Mungu wa kweli hahitaji haya tunayoaminishwa

Mungu wa kweli hahitaji haya tunayoaminishwa

Habari wakuu!

Mungu wa kweli, mwenye uweza wote, na aliyeumba kila kitu hahitaji mambo yafuatayo:-

1. Hahitaji Zaka wala Sadaka
Mungu wa kweli si mhitaji, uhitaji ni karba ya viumbe. Mungu hana anachohitaji kutoka kwa kiumbe. Yeye ndiye huamua nini kiwe na nini kisiwe. Mungu wa kweli hahitaji sadaka kama watu wengi wanavyoaminishwa. Hahitaji zaka kama wachungaji wanavyosema. Wachungaji wanamsingizia Mungu mambo mengi ikiwemo hili la zaka na sadaka. Wanachoshindwa kusema ni kuwa wao ndio wanahitaji hizo zaka na sadaka kama sehemu ya huduma yao. Ni uongo na dhambi kubwa kusema Mungu anataka sadaka na zaka jambo ambalo linamdhalilisha Mungu muweza wa yote.

Wachungaji, mashehe na viongozi wote wa dini kwa majina yao. Muache kuhadaa watu na kumdhalilisha Mungu. Tutatoa sadaka na zaka kwa kujua kuwa mnatupa huduma za kiroho na si kusema kuwa Mungu anahitaji sadaka na zaka tena fungu la kumi. Kama tunawalipa waalimu, madaktari, wanasheria na kada zingine iweje tusiwalipe nyie. Kwa nini mumsingizie Mungu mambo ya uongo. Eti fungu la kumi ni la Mungu. Si kweli. Mtu atatoa zaka na sadaka kulingana na umuhimu wa huduma anayoipata na si kumtishia vitisho vya uongo.

2. Kafara si ondoleo la dhambi
Watu wameaminishwa kuwa eti ili mtu asamehewe dhambi basi sharti amwage damu. Zamani walimwaga damu ya wanyama lakini sasa hivi wanaamini kuwa Yesu(mtu ninayemheshimu sana) alikufa kwa ajili ya watu jambo ambalo ni uongo. Mungu wa kweli hawezi kufikiri achilia mbali kutenda jambo kama hilo. Hiyo ni mila za kuabudu miungu ya Kiyahudi ambayo msingi wake mkuu umetokana na Abrahamu aliyechukua baadhi ya mila za Kiashuru( kwa sasa ni Syria). Miungu ya Abrahamu ndiyo ilimtaka amtoe Isaka kafara kama ilivyodesturi.

Mungu wa kweli hahitaji mchakato huo kusamehe dhambi, na kumwaga damu si suluhu ya dhambi kuishi. Kwa kutambua hili jambo hili moja kwa moja linaonekana ni wazo la kibinadamu zaidi kuliko la Mungu.

3. Maombi hayabadili chochote kwa Mungu mwenye uweza.
Wachungaji, mashehe na viongozi wa dini wengine kwa majina yao wanawadanganya watu kuwa ukimuomba Mungu jambo lolote anaweza akakupa kitu ambacho si kweli hata kidogo. Vile Mungu alivyopanga kabla hajakuumba ndivyo itakavyokuwa. Kusema kuwa ukimuomba Mungu anabadili mipango yake ni kujidanganya na kupoteza muda. Kumuomba Mungu ni kumfundisha namna ya kufanya mambo yake. Hakuna ushahidi wa moja kwa moja unaoonyesha kuwa mtu akiomba jambo kwa Mungu hupewa isipokuwa ushahidi uliowazi ni kuwa Mtu akifuata maagizo ya Mungu na sheria zake ndio hupata akitakacho. Mungu anataka watu wafuate sheria zake na si kuomba omba tuu.

Hii inamaanisha kuwa viongozi wa dini jukumu lao ni kuwafundisha watu sheria za Mungu na si kuwadanganya waombe au kuwaombea. Kuwaombea watu ni kuwafundisha uvivu. Na kuamini katika hamna.

