SOCIOLOGISTTZ
JF-Expert Member
- Jun 16, 2013
- 2,615
- 927
Baada ya kutamba sana kwenye miziki ya bendi za dansi hapa nchini, Muumini mwijuma amehamia kwenye taarabu. Ikumbukwe kuwa Mwijuma muumini alianza kujulikana sana akiwa na Nchinga sound mpaka akajipachika jina la kocha wa dunia, baada ya hapo akachuliwa na bendi ya African Revolution iliyokuwa inatumia mtindo wa chumvi chumvi na akaubadilisha ukaitwa Tamtam. Tamtam ambayo ni kati ya bendi za kampuni ya ASET inayoongozwa na Asha Baraka ikavuma sana. Baadaye akaanzisha bendi yake mwenyewe aliyoiita Double M Sound. Akiwa Double M sound alisafiri na bend hadi tanga na alifanikiwa kuoa mwana dada anayeitwa Sadah Salehe. na alimtungia nyimbo wimbo....kuwa mtoto wa chumbageni ameumbika, (ikumbukwe kuwa alimuacha mke aliyepewa na baba yake kabla ya kumuoa Sada)
Vituko ndani ya ndoa vikaanza na Muumin Mwijuma akaanza kumuimba mke wake kuwa ni Call Box yaani kila anyetaka kupiga simu anapiga. wimbo huu uliwahuzunisha sana wanawake wakawa wamesusa kwenda kwenye maonyesho ya bend yake. Bend mwishowe ikafa.
Muumini kwa vile alivyokuwa anapenda kuimba mipasho kwenye bendi nadhani sasa ameenda mahali patakapomfaa, kwani anapenda sana mipasho na vijembe.
Vituko ndani ya ndoa vikaanza na Muumin Mwijuma akaanza kumuimba mke wake kuwa ni Call Box yaani kila anyetaka kupiga simu anapiga. wimbo huu uliwahuzunisha sana wanawake wakawa wamesusa kwenda kwenye maonyesho ya bend yake. Bend mwishowe ikafa.
Muumini kwa vile alivyokuwa anapenda kuimba mipasho kwenye bendi nadhani sasa ameenda mahali patakapomfaa, kwani anapenda sana mipasho na vijembe.