Muliro: Wanaoshangaa kuwaona Askari Mtaani wakiwa na mitutu, wana vimelea vya uhalifu

Muliro: Wanaoshangaa kuwaona Askari Mtaani wakiwa na mitutu, wana vimelea vya uhalifu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Akiulizwa swali na Mwandishi wa habari kuhusu kuwepo na wimbi kubwa la askari walioshikilia silaha za moto mitaani tofauti na ilivyozoeleka, Kamanda wa Kanda ya Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema kuwa wananchi hawana hofu wanaendelea na majukumu yao kama kawaida.

Amesema kuwa Watu wema wanatamani hata askari wenye silaha wawepo hadi mafike hadi majumbani kwao huku akidai kuwa kama kuna wenye wanaoshangaa basi wana vimelea vya uharifu.

"Mtu Mwema anafurahi kuona hiyo unayoita mitutu kwa sababu haina uhusiano na yeye, wanatamani iwe mpaka milangoni, watu wema wanataka amani wantaka usalama, kwahiyo watu wanaoshangaa ni watu wenye vimelea vya kiharifu, lakini wale watu wazuri wanatamani hali hii iende kule waliko chini"

Amesisitiza kuwa doria za aina hiyo zitakuwa endelevu katika kulinda wananchi na mali zao.

Hata hivyo kuanzia September 21, 2024 imeshuhudiwa baadhi ya askari wakiwa wameshikiria silaha za moto na magari yanayodhaniwa kuwa ya 'washawasha' wakiwa katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.

Ambapo baadhi ya Watu waliosikika wakihojiwa na vyombo vya habari mbalimbali walidai kuwa na hofu wakidai kuwa haijazoeleka kushuhudia askari wengi wakiwa na silaha za moto maeneo ya mitaani ambapo shughuli za kijamii zinafanyika isipokuwa kama kuna sababu maalumu.

Pia, soma: LIVE - Yanayojiri kwenye Maandamano ya CHADEMA 23/9/2024
 
Inapendeza sana ikiwa hivyo lakini shida ni moja ghafla watapotea, ghafla ukipiga simu kuna tukio waje kwa haraka hivi hivi mana siku mbili hizi huko daslamu watu wamelala milango wazi
Nadhan sasa hv tunawaona sana mitaani labla kwa kuwa waliona kuna viashiria vya uvunjifu wa amani kutokana na maandamano ambayo wao waliyakataa, ila n jukumu lao kufanya hv wanavyofanya sasa
 
Nadhan sasa hv tunawaona sana mitaani labla kwa kuwa waliona kuna viashiria vya uvunjifu wa amani kutokana na maandamano ambayo wao waliyakataa, ila n jukumu lao kufanya hv wanavyofanya sasa
Kabisa kabisa mkuu kuna mitaa haipitiki kwa sababu ya matukio ya ubakaji na wizi lakini hata siku moja hutasikia wameweka makambi ,lakini kumbe inawezekana kabisa ona polisi walivyozagaa hadi wengine hawana pa kupita
 
Kabisa kabisa mkuu kuna mitaa haipitiki kwa sababu ya matukio ya ubakaji na wizi lakini hata siku moja hutasikia wameweka makambi ,lakini kumbe inawezekana kabisa ona polisi walivyozagaa hadi wengine hawana pa kupita
Hawa polisi wanatakiwa kupambana na hayo yote ila ndo hvy wanazingatia mambo ya siasa tuu badala ya kutatua matatizo ya wananchi kama hayo.
 
Afande sio kweli kwamba tuna vimelea vya uharifu.. hayo maneno yakoo..

Leo nimeshinda maghetoni tu.. nyuma ya keyboard
 
Hakika waamuzi ni wa aina tatu: mmoja atakuwa Peponi na wawili watakuwa Motoni. Yule aliyehukumu kwa haki na kwa ujuzi atakuwa Peponi. Yule aliyehukumu bila ujuzi, na akaonea katika hukumu, atakuwa Motoni.”
(Sunan Abu Dawood, Hadithi 3573)
 
Akiulizwa swali na Mwandishi wa habari kuhusu kuwepo na wimbi kubwa la askari walioshikilia silaha za moto mitaani tofauti na ilivyozoeleka, Kamanda wa Kanda ya Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema kuwa wananchi hawana hofu wanaendelea na majukumu yao kama kawaida.

Amesema kuwa Watu wema wanatamani hata askari wenye silaha wawepo hadi mafike hadi majumbani kwao huku akidai kuwa kama kuna wenye wanaoshangaa basi wana vimelea vya uharifu.

"Mtu Mwema anafurahi kuona hiyo unayoita mitutu kwa sababu haina uhusiano na yeye, wanatamani iwe mpaka milangoni, watu wema wanataka amani wantaka usalama, kwahiyo watu wanaoshangaa ni watu wenye vimelea vya kiharifu, lakini wale watu wazuri wanatamani hali hii iende kule waliko chini"

Amesisitiza kuwa doria za aina hiyo zitakuwa endelevu katika kulinda wananchi na mali zao.

Hata hivyo kuanzia September 21, 2024 imeshuhudiwa baadhi ya askari wakiwa wameshikiria silaha za moto na magari yanayodhaniwa kuwa ya 'washawasha' wakiwa katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.

