mpaka sasa sijasoma cjui uzi unahusu niniukasepa halafu bado upo.
Nitajaribu kufanya hivyo dear.[emoji120]
Halafu Mungu akitoa kibali cha ndoa nitamuomba Mr. aniruhusu tulete mtoto mwingine wa kiume ili wawe wawili mana nahisi hii kucheza na huyu pacha wake wa kike kila mara labda sio nzuri sana.
Hali inaogopesha mwenzanguIla hii ilikuwepo toka zamani sana. Enzi hizo ushoga haujaenea tulikuwa tunaangalia tunaona kawaida tu miaka ya 2000's. Nilikuwa naipenda sana ila kwa hali ya sasahivi lazima ionekane ni mambo ya kuhamasisha ushoga hasa ukiangalia John mwenyewe ni mtoto wa mama.
Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
Mwenzangu acha tu😂.Kwa nin wanasema wewe ni mwanaume,
Binafsi sijapata kiunganishi chochote Cha kuona wwe ni mwanaume
Mwenyewe pia anadai hajawahi na wala hawezi kupiga mwanamke.Anadai aliongea vile sbb ya hasira tu.Sijui mkuu.
Mimi babu yangu alikua anatuchakaza mbaya mbovu, akikushika anakucharaza bakora na ngumi zipo ila ajabu ni kua hakuwahi kumpiga mkewe hata kofi tu.
Bibi nae alikua anatuambia hilo kua mumewe pamoja na ukorofi na ukali wake woote lakini hakuwahi kumgusa hata kidogo. Sijui ni mila maana hata mkamwana wake hakuwahi kumfokea wala kumuagiza chochote.
Labda asemayo ni kweli mkuu, ila jaribu pia kufatilia historia yake.
Nimempenda sana babu yako mkuu🙏🙏.Sijui mkuu.
Mimi babu yangu alikua anatuchakaza mbaya mbovu, akikushika anakucharaza bakora na ngumi zipo ila ajabu ni kua hakuwahi kumpiga mkewe hata kofi tu.
Bibi nae alikua anatuambia hilo kua mumewe pamoja na ukorofi na ukali wake woote lakini hakuwahi kumgusa hata kidogo. Sijui ni mila maana hata mkamwana wake hakuwahi kumfokea wala kumuagiza chochote.
Labda asemayo ni kweli mkuu, ila jaribu pia kufatilia historia yake.
Ni kweli dear ila naona umuhimu wa kiume wawe wawili.sio mbaya mana wamelala kwenye tumbo moja na wamekua pamoja ila muwaelekeze hao watoto wajue mipaka ya kila mmoja mwa mwenzie wa kike ajue kua huyo ni kaka ake same kwa wakike[emoji4][emoji4] pia msiwaringanishe wala wasijiringanishe au kufananishwa kwa chochote kila mtoto ana namna yake ya kukua sio kiakili tuu
Huyo huwezi kumuacha. Nakumbuka Dada yangu aliolewa na jamaa ambae alikuwa akimpiga mara kwa mara na Dada alikuwa akirudi Nyumbani kwa kukimbia vipigo na wazazi walikuwa wanamrudisha kwa mume wake.Daah!
Uzuri nampenda siwezi kuchepuka
Dizaini kama Chai 🍵 🍵🍵Ndugu zangu,
Ijumaa iliyopita mume wangu mtarajiwa alileta watoto wake (wetu) walale kwangu ili Jumamosi nikawafanyie shopping ya mavazi.
Jumamosi nikawawafanyia watoto wetu shopping hadi hela yote alonipa baba yao ikaaisha na baada ya kuridhika kuwa watoto wamepata nguo za kutosha nikaona sio mbaya na mimi nikitoa tu senti twangu kuwapeleka madogo wakale bata.
Hakika mim na wanangu tulikula bata tukafurahi na tukapata new friends from Canada na jioni ilipofika tukarudi zetu home (kwangu) tukalala wote tukiwa na nyuso za furaha.
Japo sio muda mrefu tokea watoto hawa waje katika maisha yangu ila wamekua baraka na darasa kubwa kwangu. Wamenikomaza.
My babies are so cutie and sweet na kila nikiwa nao najisikia huzuni vinapoondoka.
Hawa watoto ni mapacha, wa kike na wa kiume na ni watundu kishenzi na mwanzoni walikua wakiletwa kukaa na mimi nilikua nachanganyikiwa maana nilishazoea naishi mwenyewe hakuna wakunivurugia nyumba ila mara tu baada ya kuwa mama ndo nikaelewa maana ya kuzaa sio kazi bali kulea ndio kazi.
Hawa madogo walikua hawaoni tabu kuchukua jagi la maua na kuanza kurushiana kama mpira na mechi itaisha pale litakapovunjika.
Kuna siku nilikua chumbani nimejipumzisha mchana nikaamshwa na simu ya jiran ananambia kuna mtoto juu ya paa. Kutoka namkuta ni yule wa kiume kafata kitoto cha ndege walikikamata then kikarukia juu ya paa.
Siku nyingine wakaenda kuwapa mbwa Lunch yote kwenye sufuria kisa mlinzi aliwaambia mbwa wanampenda yeye sababu yeye ndo anawapa chakula kwa hiyo walitaka na wao mbwa wawapende.
Yaani ni mambo mengi ila pamoja na utundu wao wote sijawahi kuwaza kuwachapa sababu siamini katika kupiga watoto.
Watu walinishauri sana niwachape ila nilipuuza na nilichofanya ni kuongea nao na kuwaelewesha madhara ya kila kitu kibaya wanachofanya.
Mfano waliharibu blender kwa hiyo kila wakisema mom we want juice nawakumbusha kuwa wameharibu blender kwa hiyo dada hawezi tena kuwasagia juice.
Nikiona wanataka kuharibu remote namuuliza what is your favorite cartoon? Akinijibu namwambia sasa ukiharibu hiyo remote hutaweza tena kuangalia hiyo katuni yako. Unakuta anaacha bila kupigwa na anakua na uelewa.
Namshukuru Mungu mapacha wangu wamebadilika sana na wamepunguza utundu na hata wakija hawanivurugi tena kichwa changu.
Sasa Jumapili mchana wakati baba yao anakuja kuwachukua mimi nilikua chumbani na watoto walikua sebuleni wakiangalia katuni.
Kumbe katuni waliyokua wakiangalia ni katuni fulani hivi yenye character ambae ni katuni mtu mzima baunsa, juu mnene chini mwembamba. Sasa bwana kumbe hiyo katuni sio nzuri maana kuna saa huwa anakua kama anabong'oa halafu anatikisa wowowo ila sikua najua. Wazazi kuweni makini kuna katuni nyingi mbaya.
Sasa nikiwa chumbani nikasikia yule wa kiume akisema neno "sitaki" halafu yule wa kike akasema huwezi. Wa kiume nikasikia akisema nikiamua naweza ila wanaume hawafanyagi hivyo. Yule wa kike akasema, "Mbona huyo (akataja jina la huyo katuni) ni mwanaume na anafanya? Wa kiume akasema ni mwanaume mjinga mbona baba hafanyagi?" Wa kike akamwambia, "Kila kitu huwezi ndio mana shuleni walimu wananisifia mimi sababu najua vitu vingi kuliko wewe, hata bibi anasema wewe unachoweza ni kuharibu tu vitu. Hilooo. Yule wa kiume akasema kwa nguvu na hasira, nawezaaa!
Wa kike akasema huwezi kitu. Wa kiume akasema kwa hasira na kwa sauti ya juu zaid" Nawezaaa! Wa kike akasema "Kama unaweza cheza kidogo nione!
Mpaka hapo nikataka nione kinachoendelea sebuleni sababu maongezi yao yalishanitia mashaka. Nkafungua mlango taratibu kisha nikawa naelekea sebuleni kwa kunyata.
Ile kufika usawa wa kuwaona yule wa kiume akiwa hanion maana alinigeuzia mgongo akasema kwa hasira "Naweza ila sitaki' kisha akaanza kukatika kama ile katuni.
Unaambiwa siku ukitembea uchi ndo siku utakutana na mkweo. Masikini dogo, ile anaanza tu kukatika na baba yake anafungua mlango na kumkuta mwanae wa kiume, jembe lake analolisifia likiwa limebong'oa linakata viuno.
