Mume wa jinsi hii........kama mke utavumilia kweli?

Oooops! That is too junky for me, I got a graceful body that responds too positively with food. Well, you ar a big boy, neh!?

Naongelea appetite ya nanilii, kama baba ameloose appetite shauri ya ku-diet-ishwa mfululizo (sexual aneroxia), maybe mdada aliloose appetite kwa sababu the menu was monotonous? Forgive my thinking...
 
........kweli heri nusu shari, kuliko shari nzima.
 

one sided analysis

what if there are underlying factors kama infidelity, poor communication, kupotea mvuto wa sex (uchafu, maugomvi, cheating, visasi, kauli chafu)

we havent heard a chance to listen to the other part
 
Ofcoz it is one sided manake tukimsaka mume nae (ukumbuke hii ni 2nd hand reporting) tutahitaji fund ya kufanyia utafiti huu,lol!

Sasa baba, uchafu na ugomvi ndo vimfanye huyu mzee apeleke familia hadi huko 'out' na kubaki garini? Ofcoz niliwaza kwa chale la 9 huenda jamaa ana ka-small world kake ana-connect nako kwa raha, so anapenda kuwa alone.

Come to think of that: hivi jf addiction haiwezi kuwa ni ka-emotional cheating flani?
one sided analysis

what if there are underlying factors kama infidelity, poor communication, kupotea mvuto wa sex (uchafu, maugomvi, cheating, visasi, kauli chafu)

we havent heard a chance to listen to the other part
 
Byshernger, pole na kichapo ulichochezea jana
Hope leo unaweza fikiri vizuri ni wapi ulikosea.
 
......ujue tatizo nililoliona mie ni mdada kuwa mpweke, sasa unaenda out na watoto mume hayupo.....huko huko outing unaona couple nyingine na watoto wao. Hapa lazima mdada ajisikie yupo lonely.

kumbuka si wanaume wote wanapenda outing! Tatizo kubwa ninalo liona hapa, huyu mwanamke inaonekana humlazimisha mumewe kufanya asivyopenda! Outing si lazima saaana hasa kama mwenzio hajisikii! Cha muhimu mwanamke atumie njia za ushawishi kuliko kuforce! Mf: asiombe tena kwenda outing aone reaction itakuwaje! Kuhusu mambo ya ndani, hasa tendo la ndoa, ni kazi ndogo sana kwa mwanamke! Yeye ajitume tu kuandaa mazingira, mf: kumchangamkia kwa kumkaribia sana pindi wawapo chumban, kuvaa nguo znazoshawshi, kwenda nae bafuni na kumchokoza chokoza kiutundu, na utundu mwingine wa kike!
 
Ngoja nione michango ya wanawake kwanza ili nikija namaliza kabisa!Ila Kongosho umechangia vyema!Chukua tano mama!
 
Kama huyo baba hakua hivyo mwanzo kuna uwezekano huyo mwanamama ameshiriki sana kuwafikisha kwenye hali waliyofikia. Ila sasa kwasababu watu hua hawapendi kukubali au hata kuona kwamba wao ndio haswa chanzo cha matatizo basi lawama zote zinaelekezwa kwa mume.
Ukute kamfokea jamaa wa watu mpaka kapoteza kujiamini. . .au ndio zake kumsema sema vibaya kwa watu mpaka anashindwa kuungana nae wakitakiwa kuwa na watu wengine au sio mpenzi tu wa kufanya hivyo. . .sema kama hajawahi kuchukua muda kumsoma mwenzake hawezi jua hata hilo. Matokeo yake yeye anafanya kila kitu kiwe about HER and no one else. Huko chumbani nako ukute kuna kipindi alikua anamnyanyasa jamaa na "sijisikii/kichwa kinauma" nyingi mpaka akazoea alafu sasa hivi anatafuta mchawi kwingine. Pengine hajiweki kwenye mazingira tamanishi wala hasemi yeye anamhitaji jamaa.

Kwasababu mengi hayajulikani na ni dhahiri huyo mama yeye hajakwambia matatizo yake ni yapi sina lawama za kumshushia huyo baba. Mwambie huyo dada AJICHUNGUZE.
 
BTW huyo mume anavumilika sana kama mhusika akiacha kulalamika na kujaribu kufanyia kazi hicho alichonacho.

Mwanaume asiependa sana hiyo motoko is actually a good catch. . all about family kinda man.Ndio maana hata kwenye mitoko yao anahakikisha anawapeleka na sio anasema tu gari hiyo hapo nendeni msinisumbue. Huyo mama anaweza akatumia huo mwanya kuwa karibu na mume wake pamoja na watoto wawapo nyumbani badala ya kujali wawapo wamezengukwa na watu, maana anachotaka yeye ni kuonekana yuko na mume na sio kwamba anakua lonely. Angekua lonely angekua anaachana na hiyo mitoko wakati mwingine na kutulia na mume wake nyumbani. . . yani hapa angesema hua hataki kuungana nao ili akalewe zake bar ningemwelewa, ika kwasababu sivyo ajue kabisa huyo mume anakosa attention toka kwa mke wake maana sio ajabu kabisa ukakuta hata akisindikizwa mpaka ndani anasahau kaja na mume, story zinanoga na watu wengine tu na kujiweka mbali ndio namna ya mume kuonyesha hajisikii kuwa left out/unappreciated kwa watu.

Sex mwanaume hata akiwa amekasirika/huzunika ukajitahidi kulainisha lugha na kupunguza sauti nyumbani atajitoa mwenyewe tu achilia mbali mdada kusema na kuonyesha kwamba muda umefika. Au hamjawahi kuona mtu anambusu/kumbatia mwenzake kimahaba huku macho yamejaa machozi na moyo umejaa majonzi?

Aache kumlazimisha watoke watoke na badala yake apunguze yeye kutoka kwa muda. Na wakiwa nyumbani afanye kazi ya ziada kumfanya mume wake afurahie kampani yake alafuukitokea mtoko wa muhimu ambembeleze baada ya kumfanya ajisikie vizuri kama mume hatomfuata nyuma kama kondoo.
 



Uko sawa kabisa , haya mambo ya outing si muhimu sana ila unaweza kukuta mwenzio analikomalia kama vile ni jambo la maana sana. Unaweza kumkokota punda mpaka mtoni lakini uamuzi wa kunywa maji ni wake
 
Mleta mada, unaweza kumshawishi huyo mamaa kujiunga hapa JF ili tumsikilize moja kwa moja.Naamini kwa vile ww ni mtu wa pili huenda usiyafikishe yote yanayoshauriwa.Si rahisi kuyakumbuka yote.
 
Pengine huyo mdada anampeleka jamaa sehemu ambazo colleague wa huyo mdada wa kazini huwa wanakuwepo, na jamaa kama kweli ana hiyo low self esteem anakuwa akiwaona hao colleague esp wa kiume ananywea so anaona sio poa kuonesha mbele za watu anaamua ku chill kwenye gari.

Au inawezekana huyo binti amepoteza mvuto labda kwa kunenepa kupita kiasi sasa jamaa anajisikia embassed kwenda nae kwenye public ila hawezi kumwambia sasa na binti anashindwa kusoma mchezo.
 
ukipata raha sana
wakati mwingine unaanza kutafuta shida

huyu mama kashiba!

Yaani Kongosho umenena. Hizi mbona c tatizo! Mwambie mdada ajiadjust kwa kumpokea na kumchukulia mumewe kama alivyo. Pengine malezi yake yalikuwa hivyo atambadilishaje sasa hivi?!

Tatizo lipo kwenye tendo la ndoa. Hebu kwanza kabla ya kuchukua hatua aongee naye, ajichungue na yeye asijekuwa yeye ndo hasisimshi!
 
Wanawake wa siku hizi mna matatizo sana. Mnapenda maisha ya kuiga iga mpaka mnaona waume zenu kama wanamatatizo
 
Jamani huyu baba mbona mnamuonea?? ana kosa gani?? wanawake kweli nimeamini hawaridhiriki.....Unataka mlevi??mzururaji??ambaye hana mda wa kukaa na watoto?? kiwembe???....aghhhh
 

Huyu analinganisha mme wake na waume wa wengine.....anafanya kama kuna standard ya mme, na kimsingi anaweza kuwa hajui mahitaji yake ya mwanaume (anaiga na kulinganisha tu).......nadhani akifanya vyote alisema bado atataka vingine! (Kongosho kamaliza).

Japo hatujapata maelezo ya mme, ila huyu mke ana tabu kweli!
 

au pia inawezekana alimpa ka-likizo ka lazima jamaa maybe baada ya mkwaruzano au tu dada alikosewa akajinunisha hata wiki nzima wakati jamaa ana mahitaji yake,na ikachukua muda ku-reconcile,niaminini mimi,kwa baadhi ya watu(kama mimi) inaweza kuharibu kabisa apetite ya 'chakula' (haswa kwa huyo mama) na huchukua muda kuisha.na haswa kama yeye ndo alikosea na hakutaka kurekebisha ndo kabisa,huko anakoendea jamaa atakuwa hata 'hamgusi' na sababu nyingi....mwisho nyumba ndogo!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…