CHA The GREAT
JF-Expert Member
- Nov 11, 2010
- 651
- 854
Muswada wa Sheria ya Fao La Kukosa Ajira Huu Hapa
Ule mbadala wa fao la kujitoa ambao umekuwa ukisemwa na mamlaka ya udhibiti na uendeshaji wa mifuko ya hifadhi ya jamii nchini SSRA, na wakati fulani waziri wa nchi, ofisi ya waziri mkuu (sera, uratibu na bunge), Jenista Mhagama sasa umepatikana.
Tarehe 12/Mei/2017, waziri huyo mwenye dhamana ya wizara inayohusika na masuala ya ajira na vijana--alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kwamba fao la kujitoa kwa sasa limefutwa na badala yake kutakuwa na fao la kukosa ajira.
Mbali na waziri Mhagama, pia Rais John Pombe Magufuli naye alilizungumzia fao la kukosa ajira kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani zilizofanyika kitaifa mkoani Kilimanjaro, tarehe 1/Mei/2017. Katika kulizungumzia fao la kukosa ajira Rais Magufuli aliwatoa wasiwasi wafanyakazi akiahidi kwamba mambo yatakuwa mazuri.
Ufuatao ni muswada na utaratibu wa fao la kukosa ajira (unemployment benefits) kwa mifuko yote ya jamii nchini, ambayo inadhibitiwa na kusimamiwa na mamlaka ya SSRA.
Kwamba, iwapo mtu atapoteza ajira, kwa mujibu wa muswada huu ambao kama utatiwa saini na Rais ndiyo itakuwa sheria, ni kuwa mfuko husika mfano NSSF, PPF au LAPF unalazimika kumlipa mwanachama wake asilimia kumi na nane na nusu (18.5%) ya mshahara wake wa mwisho kwa kipindi cha miezi sita.
Ikitokea mwanachama huyo hajapata ajira baada ya kipindi hicho cha miezi sita tangu kupoteza ajira, basi mwanachama huyo atalipwa asilimia kumi na sita na nusu (16.5%) ya salio lililobaki kutokana na malipo ya asilimia kumi na nane na nusu (18.5%) yaliyofanyika kwa miezi sita.
Mfano unalipwa mshahara wa Tsh. 300,000/- (laki tatu), basi hesabu yake ni asilimia kumi na nane na nusu (18.5%) ya Tsh. 300,000/- (laki tatu) kwa kila mwezi kwa miezi sita.
Na ikitokea kwa bahati mbaya mwanachama hakupata ajira baada ya miezi 6, basi mfuko unamlipa mwanachama huyo asilimia kumi na sita na nusu (16.5%) ya kiasi kilichobaki baada ya malipo ya asilimia kumi na nane na nusu (18.5%) yaliyofanyika kwa miezi sita.
Mfano salio lako ni Tsh. 2,000,000/- (milioni mbili) baada ya kulipwa asilimia kumi na nane na nusu (18.5%) kwa miezi sita, basi asilimia kumi na sita na nusu (16.5%) ya hiyo milioni mbili iliyobaki, ndiyo mwanachama atapewa na kiasi kitakachobaki kitakuwa granted kwa mwanachama pale atakapofikisha umri wa kustaafu kwa hiyari au lazima--miaka 55 ama--miaka 60; vinginevyo mwanachama aendeleze uanachama atakapopata ajira mpya au kujiajiri.
Kwa mujibu wa muswada huu, wale wanaoacha kazi wenyewe (resignation) watapewa asilimia kumi na nne tu (14%) ya michango yao kwa kipindi chote ambacho wamekuwa wakichangia mfuko; na kiasi kitakachobaki kitakuwa granted pale mwanachama atakapofikisha umri wa kustaafu.
Aidha, kwa wale ambao wamechangia mfuko chini ya miezi 18 (kumi na nane) ikitokea wamepoteza ajira kwa kufukuzwa au kupunguzwa kazini, wao watalipwa asilimia arobaini (40%) ya mafao yao na salio litakalobaki litatolewa kwa mwanachama pale atakapofikisha umri wa kustaafu aidha kwa lazima au kwa hiyari.
Muswada huu iwapo ukasainiwa na Rais na kuwa sheria, maana yake sheria hii mpya itakuwa imefuta sheria ya sasa ya mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo inamruhusu mtu kuchukua mafao yake pale anapopoteza ajira, licha ya kusemwa kuwa sheria hii ilishafutwa.
