FairPlayer
JF-Expert Member
- Feb 27, 2006
- 4,145
- 723
Mwenyekiti wa baraza la mawaziri ni Rais wa jamhuri wa muungano wa Tanzania.
Kumbe Karume ni waziri wa Tanzania Zanzibar?
Weee acha choko choko...
Rais wa Zanzibar ni Mjumbe wa Baraza la Mawaziri, kama ilivyo mwanasheria mkuu nadhani pia ni mjumbe.
Wildcat nategemea ni mkubwa wa umri wa kukumbuka jinsi Benjamin William Mkapa alivyoupata Urais1995. Kama hukumbuki aliupata kwa nguvu za Wazanzibari chini ya DR Salmini. Kwa hivyo unchi kama tutaupima kwa namna kiongozi fulani alipatikana vipi sijui itakuwa tafsiri gani kwa Tanzania wakati wa Mkapa. Bado sijaona hoja za kuifanya Zanzibar sio NCHI.
5) Without prejudice to the application of the Constitution
of Zanzibar in accordance with this Constitution concerning all
matters pertaining to Tanzania Zanzibar which are not Union
Matters, this Constitution shall have the force of law in the whole
of the Republic, and in the event any other law conflicts with the
provisions contained in this Constitution, the Constitution shall
prevail and that other law, to the extent of the inconsistency with
the Constitution, shall be void.
Mwenyekiti wa baraza la mawaziri ni Rais wa jamhuri wa muungano wa Tanzania.
Hawa jamaa wanatangaza secession na Rais wa Muungano anabaki kucheka cheka tu!!
The Prez needs to do something........
Tunaenda kubaya. Hawa jamaa akili yao sio nzuri naona. Dr Mwakyembe ni mwanasheria hawezi kukurupuka. By the way hata tukiwapoteza hawana cha maana! Wamezoea kutawaliwa hawa!
Kumkatalia Pinda kuwa hana mamlaka nao ni kichekesho!. Bunge la Muungano na la wawakilishi lipi lipo juu?
Ni kutoelewa sijui?
Mimi nimestushwa... na the so called defence system! kama ilivyo quoted kwenye original post!
Hilo ni neno zito sana na jipya kulisikia kwenye sakata hili,,, ambalo waandishi wa habari wana haja/wajibu wa kuhitaji clarification zaidi kutoka kwa msemaji huyo.
Kumbukeni... Jeshi la Poli ni (Usalama wa Raia) ni tofauti na TPDF (Tanzania Peoples Defence force)!
Mtu anaposema kuna version ya TPDF kule Zanzibar lazima aulizwe vizuri...
Hili la bendera sina shida nalo... hata Jiji la Dar es Salaam... na halmashauri zote zina bendera zao... alafu pia shule zina nyimbo zao za shule mfano Ilboru Sekondari niliwahi kuambiwa wa wimbo wa shule... no issue on this!
(1) Jamaa anayedai kuwa waziri wa serikali ya mapinduzi hawajibniki kwa waziri mkuu wa Tanzania ni mpuuzi kabisa. Huyu hafai hata kuwa kiongozi kwa vile hajui itifaki. Hivi hajui kuwa mkulima wa kijijini pamoja na kutokuwah mtumishi wa serikali, lazima anawaheshimu mawaziri wote wa muungano na wale wa serikali ya mapinduzi? Kama zanzibar ni sovereign state, kwa nini basi raisi wake Karume awe ni sehemu ya baraza la mawaziri wa Serikali ya jamhuri ya Muungano, tena akiwa chini ya waziri mkuu? Itifaki kwenye cabinet ni Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu halafu Raisi wa Zanzibar, mawaziri wote, mwanasheria mkuu
(2) Mtu wa kuadhibiwa hapa siyo yule anayedai kuwa Zanzibar ni sovereign state, bali maraisi wote wawili: Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Raisi wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kushindwa kulinda na kutetea katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama walivyoapa wakati wanachukua madaraka waliyo nayo.
KMKM ni Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo.
Sio jeshi la ulinzi. ila nawalaumu waandishi wetu ambao hawakuhoji huo ulinzi. jamaa wa Zenji kwa mara nyingine wanaanika ujinga wao. Samahani Dr Who aka game theory.
Zenji to me ni mkoa tu tena wenye watu wasiojilewa na wasio elewa muungano ni nini.
Nini maana ya mfumo wa ulinzi na umesahau jeshi la kujenga Taifa na hata amri ya Abbass Kandoro ya Mgambo. Ama kweli kama Wazanzibar wajinga basi kuna mliowazidi kwani unakurpuka kumwambia mwenzio yuko uchi kwa kuvaa msuli wewe umevaa chupi hadharani.
Mkjj
Naungana na wewe, hata nyumbani baba akiwa ana cheka cheka sana na watoto wanapunguza heshima na hata kuaibisha mbele ya wageni. Rais wetu amekuwa soft sana, wanajua hilo kwani enzi za BWM hawa jamaa walikuwa na heshima na serikali ya Muungano.
JK anatakiwa achukue hatua na aanze na wote wenye tuhuma za ufisadi kama kina Lowassa, RA, Chenge n.k. Akishawashughulikia hawa jamaa watamuheshimu kama Rais wa Tanzania, kwani kachaguliwa na watanzania wote Bara na visiwani.
Hawa wazenji wanajaribu kuchokonoa nyuki kwenye mzinga. na kwa kuwa sasa hivi Nyuki hawaumi? wanaanza kuwatia mifukoni na makwapani. Uoga wa kina JK Muungano kuwafia mikononi mwao ndio unawapa kibri SMZ. Mbona Nyerere aliwawajibisha akina AJ na SSH?.
Lakini pia ukiangalia upande wa pili wa sarafu inawezekana hawa Jamaa CCM, wapo kwenye strategy ya kuwasahaulisha wadanganyika mjadala juu ya UFISADI unaofanywa na CCM na kushinikiza hatua kuchukuliwa kwa wale wote walioshiriki. "Strategic distortion of Gland Corruption Forums towards 2010".