Dogo alivyomuona tu baba yake akajua siku yake ishaharibika Ila hakupanga kufa kizembe. Akarukia kwenye meza. Baba ake akienda huku anakimbilia huku na macho ya dogo yalionyesha target yake ni kukimbilia mlangoni atoke nje lakini baada ya kusumbua kidogo baba yake akamdaka.
Ndugu zanguni. Baada ya huyu mume wangu mtarajiwa kumkamata mwanae ndio nilipoiona sura yake ya ukatili.
Alivyomkamata mwanae akamkaba shingo kwa mkono mmoja huku akimvuta kwa hasira akaenda mpaka iliko pasi yangu akaichukia.
Samahani wapendwa, ila alivyochukua pasi tumkojo tulianza kunitoka maana nilijua anachotaka kukifanya. Kumchoma mtoto na pasi. Nikawa namuombea mtoto msamaha ila bwana yule ni kama vile alikua hanisikii, kabisa.
Baada ya kuchukua ile pasi akamburuta mtoto mpaka jikoni huku kamkaba shingo akachukua kisu then akamkandamiza dogo ukutani akakata waya wa ile pasi kwa kisu kisha akashika ule waya na mkono mmoja na mkono mmoja akamnyanyua dogo kichwa chini miguu juu akarudi nae sebuleni kisha akaanza kumchapa.
Hapo kidogo tumkojo tukakata. Bwana yule akikasirika macho yanakuwa mekundu hadi anatisha na sura yake inakua kama kuna roho fulani ya giza imemuingia. Shindwaaa!
Basi dogo alichapwa kama mwizi. Dogo alichapwa hadi akaacha kulia na damu za puani zikaanza kumtoka.
Nikaona huu ni upuuzi siwezi kuangalia tu kiumbe cha watu kikiuliwa bila hatia hivyo nliivyoona hanisikilizi, nikapanda juu ya meza ili nimfikie vizuri maana ni supa tolu halafu nikamkaba kwa nyuma kwa nguvu zangu zote ili aishiwe pumzi amuachie dogo ila badala yakumuachia dogo akatupa ule waya halafu ule mkono alokua kashikia waya akaniminya kwa nguvu kwenye vidole hadi nikamuachia.
Nilivyomuachia akanishika kwenye shingo ya gauni halafu akaninyanyua kutoka mezani akanishusha chini sakafuni halafu kwa hasira akaniuliza unafanya nini? Nikamwambia muachie mtoto utamuua.
Akasema kwa hiyo wewe unaona ni sawa alichofanya, nikasema sio sawa ila ulivyompiga inatosha. Akasema kwa alichofanya nitampiga mpaka mimi nitakapoona inatosha na wala sitamuacha kisa wewe umesema nimuache.
Sijui hata ilikuaje ila nilijikuta tu nasema, "Najuta kupenda jitu katili kama wewe!" Akasema rudia ulichosema, nikanyamaza. Akanitizama kwa hasira kwa sekunde kadhaa na macho yake mekundu halafu akasema, "Hata wewe ukileta upumbavu nakunyanyua miguu juu kichwa chini nakuchapa kama mtoto mdogo. Tumeelewana?"
Nikanyamaza, akarudia tena, "Tumeelewana?" Nikaona nikiendelea kunyamaza na mimi nitachapwa, nikajibu huku natetemeka "Ndio tumeelewana".
Akamchapa dogo viboko viwili vya nguvu kisha akatupa wapa akamsimamisha kawaida. Cha ajabu dogo alivyosimamishwa tu nilishangaa kapata wapi nguvu za kukimbia hadi chumbani kwangu na mimi nikakurupuka mbio nikamfuatia dogo nyuma nikakimbilia chumbani nikafunga mlango tukamuacha mwenyewe sebuleni. Yule wa kike tulimkuta keshatangulia mvunguni.
Kila akisema nifungue nimpe watoto waondoke watoto wanalia huku wamenikumbatia miguuni wakiomba nisiwatoe na sikuwatoa akaondoka zake akawaacha wakafuatwa siku nyingine.