Kwa mujibu wa sheria ya hifadhi ya mifuko ya jamii ya mwaka 2002, kifungu na: 44 (1) imeainishwa kuwa, ikitokea mtu kapoteza ajira, basi michango yake yote pamoja na ile ambayo mwajiri alikuwa akichangia kwa mfuko kwa ajili ya mtu huyo, itatolewa kwa mtu huyo ambaye kapoteza ajira.
MKANGANYIKO:
Kabla ya muswada huu ambao umevuja, watu walipopoteza ajira na kuamua kufuatilia mafao yao, wamekuwa wakiambiwa kwamba…sheria ya fao la kujitoa imefutwa. Lakini wakati wakiambiwa hivyo, watu ambao wamekuwa wakipunguzwa makazini (redundancy) wao wamekuwa wakipewa mafao yao. Ila kwa wale waliopoteza ajira kwa misingi ya kufukuzwa na mwajiri, wamekuwa wakinyimwa mafao yao kwa sababu ambazo hazikuwa zikiwekwa wazi.
KIMAHESABAU:
Kutokana na ukokotoaji, hesabu zinaonesha kuwa; malipo ya miezi sita yatakayokuwa yakifanywa chini ya mpango huu, pamoja na malipo ya asilimia kumi na sita na nusu (16.5%) ni sawa na mshahara wa mtu kwa miezi miwili na nusu.
Suala la fao la kujitoa lilileta mtafaruku mwishoni mwa mwaka jana hali iliyopelekea shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini TUCTA chini ya katibu mkuu Nicolas Mgaya, kutamka wazi kuwa shirikisho hilo lingeitisha mgomo wa wafanyakazi nchi nzima, na kuiburuza serikali mahakamani iwapo ingefuta fao hilo la kujitoa ambalo limeonekana kuwa mkombozi kiuchumi kwa wafanyakazi kutokana na mazingira ya ajira nchini kutokuwa rafiki.
Hoja zilizotolewa na TUCTA kutaka fao la kujitoa lisifutwe zilizingatia mazingira ya ajira nchini kwamba, ajira hasa sekta binafsi si za uhakika, malipo kidogo ya mishahara kitu kinachopelekea watu washindwe kuweka akiba hivyo kulifuta fao hilo itakuwa ni kuumiza watu ambao fao la kujitoa hulitumia kujiendeleza kielimu, kujiajiri na hata kujikimu kimaisha.
Ule mbadala wa fao la kujitoa ambao umekuwa ukisemwa na mamlaka ya udhibiti na uendeshaji wa mifuko ya hifadhi ya jamii nchini SSRA, na wakati fulani waziri wa nchi, ofisi ya waziri mkuu (sera, uratibu na bunge), Jenista Mhagama sasa umepatikana.
Tarehe 12/Mei/2017, waziri huyo mwenye dhamana ya wizara inayohusika na masuala ya ajira na vijana--alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kwamba fao la kujitoa kwa sasa limefutwa na badala yake kutakuwa na fao la kukosa ajira.
Mbali na waziri Mhagama, pia Rais John Pombe Magufuli naye alilizungumzia fao la kukosa ajira kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani zilizofanyika kitaifa mkoani Kilimanjaro, tarehe 1/Mei/2017. Katika kulizungumzia fao la kukosa ajira Rais Magufuli aliwatoa wasiwasi wafanyakazi akiahidi kwamba mambo yatakuwa mazuri.
Ufuatao ni muswada na utaratibu wa fao la kukosa ajira (unemployment benefits) kwa mifuko yote ya jamii nchini, ambayo inadhibitiwa na kusimamiwa na mamlaka ya SSRA.
Kwamba, iwapo mtu atapoteza ajira, kwa mujibu wa muswada huu ambao kama utatiwa saini na Rais ndiyo itakuwa sheria, ni kuwa mfuko husika mfano NSSF, PPF au LAPF unalazimika kumlipa mwanachama wake asilimia kumi na nane na nusu (18.5%) ya mshahara wake wa mwisho kwa kipindi cha miezi sita.
Ikitokea mwanachama huyo hajapata ajira baada ya kipindi hicho cha miezi sita tangu kupoteza ajira, basi mwanachama huyo atalipwa asilimia kumi na sita na nusu (16.5%) ya salio lililobaki kutokana na malipo ya asilimia kumi na nane na nusu (18.5%) yaliyofanyika kwa miezi sita.
Mfano unalipwa mshahara wa Tsh. 300,000/- (laki tatu), basi hesabu yake ni asilimia kumi na nane na nusu (18.5%) ya Tsh. 300,000/- (laki tatu) kwa kila mwezi kwa miezi sita.
