Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
Wanajamvi, mara nyingi tumeongelea muungano na madhaifu yanayotishia hatma yake
Kwa hali na mwelekeo uliopo ipo haja ya kuzungumzia tena na tena ili wakati ukifika tusijejiuliza maswali yenye majibu leo hii
Tatizo la muungano ni la muda mrefu likijitokeza kwa namna tofauti kila mara
Katika uhai wa muungano, nchi hii haijaongozwa na chama kingine zaid ya CCM
Ilitegemewa, kwa uzoefu mengi ya matatizo yangepatiwa ufumbuzi.
Kinyume chake udhaifu unatitia, ufa unapanuka na hatma yenye mashaka ni dhahiri
Serikali na chama tawala wanatafuta majibu , haionekani kama wamepata lolote
Kinachojitokeza ni majibu yanayokoleza hoja zinazodhoofisha muungano kila siku
Chama na serikali yake inaamini muungano ni 'mali yao' na wana haki ya kuulinda kwa nguvu na maguvu wakitumia mbinu zile zile zilizochoka na kuchokwa
Kwa dhana ya kulinda muungano kwa nguvu, kauli za kutisha zimekuwa utamaduni.
Mbinu za kuunda tume na kamati zinatumika kila mara ingawa yapata tume Zaidi ya 7 hazikutoa majibu na sasa ipo nyingine inayochochea udhaifu wa muungano
Yapo maswali wasiyojiuliza viongozi wa chama na serikali zake za awamu tano
1. Je, muungano ni mali ya CCM au ni mali ya wananchi?
2. Je, ipo ridhaa ya wananchi wa pande zote kuhusu muungano?
4.Je, muungano unalindwa na wananchi au maguvu kwa kutumia dola?
5. Kwanini kwa miaka 50 na utawala wa chama kile kile matatizo yanaendelea?
6.Ni wapi duniani muungano umehodhiwa na viongozi, umelindwa kwa nguvu?
Tutakuwa na mabandiko endelevu tukichagizwa na kile kilichoitwa 'kutatuliwa kwa kero za muungano kutoka kamati ya pande mbili za chama na serikali moja''
Kamati iliyotoa hoja zinazohitaji fikra na zinazoonyesha unyonge na udhaifu wa muungano
Sehemu ya I inafuata
Kwa hali na mwelekeo uliopo ipo haja ya kuzungumzia tena na tena ili wakati ukifika tusijejiuliza maswali yenye majibu leo hii
Tatizo la muungano ni la muda mrefu likijitokeza kwa namna tofauti kila mara
Katika uhai wa muungano, nchi hii haijaongozwa na chama kingine zaid ya CCM
Ilitegemewa, kwa uzoefu mengi ya matatizo yangepatiwa ufumbuzi.
Kinyume chake udhaifu unatitia, ufa unapanuka na hatma yenye mashaka ni dhahiri
Serikali na chama tawala wanatafuta majibu , haionekani kama wamepata lolote
Kinachojitokeza ni majibu yanayokoleza hoja zinazodhoofisha muungano kila siku
Chama na serikali yake inaamini muungano ni 'mali yao' na wana haki ya kuulinda kwa nguvu na maguvu wakitumia mbinu zile zile zilizochoka na kuchokwa
Kwa dhana ya kulinda muungano kwa nguvu, kauli za kutisha zimekuwa utamaduni.
Mbinu za kuunda tume na kamati zinatumika kila mara ingawa yapata tume Zaidi ya 7 hazikutoa majibu na sasa ipo nyingine inayochochea udhaifu wa muungano
Yapo maswali wasiyojiuliza viongozi wa chama na serikali zake za awamu tano
1. Je, muungano ni mali ya CCM au ni mali ya wananchi?
2. Je, ipo ridhaa ya wananchi wa pande zote kuhusu muungano?
4.Je, muungano unalindwa na wananchi au maguvu kwa kutumia dola?
5. Kwanini kwa miaka 50 na utawala wa chama kile kile matatizo yanaendelea?
6.Ni wapi duniani muungano umehodhiwa na viongozi, umelindwa kwa nguvu?
Tutakuwa na mabandiko endelevu tukichagizwa na kile kilichoitwa 'kutatuliwa kwa kero za muungano kutoka kamati ya pande mbili za chama na serikali moja''
Kamati iliyotoa hoja zinazohitaji fikra na zinazoonyesha unyonge na udhaifu wa muungano
Sehemu ya I inafuata