Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,750
Unajua hapa tulipo kwa kweli Tanzania imechafuka ,japo hali haionekani kwa uwazi ,lakini tunaweza kusema kuna machafuko ndani ya Tanzania ,na machafuko haya sio hali ya Zanzibar ni nchi au si Nchi lakini ujumla serikali ya Mheshimiwa Kikwete ipo mashakani ,kuanzia T/bara hadi T/Visiwani ,tunasema nchi inayumba ,uchumi wa Nchi upo katika hali mbaya sana ,jambo ambalo limechangia kwa kiasi kikubwa manung'uniko kutoka kila pembe,ndani ya serikali viongozi hawaelewani ndani ya Chama Tawala hawaelewani wala hawajui wanafanya nini maana kila wanapoziba kunatoboka kwengine ,wapinzani nao wamekuta wananchi wana uelewa mdogo hawajui wawafahamishe vipi hadi wawashawishi kuwapa kura zao ,na hata wakiwapa kura bado vyombo vya dola vipo nyuma kulinda chama cha mafisadi inakuwa ni shagala bagala tupu,ni fujo tu.Ustadh Mwiba mata nyingi hupinga mawazo yako. Kumradhi yakhe (Ndo demokrasia). Lakini kwa haya mengine nakuunga mkono uelezayo ni sahihi. Hiyo kunyamaza na kupiga makofi tu japo yanaenda mrama imewakosesha mengi Wazanzibari. Endelea na msimamo wako Mwiba elezea uelezayo. Mwakyembe amefurunda -yeye.
Ukiangalia viongozi tulionao ndio hao kina Mwakiembe na Mwakipapai ,woga ,wanaogopa ,kuogopa kwao kunawafanya na wao wawatishe wengine.Kila siku tunasikia mawasilisho ya mawaziri yamejaa utata lakini kwa kuogopa na kukosa adabu ,wabunge wa kundi la akina mwakiyembe wameshindwa kusitisha hata bajeti moja na makelele yao unasikia bajeti ya waziri fulani imepitishwa,tutaogopana mpaka lini wakati nchi inazama na kuzamishwa kwa bajeti zilizojaa mizengwe ,si mmesikia viwanda viwili vimeuzwa kwa bei ya kiwanda kimoja : -
Alisema jambo ambalo limeishtua zaidi kambi hiyo, ni pale ilipobaini kuwa kulikuwa na viwanda viwili ndani ya kiwanda hicho ambavyo ni K1 chenye ukubwa wa hekta 6,214.5 na K2 ekari 3,153, lakini vyote vilihesabiwa kama kiwanda kimoja na kuuzwa kwa bei ya Sh16 bilioni.
"Kambi ya upinzani inaitaka serikali itoe majibu sahihi inakuaje viwanda viwili vyenye eneo la jumla ya ekta 9,367.5 viuzwe sawa na kiwanda kimoja cha Mtibwa?" alihoji Owenya na kusisitiza
Hapa si sehemu ya upinzani bali ni sehemu pia inayowahusu akina Mwakiyembe na Mwakipapai Je walisema kitu gani ? Au waliogopa kumukosea adabu Waziri husika na kuonekana hawana adabu ?
Akizungumzia Kiwanda cha Mgololo kilichobinafsishwa kwa Kampuni ya RAI Group Ltd ya Kenya mwaka 2004, Owenya alisema kauli ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko aliyoitoa bungeni mwishoni mwa wiki imezidi kuzua utata kwa kuwa mkataba wa mauziano una upungufu mkubwa ambao upinzani unahitaji ufafanuzi.
Alisema kuwa, upungufu huo ni pamoja na tofauti za bei ya mauzo katika mkataba huo ambazo zimeonyesha tofauti kubwa ya fedha kati ya bei ya mauziano ya awali na maelezo ya mkataba.
Mwakiembe na Mwakipapai hapa mnahusika au hamhusiki katika kuhoji au mpo hapo kulinda mafisadi tu ,kazi iliyopo hapa ndio inayokuhusu Mheshimiwa Mwakiembe uivalie njuga uwe tayari kumhoji waziri na serikali yake,na sio mambo ya Zanzibar hayo huyawezi labda kwa kutoa amri za fulani asulubiwe maana unajikomba kwa wakubwa ambao wao wenyewe wanakiri mambo ya Zanzibar ni mazito na sio mchezo hata mtoto mdogo akikwambia Zanzibar ni Nchi basi bora unyamaze la si hivyo atakuumbua na utake kumuadhibu.