Na ikitokea kwa bahati mbaya mwanachama hakupata ajira baada ya miezi 6, basi mfuko unamlipa mwanachama huyo asilimia kumi na sita na nusu (16.5%) ya kiasi kilichobaki baada ya malipo ya asilimia kumi na nane na nusu (18.5%) yaliyofanyika kwa miezi sita.
Mfano salio lako ni Tsh. 2,000,000/- (milioni mbili) baada ya kulipwa asilimia kumi na nane na nusu (18.5%) kwa miezi sita, basi asilimia kumi na sita na nusu (16.5%) ya hiyo milioni mbili iliyobaki, ndiyo mwanachama atapewa na kiasi kitakachobaki kitakuwa granted kwa mwanachama pale atakapofikisha umri wa kustaafu kwa hiyari au lazima--miaka 55 ama--miaka 60; vinginevyo mwanachama aendeleze uanachama atakapopata ajira mpya au kujiajiri.
Kwa mujibu wa muswada huu, wale wanaoacha kazi wenyewe (resignation) watapewa asilimia kumi na nne tu (14%) ya michango yao kwa kipindi chote ambacho wamekuwa wakichangia mfuko; na kiasi kitakachobaki kitakuwa granted pale mwanachama atakapofikisha umri wa kustaafu.
Aidha, kwa wale ambao wamechangia mfuko chini ya miezi 18 (kumi na nane) ikitokea wamepoteza ajira kwa kufukuzwa au kupunguzwa kazini, wao watalipwa asilimia arobaini (40%) ya mafao yao na salio litakalobaki litatolewa kwa mwanachama pale atakapofikisha umri wa kustaafu aidha kwa lazima au kwa hiyari.
Muswada huu iwapo ukasainiwa na Rais na kuwa sheria, maana yake sheria hii mpya itakuwa imefuta sheria ya sasa ya mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo inamruhusu mtu kuchukua mafao yake pale anapopoteza ajira, licha ya kusemwa kuwa sheria hii ilishafutwa.
Kwa mujibu wa sheria ya hifadhi ya mifuko ya jamii ya mwaka 2002, kifungu na: 44 (1) imeainishwa kuwa, ikitokea mtu kapoteza ajira, basi michango yake yote pamoja na ile ambayo mwajiri alikuwa akichangia kwa mfuko kwa ajili ya mtu huyo, itatolewa kwa mtu huyo ambaye kapoteza ajira.
MKANGANYIKO:
Kabla ya muswada huu ambao umevuja, watu walipopoteza ajira na kuamua kufuatilia mafao yao, wamekuwa wakiambiwa kwamba…sheria ya fao la kujitoa imefutwa. Lakini wakati wakiambiwa hivyo, watu ambao wamekuwa wakipunguzwa makazini (redundancy) wao wamekuwa wakipewa mafao yao. Ila kwa wale waliopoteza ajira kwa misingi ya kufukuzwa na mwajiri, wamekuwa wakinyimwa mafao yao kwa sababu ambazo hazikuwa zikiwekwa wazi.
KIMAHESABAU:
Kutokana na ukokotoaji, hesabu zinaonesha kuwa; malipo ya miezi sita yatakayokuwa yakifanywa chini ya mpango huu, pamoja na malipo ya asilimia kumi na sita na nusu (16.5%) ni sawa na mshahara wa mtu kwa miezi miwili na nusu.
Suala la fao la kujitoa lilileta mtafaruku mwishoni mwa mwaka jana hali iliyopelekea shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini TUCTA chini ya katibu mkuu Nicolas Mgaya, kutamka wazi kuwa shirikisho hilo lingeitisha mgomo wa wafanyakazi nchi nzima, na kuiburuza serikali mahakamani iwapo ingefuta fao hilo la kujitoa ambalo limeonekana kuwa mkombozi kiuchumi kwa wafanyakazi kutokana na mazingira ya ajira nchini kutokuwa rafiki.
Hoja zilizotolewa na TUCTA kutaka fao la kujitoa lisifutwe zilizingatia mazingira ya ajira nchini kwamba, ajira hasa sekta binafsi si za uhakika, malipo kidogo ya mishahara kitu kinachopelekea watu washindwe kuweka akiba hivyo kulifuta fao hilo itakuwa ni kuumiza watu ambao fao la kujitoa hulitumia kujiendeleza kielimu, kujiajiri na hata kujikimu kimaisha.