Ukitaka uamini nikisemacho, kaa ndani omba alafu usiende kufanya kazi uone kama Mungu atakupa ukitakacho, alafu mwenzako asiombe aende kufanya kazi uone nani atapewa/atapata. Hakuna sheria ya Mungu mahali popote kwenye torati inayomtaka mtu aombe. Tafsiri yake nadhani mnaelewa ni nini. Usishangae kwa nini bara la Afrika ni masikini ilhali ndilo linaloongoza kwa waumini wenye kuomba makanisani na misikitini. Jibu unalo.

4. Wachungaji/mashehe na viongozi wa dini si watu pekee wanaotakiwa kuheshimiwa.
Kuna dhana watu huaminishwa kuwa kundi fulani la watu ndilo linalotakiwa kupewa heshima kuliko kundi jingine. Huu ni uongo mkubwa. Mchungaji ni mtumishi kama walivyo watumishi wengine. Anahudumia watu kama wanavyohudumia wengine. Hana uspesho wowote zaidi ya wao kuwahadaa watu wenye akili ndogo na wasioujua ukweli ndio maana wamegeuka watumwa wa makuhani na mashehe. Kila mtu duniani anahitaji heshima ikiwa anafanya kazi ya kuhudumia wengine. Iwe ni fundi nguo, fundi magari, mbunge, mwalimu, muuguzi, mhandisi wote wapo sawa na wote wanategemeana. Kumpa mtu fulani heshima kuliko mwingine si tu kwamba ni ukosefu wa maarifa bali ni kuonyesha hali ya kutoujua ukweli.'

Viongozi wa dini wamejipa hadhi kubwa na kujiona wao ndio wenye mamlaka. Usishangae kiongozi wa dini mjinga akisema kuwa anakulaani kwa Mungu. Nikisiaga hivi huwa nacheka sana. Mtu hupata laana kwa kuacha sheria za Mungu na si maneno ya Mchungaji au mzazi. Kwa ujumla ni kuwa mtu hujilaani yeye mwenyewe ikiwa ataacha sheria za Mungu.

Hivyo watu wamejikuta wakiwaogopa wanadamu wenzao kwa kutoujua ukweli. Unamuogopa mtu aliyezaliwa na mwanamke? Mtu anayehitaji chakula ili apate nguvu ya kuishi. Unakuta mtu anaenda kanisani anaitwa na mchungaji mbele ya kanisa na kutabiriwa vitu vya uongo na yeye anasema kweli wakati sio kweli. Kwa mfano;
Mchungaji: wewe unatatizo la ugumba
muumini: Kweli
Mchungaji: Mama yako anakuloga
Muumini: Kweli
wakati yote ni uongo, anasema kweli kwa uoga na utumwa wa kifikra.

Wito wangu, lazima watu waishi kwa kupendana na kuzishika amri na sheria za Mungu ili wapate kuwa huru na maisha. Vinginevyo tutabaki kuwa watumwa na kuona sisi ni wasindikizaji wakati wengine ndio walioumbiwa huu ulimwengu jambo ambalo si kweli
Namba 3 uko sahihi kabisa..
Mengine sijui


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siyo Mungu anaagiza shetani kuua, bali shetani kwa shetani wanaangamizana wao kwa wao, Mungu anatengeneza njia tu, nimekupa mfano wa Htler na waisrael, huoni baada ya Hitler kuua waisrael kilifuatia nini??!, naye Hitler alisambaratishwa na majeshi ya umoja. Huo ndiyo mpango wa mungu wa namna ya kumtumia shetani.
"Mungu anatengeneza njia " ebu tuambie zipi izo njia Mungu anazotengeneza hili mashetani waangamizane, pili vip mungu aepuke lawama za uuaji wakati yeye ndio bwana mipango ?
 
Jf inawezekana Kuna majini mashetani maagent wa ibilisi wengi sana. Tujihadhari kwa post zao, kwa nn kila siku wanakuja na hoja za kumpinga Mungu.
 
"Mungu anatengeneza njia " ebu tuambie zipi izo njia Mungu anazotengeneza hili mashetani waangamizane, pili vip mungu aepuke lawama za uuaji wakati yeye ndio bwana mipango ?



Ngoja nikupe mfano hai ndipo utaelewa, kulitokea wezi wawili na kila mmoja alikuwa na nia ya kuiba sehemu fulani bila wao kujuana kuhusu jambo hilo lakini wao walikuwa wanafahamiana kwa tabia ya wizi, ikatokea siku moja wakakutana mahali fulani kwa bahati kabla ya kufanya tukio la wizi , walipokutana tu kila mmoja akatambua dhamira ya mwenzake hivyo wakasalimiana lakini kila mmoja akiwa na chuki moyoni juu uwepo wa mwenziwe mahali pale na hii yote ilitokana na kila mmoja kuwa na tamaa ya kutaka kuiba zile mali pekee yake, kilichotokea wakaondoka mahali pale kwa pamoja kirafiki na kwenda falagha kujadiliana huko falagha mmoja akamuwahi mwenzake na kumuua na kabla hajatoroka akashikwa na watu akala kibano kabla ya kuchukuliwa na polisi kwa upelelezi zaidi.

Hapo sasa unaona wahalifu wakidhuriana na kushindwa kutimiza dhamira zao za uhalifu, na ndivyo kama hivyo mipango ya Mungu inavyofanya kazi.
 
1.Fungu la kumi linahitajika kama shukrani kwa MUNGU mkuu nakushauri usome biblia vizuri.
3, Nabishana na wewe.
Mungu kamuumba binadamu ili amtumikie na kumpa uhuru wa kuchagua yeye mwenyewe.
Hata Yesu alifunga kwa hiyo utaona maombi ni muhimu.
Ufalme wa mbingu unapatikana vigumu ndugu so pambana kuutafuta ufalme wa mbinguni.
Kwa namna uliyoweka hapo sidhani kama kungekua na haja ya uwepo wa MUNGU.
 
Habari wakuu!

Mungu wa kweli, mwenye uweza wote, na aliyeumba kila kitu hahitaji mambo yafuatayo:-

1. Hahitaji Zaka wala Sadaka
Mungu wa kweli si mhitaji, uhitaji ni karba ya viumbe. Mungu hana anachohitaji kutoka kwa kiumbe. Yeye ndiye huamua nini kiwe na nini kisiwe. Mungu wa kweli hahitaji sadaka kama watu wengi wanavyoaminishwa. Hahitaji zaka kama wachungaji wanavyosema. Wachungaji wanamsingizia Mungu mambo mengi ikiwemo hili la zaka na sadaka. Wanachoshindwa kusema ni kuwa wao ndio wanahitaji hizo zaka na sadaka kama sehemu ya huduma yao. Ni uongo na dhambi kubwa kusema Mungu anataka sadaka na zaka jambo ambalo linamdhalilisha Mungu muweza wa yote.

Wachungaji, mashehe na viongozi wote wa dini kwa majina yao. Muache kuhadaa watu na kumdhalilisha Mungu. Tutatoa sadaka na zaka kwa kujua kuwa mnatupa huduma za kiroho na si kusema kuwa Mungu anahitaji sadaka na zaka tena fungu la kumi. Kama tunawalipa waalimu, madaktari, wanasheria na kada zingine iweje tusiwalipe nyie. Kwa nini mumsingizie Mungu mambo ya uongo. Eti fungu la kumi ni la Mungu. Si kweli. Mtu atatoa zaka na sadaka kulingana na umuhimu wa huduma anayoipata na si kumtishia vitisho vya uongo.

2. Kafara si ondoleo la dhambi
Watu wameaminishwa kuwa eti ili mtu asamehewe dhambi basi sharti amwage damu. Zamani walimwaga damu ya wanyama lakini sasa hivi wanaamini kuwa Yesu(mtu ninayemheshimu sana) alikufa kwa ajili ya watu jambo ambalo ni uongo. Mungu wa kweli hawezi kufikiri achilia mbali kutenda jambo kama hilo. Hiyo ni mila za kuabudu miungu ya Kiyahudi ambayo msingi wake mkuu umetokana na Abrahamu aliyechukua baadhi ya mila za Kiashuru( kwa sasa ni Syria). Miungu ya Abrahamu ndiyo ilimtaka amtoe Isaka kafara kama ilivyodesturi.

