyokushawishi kulima lakini mazao yakikomaa utashangaa wanavyokukwepa!! 🤣🤣🤣

Kilimo kwa nchi hii ni kama kubeti tu na si shughuli ya uhakika kuinua uchumi!! Ukiotea unaibuka kikikukamata unalia vile vile!!

Nililima muhogo sijaamini kilichotokea, ila utashangaa watu wanakuja humu una soko una soko ila soko lililo wazi halipoo!!

Utapambana na madalali, walanguzi na matapeli kuhusu wanunuzi wa uhakika hakuna!! Wengi wababaishaji, mashirika nayo hayana ushirikiano yaan ni bure tu!!
 
Back
Top Bottom