Utangulizi - Mambo ya nyakati ni nini?
Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati kinatueleza kuhusu ibada katika hekalu na kinatupa habari zaidi kuhusu ukoo wa Masihi. Kikiwa sehemu ya Neno la Mungu lililoongozwa kwa roho, ujumbe wake unaimarisha imani yetu na kuboresha uelewaji wetu wa Biblia
Mbali na rekodi za ukoo, Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati kinasimulia matukio ya kipindi cha miaka 40 hivi, tangu kifo cha Mfalme Sauli mpaka kifo cha Mfalme Daudi. Inaaminika kwamba kuhani Ezra ndiye aliyeandika kitabu hicho mwaka wa 460 K.W.K
Baada ya utangulizi huo sasa fungua Biblia yako Mambo ya Nyakati 1 sura ya 6 mstari wa 19 unasema
"Wana wa Merari walikuwa Mali na Mushi. Na hizi ndizo zilizokuwa familia za Walawi kulingana na mababu zao":
Lawi au walawi ni watu gani katika historia ya biblia?
Wametoka katika ukoo wa Aroni (au Haruni), aliyekuwa wa kabila la Lawi. Kitabu cha mambo ya walawi kinaelezea amri na maagizo ya Mungu kwa Wanaisraeli hasa sheria za ibada zenye kulenga utakatifu wa makuhani na wa sadaka.
Tujadiliane:
Tunaambiwa katika miaka hiyo ya uhamisho wa babilon Mushi na wana ukoo wake alikuja na kuishi katika mlima kilimanjaro; walizaliana sana sana wengine wakawa upande wa pili wa milima yaani Kenya hawa ndiyo wakikuyu na wengine wakawa upande huu wa Mlima yaani Tanzania hawa ndiyo wa-Mushi.
Je kuna ukweli hapa? hebu angalia makabla 12 ya wana wa Islaeli je Lawi anaonekana ambaye ndiye Mushi?
Kabila 12 za Israel: Je Lawi yumo?
Makabila hayo yalitokana na wana wa kiume 12 wa babu Yakobo, bin Isaka na mjukuu wa Abrahamu. Ni Yakobo aliyepewa kwanza jina la Israeli.
Ibrahim alimzaa Isaka, Isaka akamzaa Yakobo, Yakobo naye akazaa watoto 12 ambayo ndiyo makabila 12 ya Israel. Kwenye mabano ni maana ya jina:
1. Reubeni (Ona)
2. Simeoni. (Sikia)
3. Lawi. (Ungana)
4. Yuda. (Sifu)
5. Dani. (Haki)
6. Naftali. (Mashindano)
7. Gadi. (Bahati Njema)
8. Asheri. (Heri, Furaha)
9. Isakari. (Ujira, Zawadi)
10. Zabuloni. (Zawadi ya Thamani sana)
11.Yusufu (Ongeza)
12. Benjamini (Mwana wa mkono wa kulia)
Sasa unaona kwamba LAWI kumbe ni mtoto wa tatu wa Yakobo, maana ya jina lake ni Ungana - na ndiyo maana wa-islaeli wakicheza ngoma ya kwao wanaunganisha mikono yao hali kadhaika wachaga ni vivyo hivyo.
Tujadili, yawezekana wenzetu hawa ni WALAWI; wanatokana na mtoto Lawi katika ukoo wa Ibrahimu; Yakobo baba yetu.
Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati kinatueleza kuhusu ibada katika hekalu na kinatupa habari zaidi kuhusu ukoo wa Masihi. Kikiwa sehemu ya Neno la Mungu lililoongozwa kwa roho, ujumbe wake unaimarisha imani yetu na kuboresha uelewaji wetu wa Biblia
Mbali na rekodi za ukoo, Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati kinasimulia matukio ya kipindi cha miaka 40 hivi, tangu kifo cha Mfalme Sauli mpaka kifo cha Mfalme Daudi. Inaaminika kwamba kuhani Ezra ndiye aliyeandika kitabu hicho mwaka wa 460 K.W.K
Baada ya utangulizi huo sasa fungua Biblia yako Mambo ya Nyakati 1 sura ya 6 mstari wa 19 unasema
"Wana wa Merari walikuwa Mali na Mushi. Na hizi ndizo zilizokuwa familia za Walawi kulingana na mababu zao":
Lawi au walawi ni watu gani katika historia ya biblia?
Wametoka katika ukoo wa Aroni (au Haruni), aliyekuwa wa kabila la Lawi. Kitabu cha mambo ya walawi kinaelezea amri na maagizo ya Mungu kwa Wanaisraeli hasa sheria za ibada zenye kulenga utakatifu wa makuhani na wa sadaka.
Tujadiliane:
Tunaambiwa katika miaka hiyo ya uhamisho wa babilon Mushi na wana ukoo wake alikuja na kuishi katika mlima kilimanjaro; walizaliana sana sana wengine wakawa upande wa pili wa milima yaani Kenya hawa ndiyo wakikuyu na wengine wakawa upande huu wa Mlima yaani Tanzania hawa ndiyo wa-Mushi.
Je kuna ukweli hapa? hebu angalia makabla 12 ya wana wa Islaeli je Lawi anaonekana ambaye ndiye Mushi?
Kabila 12 za Israel: Je Lawi yumo?
Makabila hayo yalitokana na wana wa kiume 12 wa babu Yakobo, bin Isaka na mjukuu wa Abrahamu. Ni Yakobo aliyepewa kwanza jina la Israeli.
Ibrahim alimzaa Isaka, Isaka akamzaa Yakobo, Yakobo naye akazaa watoto 12 ambayo ndiyo makabila 12 ya Israel. Kwenye mabano ni maana ya jina:
1. Reubeni (Ona)
2. Simeoni. (Sikia)
3. Lawi. (Ungana)
4. Yuda. (Sifu)
5. Dani. (Haki)
6. Naftali. (Mashindano)
7. Gadi. (Bahati Njema)
8. Asheri. (Heri, Furaha)
9. Isakari. (Ujira, Zawadi)
10. Zabuloni. (Zawadi ya Thamani sana)
11.Yusufu (Ongeza)
12. Benjamini (Mwana wa mkono wa kulia)
Sasa unaona kwamba LAWI kumbe ni mtoto wa tatu wa Yakobo, maana ya jina lake ni Ungana - na ndiyo maana wa-islaeli wakicheza ngoma ya kwao wanaunganisha mikono yao hali kadhaika wachaga ni vivyo hivyo.
Tujadili, yawezekana wenzetu hawa ni WALAWI; wanatokana na mtoto Lawi katika ukoo wa Ibrahimu; Yakobo baba yetu.
Last edited: