katika katiba hakuna kitu tanzania bara, hivyo fedha yote inayoingia kwa jina la jamhuri ya tanzanzia ni haki ya zanzibar na tanganyika ,tena nusu kwa nusu, tanzania inapopokea msaada wowote ule katika wizara zake ,misaada hiyo huletwa kwa jina la tanzania , hivyo misaada hiyo mnaipeleka tanzania bara au mnadai eti ni ya tanzania bara jamani hii tanzania bara imetokea wapi ? Mbona haikuainishwa katika katiba ,nasema mnatuzulumu tena kwa kila kitu ,sioni aibu kusema mnatudhulumu kwa sababu naitetea nchi yangu zanzibar ,mnachukua kila kitu na kukifanya cha tanzania bara .
Jamani katika katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania kuna serikali mbili tu ,serikali ya muungano na serikali ya zanzibar ,hivyo kila kitu kinachomilikiwa na serikali ya muungano .zanzibar itakuwa na haki nayo au nacho lakini kila kinachomilikiwa na serikali ya zanzibar serikali ya muungano haina haki nacho au nayo, ,hivyo misaada yote inayopokea serikali ya muungano mkae mkijua kuwa zanzibar ina haki yake na kama mnatuitumia bila ya kuwapa haki yao mjue mnakula na kulisha watoto wenu dhulma tu,hilo mlijue kuwa mnaishi kwa vitu vya kudhulumu ndio maana ufisadi ukawa haumaliziki tena mkubwa wa kutisha kwa sababu serikali ya muungano imejaa mali ya dhulma kila mmoja anachota atakavyo.
Tunapokubaliana hili ni la muungano basi liwe la muungano kweli na sio kubania na kutufanya hatuna akili ya kufahamu ,hivyo waziri wa kilimo wa tanzania anawajibika kwa serikali zote mbili ya zanzibar na ya tanganyika(ambayo haipo) na ndio hivyo hivyo kwa mawaziri wote hivyo waziri huyu anapokwenda kutafuta na kusaka misaada akipewa inasemwa kuwa imepewa tanzania lakini akirudi hapa na kitita cha misaada zanzibar hawaoni kitu ,hali hii inakuwaje kuwaje ,hivi hapa hamuoni kama muungano una matatizo ?