Sasa ndugu zanguni naombeni mnisaidie jamani. Huyu mtu kaniambia tayari kuwa atanichapa kama mtoto mdogo. Je, ni hasira tu hakumaanisha alichosema au nikiolewa ndio nitakua nimeingia maisha ya kuchapwa kama mtoto mdogo?
Bado nampenda ila namuogopa. Kaniomba msamaha na kasema eti hapigagi wanawake ila kwa nilivyomuona anavyokua akikasirika nahisi kabisa atakua ananichapa huyu.
Kwako Yesu nasimams,
Ndio mwamba ni salama,
Ndio mwamba ni salama🙏.
Duuh!Huyo huwezi kumuacha. Nakumbuka Dada yangu aliolewa na jamaa ambae alikuwa akimpiga mara kwa mara na Dada alikuwa akirudi Nyumbani kwa kukimbia vipigo na wazazi walikuwa wanamrudisha kwa mume wake.
Baada ya mwaka mmoja Dada alishindwana nae wakaachana. Cha ajabu na mtu mwingine aliekuja kumuoa nae anatabia za kitemi kama zile za yule alieachana nae.
Hivyo nilichogundua ni kwamba kuna uhusiano wa moyo wako na aina ya watu unaowapenda. Si ajabu ukipata mwanaume mpole unaweza ukamkinai mapema tu.
Wote walishatangulia mbele za haki mkuuNimempenda sana babu yako mkuu🙏🙏.
Mungu ampe yeye na bibi maisha marefu🙏🙏
Kua nae makini tu.Mwenyewe pia anadai hajawahi na wala hawezi kupiga mwanamke.Anadai aliongea vile sbb ya hasira tu.
kwa hasira za namna hiyo hapana kwa kweli maana anaweza kuua mtuNdugu zangu,
Ijumaa iliyopita mume wangu mtarajiwa alileta watoto wake (wetu) walale kwangu ili Jumamosi nikawafanyie shopping ya mavazi.
Jumamosi nikawawafanyia watoto wetu shopping hadi hela yote alonipa baba yao ikaaisha na baada ya kuridhika kuwa watoto wamepata nguo za kutosha nikaona sio mbaya na mimi nikitoa tu senti twangu kuwapeleka madogo wakale bata.
Hakika mim na wanangu tulikula bata tukafurahi na tukapata new friends from Canada na jioni ilipofika tukarudi zetu home (kwangu) tukalala wote tukiwa na nyuso za furaha.
Japo sio muda mrefu tokea watoto hawa waje katika maisha yangu ila wamekua baraka na darasa kubwa kwangu. Wamenikomaza.
My babies are so cutie and sweet na kila nikiwa nao najisikia huzuni vinapoondoka.
Hawa watoto ni mapacha, wa kike na wa kiume na ni watundu kishenzi na mwanzoni walikua wakiletwa kukaa na mimi nilikua nachanganyikiwa maana nilishazoea naishi mwenyewe hakuna wakunivurugia nyumba ila mara tu baada ya kuwa mama ndo nikaelewa maana ya kuzaa sio kazi bali kulea ndio kazi.
Hawa madogo walikua hawaoni tabu kuchukua jagi la maua na kuanza kurushiana kama mpira na mechi itaisha pale litakapovunjika.
Kuna siku nilikua chumbani nimejipumzisha mchana nikaamshwa na simu ya jiran ananambia kuna mtoto juu ya paa. Kutoka namkuta ni yule wa kiume kafata kitoto cha ndege walikikamata then kikarukia juu ya paa.
Siku nyingine wakaenda kuwapa mbwa Lunch yote kwenye sufuria kisa mlinzi aliwaambia mbwa wanampenda yeye sababu yeye ndo anawapa chakula kwa hiyo walitaka na wao mbwa wawapende.
Yaani ni mambo mengi ila pamoja na utundu wao wote sijawahi kuwaza kuwachapa sababu siamini katika kupiga watoto.
Watu walinishauri sana niwachape ila nilipuuza na nilichofanya ni kuongea nao na kuwaelewesha madhara ya kila kitu kibaya wanachofanya.
Mfano waliharibu blender kwa hiyo kila wakisema mom we want juice nawakumbusha kuwa wameharibu blender kwa hiyo dada hawezi tena kuwasagia juice.
Nikiona wanataka kuharibu remote namuuliza what is your favorite cartoon? Akinijibu namwambia sasa ukiharibu hiyo remote hutaweza tena kuangalia hiyo katuni yako. Unakuta anaacha bila kupigwa na anakua na uelewa.
Namshukuru Mungu mapacha wangu wamebadilika sana na wamepunguza utundu na hata wakija hawanivurugi tena kichwa changu.
Sasa Jumapili mchana wakati baba yao anakuja kuwachukua mimi nilikua chumbani na watoto walikua sebuleni wakiangalia katuni.
Kumbe katuni waliyokua wakiangalia ni katuni fulani hivi yenye character ambae ni katuni mtu mzima baunsa, juu mnene chini mwembamba. Sasa bwana kumbe hiyo katuni sio nzuri maana kuna saa huwa anakua kama anabong'oa halafu anatikisa wowowo ila sikua najua. Wazazi kuweni makini kuna katuni nyingi mbaya.
Sasa nikiwa chumbani nikasikia yule wa kiume akisema neno "sitaki" halafu yule wa kike akasema huwezi. Wa kiume nikasikia akisema nikiamua naweza ila wanaume hawafanyagi hivyo. Yule wa kike akasema, "Mbona huyo (akataja jina la huyo katuni) ni mwanaume na anafanya? Wa kiume akasema ni mwanaume mjinga mbona baba hafanyagi?" Wa kike akamwambia, "Kila kitu huwezi ndio mana shuleni walimu wananisifia mimi sababu najua vitu vingi kuliko wewe, hata bibi anasema wewe unachoweza ni kuharibu tu vitu. Hilooo. Yule wa kiume akasema kwa nguvu na hasira, nawezaaa!
Wa kike akasema huwezi kitu. Wa kiume akasema kwa hasira na kwa sauti ya juu zaid" Nawezaaa! Wa kike akasema "Kama unaweza cheza kidogo nione!
Mpaka hapo nikataka nione kinachoendelea sebuleni sababu maongezi yao yalishanitia mashaka. Nkafungua mlango taratibu kisha nikawa naelekea sebuleni kwa kunyata.
Ile kufika usawa wa kuwaona yule wa kiume akiwa hanion maana alinigeuzia mgongo akasema kwa hasira "Naweza ila sitaki' kisha akaanza kukatika kama ile katuni.
Unaambiwa siku ukitembea uchi ndo siku utakutana na mkweo. Masikini dogo, ile anaanza tu kukatika na baba yake anafungua mlango na kumkuta mwanae wa kiume, jembe lake analolisifia likiwa limebong'oa linakata viuno.
Dogo alivyomuona tu baba yake akajua siku yake ishaharibika Ila hakupanga kufa kizembe. Akarukia kwenye meza. Baba ake akienda huku anakimbilia huku na macho ya dogo yalionyesha target yake ni kukimbilia mlangoni atoke nje lakini baada ya kusumbua kidogo baba yake akamdaka.
Ndugu zanguni. Baada ya huyu mume wangu mtarajiwa kumkamata mwanae ndio nilipoiona sura yake ya ukatili.
Alivyomkamata mwanae akamkaba shingo kwa mkono mmoja huku akimvuta kwa hasira akaenda mpaka iliko pasi yangu akaichukia.
Samahani wapendwa, ila alivyochukua pasi tumkojo tulianza kunitoka maana nilijua anachotaka kukifanya. Kumchoma mtoto na pasi. Nikawa namuombea mtoto msamaha ila bwana yule ni kama vile alikua hanisikii, kabisa.
Baada ya kuchukua ile pasi akamburuta mtoto mpaka jikoni huku kamkaba shingo akachukua kisu then akamkandamiza dogo ukutani akakata waya wa ile pasi kwa kisu kisha akashika ule waya na mkono mmoja na mkono mmoja akamnyanyua dogo kichwa chini miguu juu akarudi nae sebuleni kisha akaanza kumchapa.
Hapo kidogo tumkojo tukakata. Bwana yule akikasirika macho yanakuwa mekundu hadi anatisha na sura yake inakua kama kuna roho fulani ya giza imemuingia. Shindwaaa!
Basi dogo alichapwa kama mwizi. Dogo alichapwa hadi akaacha kulia na damu za puani zikaanza kumtoka.
Nikaona huu ni upuuzi siwezi kuangalia tu kiumbe cha watu kikiuliwa bila hatia hivyo nliivyoona hanisikilizi, nikapanda juu ya meza ili nimfikie vizuri maana ni supa tolu halafu nikamkaba kwa nyuma kwa nguvu zangu zote ili aishiwe pumzi amuachie dogo ila badala yakumuachia dogo akatupa ule waya halafu ule mkono alokua kashikia waya akaniminya kwa nguvu kwenye vidole hadi nikamuachia.
Nilivyomuachia akanishika kwenye shingo ya gauni halafu akaninyanyua kutoka mezani akanishusha chini sakafuni halafu kwa hasira akaniuliza unafanya nini? Nikamwambia muachie mtoto utamuua.
Akasema kwa hiyo wewe unaona ni sawa alichofanya, nikasema sio sawa ila ulivyompiga inatosha. Akasema kwa alichofanya nitampiga mpaka mimi nitakapoona inatosha na wala sitamuacha kisa wewe umesema nimuache.
Sijui hata ilikuaje ila nilijikuta tu nasema, "Najuta kupenda jitu katili kama wewe!" Akasema rudia ulichosema, nikanyamaza. Akanitizama kwa hasira kwa sekunde kadhaa na macho yake mekundu halafu akasema, "Hata wewe ukileta upumbavu nakunyanyua miguu juu kichwa chini nakuchapa kama mtoto mdogo. Tumeelewana?"
Nikanyamaza, akarudia tena, "Tumeelewana?" Nikaona nikiendelea kunyamaza na mimi nitachapwa, nikajibu huku natetemeka "Ndio tumeelewana".
Akamchapa dogo viboko viwili vya nguvu kisha akatupa wapa akamsimamisha kawaida. Cha ajabu dogo alivyosimamishwa tu nilishangaa kapata wapi nguvu za kukimbia hadi chumbani kwangu na mimi nikakurupuka mbio nikamfuatia dogo nyuma nikakimbilia chumbani nikafunga mlango tukamuacha mwenyewe sebuleni. Yule wa kike tulimkuta keshatangulia mvunguni.
Kila akisema nifungue nimpe watoto waondoke watoto wanalia huku wamenikumbatia miguuni wakiomba nisiwatoe na sikuwatoa akaondoka zake akawaacha wakafuatwa siku nyingine.
Sasa ndugu zanguni naombeni mnisaidie jamani. Huyu mtu kaniambia tayari kuwa atanichapa kama mtoto mdogo. Je, ni hasira tu hakumaanisha alichosema au nikiolewa ndio nitakua nimeingia maisha ya kuchapwa kama mtoto mdogo?
Bado nampenda ila namuogopa. Kaniomba msamaha na kasema eti hapigagi wanawake ila kwa nilivyomuona anavyokua akikasirika nahisi kabisa atakua ananichapa huyu.
Kwako Yesu nasimams,
Ndio mwamba ni salama,
Ndio mwamba ni salama🙏.
binafsi, mwanamke akinyoosha mkono juu yangu, there is no guarantee kwamba hatakutana na ngumi tena nzito. hata hivyo, najizuia kwa kumwogopa Mungu tu ila sioni ajabu.Wanaogopa sheria mkuu. Japo hata mimi siwezi kumpiga mwanamke na sijawahi kumuona baba yangu akimpiga mama.
Hapo yeye kwenye kuanza kunyoosha mkono kwangu anaweza kujikuta yupo pale wodini mwaisela aisee.binafsi, mwanamke akinyoosha mkono juu yangu, there is no guarantee kwamba hatakutana na ngumi tena nzito. hata hivyo, najizuia kwa kumwogopa Mungu tu ila sioni ajabu.
Bado sijaelewa unazungumzia niniNimeona umeni follow mara tu baada ya kunikashifu hapa.
Hebu ka unfollow huko nawajua team kidney ze pisi kali mnaniwinda kwendraa