Ambapo baadhi ya Watu waliosikika wakihojiwa na vyombo vya habari mbalimbali walidai kuwa na hofu wakidai kuwa haijazoeleka kushuhudia askari wengi wakiwa na silaha za moto maeneo ya mitaani ambapo shughuli za kijamii zinafanyika isipokuwa kama kuna sababu maalumu.
Swali Muliro analotakiwa kujiuliza ni kwa nini nchi imefika hapa,na nani kaifikisha hapa.Hivi kwa nini tusikae chini tukazungumza na kutafuta suluhu ya matatizo yetu.Kila mtu kafura kama swira hakutatusaidia sana kama nchi,mwisho wake ni nchi kusambaratika.Lazima tutafakari njia zetu.Sijui Kwa nini viongozi wetu wameshindwa kuona kwamba Shetani yuko kazini akipanga kuisambaratisha nchi yetu.Ukweli ni kwamba Satan is at work slowly destroying our country.
 

Attachments

  • chadema_022308.png
    chadema_022308.png
    95.9 KB · Views: 2
Akiulizwa swali na Mwandishi wa habari kuhusu kuwepo na wimbi kubwa la askari walioshikilia silaha za moto mitaani tofauti na ilivyozoeleka, Kamanda wa Kanda ya Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema kuwa wananchi hawana hofu wanaendelea na majukumu yao kama kawaida.

Amesema kuwa Watu wema wanatamani hata askari wenye silaha wawepo hadi mafike hadi majumbani kwao huku akidai kuwa kama kuna wenye wanaoshangaa basi wana vimelea vya uharifu.

"Mtu Mwema anafurahi kuona hiyo unayoita mitutu kwa sababu haina uhusiano na yeye, wanatamani iwe mpaka milangoni, watu wema wanataka amani wantaka usalama, kwahiyo watu wanaoshangaa ni watu wenye vimelea vya kiharifu, lakini wale watu wazuri wanatamani hali hii iende kule waliko chini"

Amesisitiza kuwa doria za aina hiyo zitakuwa endelevu katika kulinda wananchi na mali zao.

Hata hivyo kuanzia September 21, 2024 imeshuhudiwa baadhi ya askari wakiwa wameshikiria silaha za moto na magari yanayodhaniwa kuwa ya 'washawasha' wakiwa katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.

Ambapo baadhi ya Watu waliosikika wakihojiwa na vyombo vya habari mbalimbali walidai kuwa na hofu wakidai kuwa haijazoeleka kushuhudia askari wengi wakiwa na silaha za moto maeneo ya mitaani ambapo shughuli za kijamii zinafanyika isipokuwa kama kuna sababu maalumu.

Pia, soma: LIVE - Yanayojiri kwenye Maandamano ya CHADEMA 23/9/2024
Jamani nikifikiri huyu Muliro ana akili!!
 
Swali Muliro analotakiwa kujiuliza ni kwa nini nchi imefika hapa,na nani kaifikisha hapa.Hivi kwa nini tusikae chini tukazungumza na kutafuta suluhu ya matatizo yetu.Kila mtu kufura kama swira hakutatusaidia sana kama nchi,mwisho wake ni nchi kusambaratika.Lazima tutafakari njia zetu.Satan is at work slowly destroying our country.
Hiyo akili hana huyo babu
 
Akiulizwa swali na Mwandishi wa habari kuhusu kuwepo na wimbi kubwa la askari walioshikilia silaha za moto mitaani tofauti na ilivyozoeleka, Kamanda wa Kanda ya Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema kuwa wananchi hawana hofu wanaendelea na majukumu yao kama kawaida.

Amesema kuwa Watu wema wanatamani hata askari wenye silaha wawepo hadi mafike hadi majumbani kwao huku akidai kuwa kama kuna wenye wanaoshangaa basi wana vimelea vya uharifu.

"Mtu Mwema anafurahi kuona hiyo unayoita mitutu kwa sababu haina uhusiano na yeye, wanatamani iwe mpaka milangoni, watu wema wanataka amani wantaka usalama, kwahiyo watu wanaoshangaa ni watu wenye vimelea vya kiharifu, lakini wale watu wazuri wanatamani hali hii iende kule waliko chini"

Amesisitiza kuwa doria za aina hiyo zitakuwa endelevu katika kulinda wananchi na mali zao.

Hata hivyo kuanzia September 21, 2024 imeshuhudiwa baadhi ya askari wakiwa wameshikiria silaha za moto na magari yanayodhaniwa kuwa ya 'washawasha' wakiwa katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.

Ambapo baadhi ya Watu waliosikika wakihojiwa na vyombo vya habari mbalimbali walidai kuwa na hofu wakidai kuwa haijazoeleka kushuhudia askari wengi wakiwa na silaha za moto maeneo ya mitaani ambapo shughuli za kijamii zinafanyika isipokuwa kama kuna sababu maalumu.

Pia, soma: LIVE - Yanayojiri kwenye Maandamano ya CHADEMA 23/9/2024

Nchi zote zenye amani hauoni askari wakizagaa ovyo namna hiyo.
 
Back
Top Bottom