Mustafa Mkulo atoka mbio kukwepa ghadhabu ya wananchi Dumila

Mustafa Mkulo atoka mbio kukwepa ghadhabu ya wananchi Dumila

Na hao wananchi wapigwe tu, maana tumeshachoka...M.P.K.PINDA(MB) - 2013
 
hao wananchi wanafiki walipokuwa wanahongwa kanga na kofia na elfu ishirini walikuwa hajui km itaji muhimu kuliko hzo kofia na khanga, imekula kwao hao ndy magamba
 
Wana bodi,

Naamini wengi mnapajua Dumila. Mji huu upo katka wilaya ya Kilosa, jimbo linaloongozwa na Mustapha Mkulo.
Leo hii takriban saa moja lililopita Mhe. Mkulo amelazimika kukimbia kabisaaa (Namaanisha kukimbia) pale wananchi wa mji huu walipoanza kupaza sauti za kumzomea baada ya kutoa majibu mabaya juu ya mradi wa maji ambao yeye aliahidi kutoa Tsh 5,000,000 toka katika Mfuko wa Jimbo tangu mwaka 2011 lakin hadi leo hajatoa na aliwahi kunukuliwa akisema hatatoa kwa madai kwamba alitukanwa na katibu wa CCM wa wilaya.

Majibu yake kwamba "... sitoi hela mpaka katibu aniombe msamaha kwa maandishi..." ndo yakaibua hasira za wananchi ambao mwaka huo wa 2011 walilazimishwa kwa vipigo kutoa kila mtu Sh 3500 tofauti na makubaliano ya kuchangia sh 2000 kwa kaya... pesa ambazo nazo zimeliwa.

Mkulo kadandia gari yake aina ya Range Rover Vogue na kutimka.

Nikiweza ntaleta picha

Huo ni uongo. Si kweli.
 
Huo ni uongo kabisa. Hata ukimdanganya Mtoto aliyetumboni mwa mama yake ataukataa na ataanza kucheza tumboni mwa mama yake kupinga uongo kama huo. Sijui kama unasema uongo kiasi hicho watoto wako wanajifunza nini kutoka kwako. Kwanza haiingii akilini uongo wako huo kugeuka ukweli.

haya mzee mkullo tueleze namna ulivyoondoka.......
 
mkulo ni fisadi na hao wananchi wanapaswa kupanga revange yeye si kakimbia na RANGE asiludi tena huko
 
Wangempiga tu hilo Vogue wangelivunjavunja; fisadi mkubwa huyu!!!
 
UPDATES=======

Mkulo atangaza vita na CCM Kilosa... Ni matokeo ya mkutano wake wa hadhara na kikao cha ndani cha ccm Dumila jana. Amemtukana diwani wa Dumila, bwana Japhet Kasanga kwamba *ameolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri, bwana Ameir (ambaye ana interest na jimbo 2015). Baada ya kuzomewa na kutimka mbio jana, ametoa taarifa kwa mara nyingine kwamba HATAGOMBEA TENA na amekilaani chama chake kwamba kitapoteza Halmashauri hiyo 2015 na ameapa kutowapa ushirikiano wowote.

My take:
Mzee anaonekana kujaa stress za kuukosa uwaziri...
 
Huyu Mzee alishawahi kumtaifisha gf wa mshkaji wakati tuko sekondari.

Zee zima na watoto likawa linajirusha na kitoto cha sekondari kidogo kuliko wanawe.

Tangu hapo nikajua hapa bogus. Kwa hiyo haya mengine nikiyasikia hata sishangai.
 
Back
Top Bottom