Musiba: Mawasiliano ndani ya Vyama vya Siasa, watu wanayaona! Mnyika asaidie Polisi kwenye Uchunguzi wa kuuawa kwa Mzee Kibao

Musiba: Mawasiliano ndani ya Vyama vya Siasa, watu wanayaona! Mnyika asaidie Polisi kwenye Uchunguzi wa kuuawa kwa Mzee Kibao

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Mwanaharakati huru kama anavyojiita, Cyprian Musiba amesema kama mtanzania ameumia sana na matukio ya utekaji na kupotezwa kwa watu hususan tukio la hivi karibuni la kuuawa kwa Ali Mohammed Kibao. Hata hivyo, amesema kama mtanzania anapinga kutumia matukio kama haya kuanza kushambulia watu baadhi ambao hawana makosa yoyote huku akishauri kusubiri ripoti kutoka kwa Vyombo vya Usalama na si kutumia matukio haya kisiasa na kuingiza chuki sababu ya watu binafsi.

Amesema "Ripoti haijatoka hajapelekewa Rais, tayari watu wameshaanza fukuza huyu, fukuza huyu, haiwezekani. Wanachosahau Vyama vya Siasa wanadhani wana Serikali yao na Wananchi wao. Ninachoweza kuwaambia ni kwamba hata ninyi mpo uchi, unaweza kuilaumu Serikali kuwa imefanya jambo fulani kumbe hata ninyi ndio mmefanya. Ninachoshauri tu mkileta tuhuma na kutengenza vipeperushi kuwa fukuza huyu, fukuza huyu hata ninyin mpo uchi. Hata ninyi huko ndani kwenye vyama vyenu kuna kamera zinawaona, mawasiliano yenu wanayaona watu. Mnaweza mkatuhumu watu, hizo tuhuma zikageuka. Mie nawatahadharisha na kuwashauri tu."

Aidha, kuhusiana na tukio la Mzee Ali Mohammed Kibao amesema anashauri yeye kama yeye kuwa kwenye uchunguzi mmoja wa Watu wanaotakiwa kusaidia Polisi ni Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika kwa sababu yeye ndio alikuwa mtu wa kwanza kutoa taarifa na kuzisambaza.

Amehoji "Nani aliyempa taarifa kuwa huyo jamaa kuwa kuna watu wanamteka? Huyu aliyempa taarifa Katibu Mkuu naya anaweza akasaidia Vyombo vyetu. Huyo aliyotea taarifa kuwa Mzee Kibao ameuawa naye anaweza akasaidia "

Ameongeza kuwa uchunguzi sio kwasababu ya Serikali tu, kwani inaangaliwa nani ameanza kutoa taarifa, kwenye basi kulikuwa na nani?, aliyewasiliana na Mnyika akiwa kwenye basi ni nani? Amesema hayo ni mambo ya msingi sana ya kuzingatia kwa sababu Katibu wa Chama amaeanza kutoa taarifa hivyo asaidie.

Amemalizia "Mimi nashauri hapa si kwa nia mbaya, maana mtaanza kunitukana hapa na kunidhalilisha hapa ila ni kwa nia njema"

Amesisitiza "Lazima tulinde hadhi ya Urais, sio kila Mtu anaweza kuongea ongea tu, unamtukana Rais. Nafuatilia rafiki yangu mmoja yupo CHADEMA, siwezi kumtaja jina yeye kila akiamka ni kumtukana Rais tu, anamtukana tu. Na yupo tu wala hakuna mtu anayemjali. Kwenye page yake yeye ni kumtukana tu lakini la kumshukuru Mungu hakuna anayemjali maana inawezekana anataka akamatwe ila watu wamemwacha hakuna naye mjali na sasa ameanza kuchoka. Sio kila kitu anahusika Rais"​
 
Anataka kutumia tukio la kuuawa kwa mzee kurudi ulingoni sio?

Sawa, haya kayasemea wapi?
Irrelevant maana alitekwa hadharani kwenye bus lenye watu wengi, Konda na wahudumu la bus wanamjua na mteja wao wa siku nyingi kama walivyokiri.

Pili mnyika ni Kiongozi mkubwa na huyu Mzee alikua msaidizi wake.