Mungu wa kweli hahitaji mchakato huo kusamehe dhambi, na kumwaga damu si suluhu ya dhambi kuishi. Kwa kutambua hili jambo hili moja kwa moja linaonekana ni wazo la kibinadamu zaidi kuliko la Mungu.

3. Maombi hayabadili chochote kwa Mungu mwenye uweza.
Wachungaji, mashehe na viongozi wa dini wengine kwa majina yao wanawadanganya watu kuwa ukimuomba Mungu jambo lolote anaweza akakupa kitu ambacho si kweli hata kidogo. Vile Mungu alivyopanga kabla hajakuumba ndivyo itakavyokuwa. Kusema kuwa ukimuomba Mungu anabadili mipango yake ni kujidanganya na kupoteza muda. Kumuomba Mungu ni kumfundisha namna ya kufanya mambo yake. Hakuna ushahidi wa moja kwa moja unaoonyesha kuwa mtu akiomba jambo kwa Mungu hupewa isipokuwa ushahidi uliowazi ni kuwa Mtu akifuata maagizo ya Mungu na sheria zake ndio hupata akitakacho. Mungu anataka watu wafuate sheria zake na si kuomba omba tuu.

Hii inamaanisha kuwa viongozi wa dini jukumu lao ni kuwafundisha watu sheria za Mungu na si kuwadanganya waombe au kuwaombea. Kuwaombea watu ni kuwafundisha uvivu. Na kuamini katika hamna.

Ukitaka uamini nikisemacho, kaa ndani omba alafu usiende kufanya kazi uone kama Mungu atakupa ukitakacho, alafu mwenzako asiombe aende kufanya kazi uone nani atapewa/atapata. Hakuna sheria ya Mungu mahali popote kwenye torati inayomtaka mtu aombe. Tafsiri yake nadhani mnaelewa ni nini. Usishangae kwa nini bara la Afrika ni masikini ilhali ndilo linaloongoza kwa waumini wenye kuomba makanisani na misikitini. Jibu unalo.

4. Wachungaji/mashehe na viongozi wa dini si watu pekee wanaotakiwa kuheshimiwa.
Kuna dhana watu huaminishwa kuwa kundi fulani la watu ndilo linalotakiwa kupewa heshima kuliko kundi jingine. Huu ni uongo mkubwa. Mchungaji ni mtumishi kama walivyo watumishi wengine. Anahudumia watu kama wanavyohudumia wengine. Hana uspesho wowote zaidi ya wao kuwahadaa watu wenye akili ndogo na wasioujua ukweli ndio maana wamegeuka watumwa wa makuhani na mashehe. Kila mtu duniani anahitaji heshima ikiwa anafanya kazi ya kuhudumia wengine. Iwe ni fundi nguo, fundi magari, mbunge, mwalimu, muuguzi, mhandisi wote wapo sawa na wote wanategemeana. Kumpa mtu fulani heshima kuliko mwingine si tu kwamba ni ukosefu wa maarifa bali ni kuonyesha hali ya kutoujua ukweli.'

Viongozi wa dini wamejipa hadhi kubwa na kujiona wao ndio wenye mamlaka. Usishangae kiongozi wa dini mjinga akisema kuwa anakulaani kwa Mungu. Nikisiaga hivi huwa nacheka sana. Mtu hupata laana kwa kuacha sheria za Mungu na si maneno ya Mchungaji au mzazi. Kwa ujumla ni kuwa mtu hujilaani yeye mwenyewe ikiwa ataacha sheria za Mungu.

Hivyo watu wamejikuta wakiwaogopa wanadamu wenzao kwa kutoujua ukweli. Unamuogopa mtu aliyezaliwa na mwanamke? Mtu anayehitaji chakula ili apate nguvu ya kuishi. Unakuta mtu anaenda kanisani anaitwa na mchungaji mbele ya kanisa na kutabiriwa vitu vya uongo na yeye anasema kweli wakati sio kweli. Kwa mfano;
Mchungaji: wewe unatatizo la ugumba
muumini: Kweli
Mchungaji: Mama yako anakuloga
Muumini: Kweli
wakati yote ni uongo, anasema kweli kwa uoga na utumwa wa kifikra.

