Muungano wa NASA hatarini kusambaratika kutokana na usaliti na uasi

Muungano wa NASA hatarini kusambaratika kutokana na usaliti na uasi

real G

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2013
Posts
5,227
Reaction score
5,299
Watu kutoka ndani wameliambia gazeti la Nation kwamba hatua ya watatu hao kutoshiriki tukio hilo, na ambalo Musyoka alielezea Jumanne, ilikuwa kuweka hai matumaini ya kuingia Ikulu mwaka 2022.

Kuhusu ikiwa alikuwa na wasiwasi kila chama kujipanga kwa uchaguzi wa mwaka 2022 kwa gharama ya umoja, Wetang'ula alisema: "Hapa niliposimama, na nilipoketi, sitaki kuvutwa na masuala kama hayo."

Naibu kiongozi wa chama cha Ford-Kenya Boni Khalwale, ambaye ni mwenyekiti mwenza wa kamati ya kuratibu shughuli za Nasa, alikuwa wazi zaidi, akichelea kidogo tu kusema umoja umekufa.

Shutuma za usaliti kwa kushindwa kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Raila Odinga na matamanio ya urais mwaka 2022 yanatishia kuvunja muungano wa upinzani wa National Super Alliance (Nasa) ikiwa ni mwaka mmoja tangu ulipoanzishwa.

Na hatua ya chama tawala cha Jubilee – kilichojiapiza kwamba Machi 2018 kiusambaratishe upinzani kwa kuwashawishi kujiunga au kutumia mbinu za gawa uwatawale – kumezidisha hali kuwa mbaya zaidi huku chama cha Odinga cha Orange Democratic Movement (ODM) kikilaumiwa kuwa ni mnufaika mkubwa katika nafasi za bungeni.

Viongozi wakuu Kalonzo Musyoka wa Wiper, Musalia Mudavadi wa ANC, na Moses Wetang'ula wa Ford-Kenya hawakuhudhuria tukio la Odinga kujiapisha kwenye viwanja wa Uhuru Park, kitendo kilichofunua mfululizo wa shutuma na mashambulizi yanayotishia kutoboa jahazi la upinzani.

Watu kutoka ndani wameliambia gazeti la Nation kwamba hatua ya watatu hao kutoshiriki tukio hilo, na ambalo Musyoka alielezea Jumanne, ilikuwa kuweka hai matumaini ya kuingia Ikulu mwaka 2022.

"Sitaki kulizungumzia suala hilo, hata kidogo, hata kidogo. Niacheni, "Wetang'ula aliiambia Nation alipoulizwa kuhusu hali ya muungano, jibu ambalo si la kawaida kwa mtu ambaye wiki moja iliyopita alikuwa akitoa majibu ya kujiamini juu ya umoja wa muungano.

Kuhusu ikiwa alikuwa na wasiwasi kila chama kujipanga kwa uchaguzi wa mwaka 2022 kwa gharama ya umoja, Wetang'ula alisema: "Hapa niliposimama, na nilipoketi, sitaki kuvutwa na masuala kama hayo."

Naibu kiongozi wa chama cha Ford-Kenya Boni Khalwale, ambaye ni mwenyekiti mwenza wa kamati ya kuratibu shughuli za Nasa, alikuwa wazi zaidi, akichelea kidogo tu kusema umoja umekufa.

"Sisi (Ford-Kenya) tumefungua milango kwa mazungumzo mapya na vyama vya siasa ndani ya Nasa na, popote pale fursa ikipatikana hata nje ya umoja huo," alisema Khalwale, seneta wa zamani wa Kakamega.

Bila kusema kuwa watatoka nje ya Nasa, Dk. Khalwale alisisitiza kuwa Ford-Kenya sasa inajihusisha na masuala ya kujiunda upya na kushinikiza mageuzi katika mfumo wa uchaguzi na mahakama ili kuhakikisha kuwa mbio za mwaka 2022 zinakuwa huru na haki.

Mwananchi
 
Wala si ajabu. Ndani ya NASA hamna demokrasia, atakachosema Supreme Leader, mzee RAO, basi hapo ndo wanakuwa tayari washapata sheria mpya!
 
Wala si ajabu. Ndani ya NASA hamna demokrasia, atakachosema Supreme Leader, mzee RAO, basi hapo ndo wanakuwa tayari washapata sheria mpya!

Kwanza kwenye chama chake cha ODM hakuna usawa wala democrasia, angalia Askari wa Raila wajukikanao kwa jina ‘men in Black’ yaani mgambo waliovalia suti nyeusi walivyovuruga mkutano ili Ababu Namwamba asichaguliwe kuwa katibu Mkuu wa chama chao kwa sababu tu hakutoka Nyanza na hasa siyo Mjaluo!!! Mdogo wangu Khalwale mwenyewe ODM ilimnyima nafasi ya Ugavana Kakamega maajabu naye bado anajitutumua kuunga mkono NASA/ODM!!!
 
Kwanza kwenye chama chake cha ODM hakuna usawa wala democrasia, angalia Askari wa Raila wajukikanao kwa jina ‘men in Black’ yaani mgambo waliovalia suti nyeusi walivyovuruga mkutano ili Ababu Namwamba asichaguliwe kuwa katibu Mkuu wa chama chao kwa sababu tu hakutoka Nyanza na hasa siyo Mjaluo!!! Mdogo wangu Khalwale mwenyewe ODM ilimnyima nafasi ya Ugavana Kakamega maajabu naye bado anajitutumua kuunga mkono NASA/ODM!!!
Ababu Namwamba na Boni Khalwale hawapo pekee yao, ongeza na jina la Issack Kariuki, na Magerer pia. Hawa wote ni wanasiasa ambao wamekuwa na nyathfa kuu kwenye miungano mbali mbali chini ya Raila. Ila wote waling'atuliwa ili nafasi za watu kutoka kanda la ziwa zipatikane!
 
Back
Top Bottom