Kwa hayo TU inatosha kutuambia kwa nini alipewa taarifa mapema na alitaka kujua alipo msaidizi wake.

Kuhusu eti Kuna video, sijui vinasa sauti. Nenda kasome Sheria Personal Data Protection utajifunza kitu sio kuropoka tu
 
Mwanaharakati huru kama anavyojiita, Cyprian Musiba amesema kama mtanzania ameumia sana na matukio ya utekaji na kupotezwa kwa watu hususan tukio la hivi karibuni la kuuawa kwa Ali Mohammed Kibao. Hata hivyo, amesema kama mtanzania anapinga kutumia matukio kama haya kuanza kushambulia watu baadhi ambao hawana makosa yoyote huku akishauri kusubiri ripoti kutoka kwa Vyombo vya Usalama na si kutumia matukio haya kisiasa na kuingiza chuki sababu ya watu binafsi.

Amesema "Ripoti haijatoka hajapelekewa Rais, tayari watu wameshaanza fukuza huyu, fukuza huyu, haiwezekani. Wanachosahau Vyama vya Siasa wanadhani wana Serikali yao na Wananchi wao. Ninachoweza kuwaambia ni kwamba hata ninyi mpo uchi, unaweza kuilaumu Serikali kuwa imefanya jambo fulani kumbe hata ninyi ndio mmefanya. Ninachoshauri tu mkileta tuhuma na kutengenza vipeperushi kuwa fukuza huyu, fukuza huyu hata ninyin mpo uchi. Hata ninyi huko ndani kwenye vyama vyenu kuna kamera zinawaona, mawasiliano yenu wanayaona watu. Mnaweza mkatuhumu watu, hizo tuhuma zikageuka. Mie nawatahadharisha na kuwashauri tu."

Aidha, kuhusiana na tukio la Mzee Ali Mohammed Kibao amesema anashauri yeye kama yeye kuwa kwenye uchunguzi mmoja wa Watu wanaotakiwa kusaidia Polisi ni Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika kwa sababu yeye ndio alikuwa mtu wa kwanza kutoa taarifa na kuzisambaza.

Amehoji "Nani aliyempa taarifa kuwa huyo jamaa kuwa kuna watu wanamteka? Huyu aliyempa taarifa Katibu Mkuu naya anaweza akasaidia Vyombo vyetu. Huyo aliyotea taarifa kuwa Mzee Kibao ameuawa naye anaweza akasaidia "

Ameongeza kuwa uchunguzi sio kwasababu ya Serikali tu, kwani inaangaliwa nani ameanza kutoa taarifa, kwenye basi kulikuwa na nani?, aliyewasiliana na Mnyika akiwa kwenye basi ni nani? Amesema hayo ni mambo ya msingi sana ya kuzingatia kwa sababu Katibu wa Chama amaeanza kutoa taarifa hivyo asaidie.

Amemalizia "Mimi nashauri hapa si kwa nia mbaya, maana mtaanza kunitukana hapa na kunidhalilisha hapa ila ni kwa nia njema"

Amesisitiza "Lazima tulinde hadhi ya Urais, sio kila Mtu anaweza kuongea ongea tu, unamtukana Rais. Nafuatilia rafiki yangu mmoja yupo CHADEMA, siwezi kumtaja jina yeye kila akiamka ni kumtukana Rais tu, anamtukana tu. Na yupo tu wala hakuna mtu anayemjali. Kwenye page yake yeye ni kumtukana tu lakini la kumshukuru Mungu hakuna anayemjali maana inawezekana anataka akamatwe ila watu wamemwacha hakuna naye mjali na sasa ameanza kuchoka. Sio kila kitu anahusika Rais"​
sure taarifa official za mwanzo wa utekaji zilitokea HQ ya chama mapema na kwa wakati muafaka sana,

vile vile Taarifa official za kuuawa kikatili kwa kamanda Ally Kibao zilitokea HQ ya chama mapema sana tena kwa WAKATI muafaka sana...

surely,
HQ haina taarifa official za hapa katikati mateka alitendewa nini na wahusika? sio HQ kweli kumzima mdomo kamanda Ally Kibao asizuie mtu kushinda uchaguzi ingawa hana hoja wala uhalali?🐒
 
Back
Top Bottom