Wito wangu, lazima watu waishi kwa kupendana na kuzishika amri na sheria za Mungu ili wapate kuwa huru na maisha. Vinginevyo tutabaki kuwa watumwa na kuona sisi ni wasindikizaji wakati wengine ndio walioumbiwa huu ulimwengu jambo ambalo si kweli
Siri zipo hapa Vatican Inamiliki Dunia - JamiiForums
 
Ngoja nikupe mfano hai ndipo utaelewa, kulitokea wezi wawili na kila mmoja alikuwa na nia ya kuiba sehemu fulani bila wao kujuana kuhusu jambo hilo lakini wao walikuwa wanafahamiana kwa tabia ya wizi, ikatokea siku moja wakakutana mahali fulani kwa bahati kabla ya kufanya tukio la wizi , walipokutana tu kila mmoja akatambua dhamira ya mwenzake hivyo wakasalimiana lakini kila mmoja akiwa na chuki moyoni juu uwepo wa mwenziwe mahali pale na hii yote ilitokana na kila mmoja kuwa na tamaa ya kutaka kuiba zile mali pekee yake, kilichotokea wakaondoka mahali pale kwa pamoja kirafiki na kwenda falagha kujadiliana huko falagha mmoja akamuwahi mwenzake na kumuua na kabla hajatoroka akashikwa na watu akala kibano kabla ya kuchukuliwa na polisi kwa upelelezi zaidi.

Hapo sasa unaona wahalifu wakidhuriana na kushindwa kutimiza dhamira zao za uhalifu, na ndivyo kama hivyo mipango ya Mungu inavyofanya kazi.
Itakuaje kama Mungu ndio kafanya wale wawe waharifu kwa uwezo wake aliokuwa nao ?
 
Nikweli mungu hana njaa ya hivyo vitu, ila wapo viumbe wanaohitaji misaada. Mi sadaka huwa nawapa wanaohitaji. maskini na mafukara. kama nitapeleka kwenye nyumba za ibada nitapeleka kwa lemgo la kuchangia labda ujenzi NK.
 
Yesu Kristo alipokuja Kwenye agano jipya mbona hajazungumzia kuhusu swala la zaka?
Kama kuna mahali alizingumzia Naomba Mwenye andiko anipe
 
Halafu agano la kale limeanisha matumizi ya zaka !
Mfano kutegemeza wajane na yatima n.k
Swali ni Je yanafanyika hayo?
Kwa asilimia ngapi ?
 
Mimi nazani kuna haja ya kuwepo na sheria ya kufanya auditing ya hesabu za taasisi zote Za kidini !
Ili kuona mambo Yao yanavyo endeshwa
 
Halafu bora hata wangekuwa wanafungua hospitals na Shule na huduma nyingine Za jamii ambazo wananchi wangeweza kupata huduma kwa unafuu lakini wala!
 
Oneni Kakobe alivyo kutwa na zile billioni Za pesa [emoji87][emoji87][emoji87]
Lakini waumini wengine hata nauli hawana, wamechoka ile mbaya!
Angefungua hospital ambayo baadae ingeleta faida pia
 
Halafu Siku hizi mahubiri ya utoaji sadaka ndo yameshika kasi kweli kweli na changizo!
 
Mahubiri ya utaua na utakatifu yamekuwa adimu!
Wewe vaa hata robo tatu uchi hakuna atakae kuonya wala kukemea
 
Unakuta yuko kanisani amevaa utazani yuko night club [emoji87][emoji87][emoji87]
Cha ajabu hakuna wa kumuonya wala nini!
Hapana naona si Sawa hata kidogo!
 
Halafu kumejengeka misingi ya nidhamu ya woga kwa kiwango cha hali ya Juu kiasi Kwamba Mtu akijaribu kuhoji anaonekana muasi!
Kitakachofuata ni kutengwa!
Mioyo wa wanadamu hii Mmnh !
 
Back
Top Bottom