Mume anapokea 1M salary kwa mwezi na mke anapokea 3M, kutakuwa na heshima kweli hapa?

Izi mi naeza sema ni non sense ideology na ni kama vile unasema kama hujatarika usioe ,we sema mwanaume hata ukifilisika unatakiwa urud upambane usikae tu uridhike mwanamke aendeshe family maana mambo ya kufanya ni mengi
 
Ipo hivi mwanamke hajawahi kuacha kupenda mwanaume anayemzidi kipato, toka enzi za wazee , hata zama za mawe na chuma wanawake walipenda mwanaume ambaye physically yupo fit sio mnyonge.
Kwa sababu walijua ataweza kuwinda, kulima na kuipa ulinzi familia.

Leo hii vitu vyote hivyo vimekuwa converted kuwa pesa.
Leo hii chakula, ulinzi, na kila aina ya mahitaji ya msingi unatumia pesa.

Mwanaume lazima upambane kuhakikisha dharau za rejareja zinapotea kwenye familia.

Tafuta pesa, haya masuala ya kusifia mwanamke kisa anakutunza na kumpa maneno mazuri mazuri si tabia zetu wanaume, na mtu unaridhika na ndevu zako eti unazidiwa kipato na mke anakukubali...

Inashangaza sana. Mtachokwa .
 
Izi mi naeza sema ni non sense ideology na ni kama vile unasema kama hujatarika usioe ,we sema mwanaume hata ukifilisika unatakiwa urud upambane usikae tu uridhike mwanamke aendeshe family maana mambo ya kufanya ni mengi
Yaani filisika yako wewe mwanaume bado iwe above your wife

Thats your job to do in this world
 
Nature of the mada ilikuwa ni mwanamke anayekuzidi kipato unaweza ishi naye....
And my answer ni inategemea na nikatolea mfano huyo jamaa.
Yes, nakubali kuwa kila mwanamke anafaa kuwa na mwanaume aliyemzidi kipato ndivyo inapswa kuwa lakini hilo halikuzuii kama wote manfanya kazi kusaidiana. Otherwise hakuna haja ya kuoa wmanamke anayefanya kazi kama hawezi toa mchango pale unaposhindwa ni afadhali abaki nyumbani alee watoto umtunze yeye na watoto ndio iwe kazi yake.
Lakini zama zimebadilika mme na mke wanafanya kazi wanaondoka asubuhi wanarudi jioni. Ni kwa sababu demand za maisha zimeongezeka ni watu wachache sana wanaoweza meet hizo demand kama wanaume halafu wakawa na maisha standard unless kama ni familia ambayo vitu vya msingi ni chakula, nguo, kulala, shule saint kayumba, na kifurushi cha azam.
Wewe tazama circle yako, turudi kwenye uhalisia ni watu wangapi wanaishi maisha mazuri, mke, mume wana usafiri, wana nyumba ya maana, watoto wanasoma shule walau za kari ya 3 mls kwa mwaka, wana maisha ya kipato cha akti ambapo mwanume tu ndiye mtoaji wa kila kitu yani mwanamke hana mchango kabisa?
 
Yaani filisika yako wewe mwanaume bado iwe above your wife

Thats your job to do in this world
Kufilisika unaeza kufilisika kabisa maama siyo swala la kutaka ,maana ingekuwa swala la kutaka kila mtu angekuwa tajir na hakuna mtu ambaye anataka kufilisika
 
Kufilisika unaeza kufilisika kabisa maama siyo swala la kutaka ,maana ingekuwa swala la kutaka kila mtu angekuwa tajir na hakuna mtu ambaye anataka kufilisika
Mkuu

Filisika yako ukifilisika still uwe juu ya huyo mwanamke

Kama huwezi leta chakula mezani,maana yake wewe ushakufa!
 
Hizi mambo zipo ila kwenye bonds chache sanaaaa
 
Sasa mfano mke wa hivi umesimama unawezaje kumuacha Yani..!!
 
Kuna wanaume ambao hawataki wake zao wafanye kazi, lakini mimi si hivyo, nachosema hapa ni kwamba hata kama kazi zako zimeenda vibaya usikae ubweteke kisa mkeo anaingiza mshahara mkubwa, hata kama ulimwezesha, inabidi walau uzungumze nae akupe mtaji mwisho wa siku urudi nyumbani na mahitaji la sivyo utadharaulika na kuonekana baba mjinga.

Mwanamke ataanza kukuona miyeyusho na utaanza kulaumu lakini kwa Africa wanawake ndivyo walivyo thats why nimesema haina haja ya kuwachukia lakini kiasili na kiuumbaji wanawake wanapenda tuwazidi kuanzia kipato hadi kimo utawalaumu bure tu.

Kwa Tanzania ni asilimia chache za familia zenye uwezo kati ya nyingi hilo lipo wazi. Lakini pia familia ambazo baba na mama wanasaidiana kuendesha familia financially zinakuwa vizuri kuliko ambazo baba pekee anategemewa.
 
Ndo wapo sasa wanaofanya hivyo na muda unavyozidi kwenda wanazidi kuongeza.
Siku hizi consultation zimekua nyingi
Na mitandao ni sehemu tosha ya kujiongezea exposure na kipato
 
Wanaume wasio na kipato hua wanagubu sana na mali za wanawake zao msigombane kidogo utashangaa mada ya hela imeingizwa hata kama ugomvi hauhusini na hela utasikia unaninyanyasa kwa sababu unanyumba,au sababu sichangii chochote ,au sababu silipi ada za watoto ,una jeuri sababu umelipa kodi n.k

hata kama hujamnyanyasa atakwambia hivyo,kamwe mwanamke hautakua na furaha na hela yako ,yalishanikuta,kiufupi mwanaume asiefanya majukumu yake katika familia ana gubu sana ,hasa mkikosana simply sababu hajiamini,wanaume tafuteni pesa .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…