MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 843
This is from Mwananchi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Muungano waibua malumbano makali katika televisheni ya taifaNa Salim Said
MVUTANO mkali umeibuka miongoni mwa wasomi, wanasiasa na serikali katika mjadala kuhusu kero za Muungano uliofanyika jijini Dar es Salaam juzi.
Katika mjadala huo, baadhi ya washiriki walikua wakinyoosheana vidole na kutuhumiana kuwa, ndio wanaosababisha kukua na usugu wa kero za Muungano wa Tangayika na Zanzibar.
Mjadala huo ambao ulirushwa na Kituo cha Televesheni TBC1 uliwashirikisha baadhi ya wasomi, viongozi wa serikali na wanasiasa..
Waziri wa Nchi katika ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Muhmmad Seif Khatib alisema muungano umeimarika na kwamba ndoto za waasisi wake, ambao ni mwalimu Julius Nyerere na hayati Abeid Aman Karume zimetimia.
Kauli hiyo pia, iliungwa mkono na Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Azaveli Lwaitama ambaye alisema muungano umeimarika na kwamba, falsafa ya waasisi imetimia.
Hata ukimuuliza ndugu yangu Duni hapo, atakwambia yeye ni Mtanzania, kero zinakuzwa na wanasiasa ambao hawajaelewa, yaliyokuwamo katika vichwa vya waasisi wa muungano huu alisema Dk Lwaitama
Kauli hizo zilionyesha kumkera Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Juma Duni Haji ambaye katika kujibu hoja hiyo alisema, kama kuimarika kwa muungano ni kuwepo kwa kero nyingi na matatizo, basi umeimarika lakini kama ni utatuzi wa matatizo na kero hizo, basi bado haujaimarika.
Katika mambo ambayo siyapendi na yananikera sana ni kuufananisha muungano huu kuwa ni wa mke na mume au mkubwa na mdogo. Huu ni muungano wa nchi mbili. Mimi nikiwa Katibu wa Wizara ya Fedha tuliisaidia serikali ya muungano dola 15 milioni za Marekani kulipa deni la Benki ya Dunia, alisisitiza Duni.
Jambo hilo, lilimfanya muongoza mjadala huo ambaye ni mtangazaji wa TBC1, kumuomba radhi mwanasiasa huyo na kuruhusu mjadala huo kuendelea.
Duni aliendelea kutoa mifano ya kutoimarika kwa muungano huo kuwa, ni pamoja na kufukuzwa katika chama, kwa Rais mstaafu, Aboud Jumbe na maalim Seif Sharif Hamad, ambaye alikuwa waziri kiongozi wa kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kutoka na kesi za muungano.
Muungano lazima ulete faida kwa wananchi kisiasa, kiusalama na kiuchumi lakini Wazanzibari wanahoji kuhusu fedha za misaada na mikopo zinazoingia nchini kwa jina la Tanzania, kwa nini hawapati, alihoji Duni
Alisema, jambo muhimu ni kushughulikia kero za muungano na si kuwa, mtu akisema aitwe katika vikao vya kamati kuu ya chama na kunyamazishwa au kuadhibiwa.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari, Kusini mwa Afrika tawi la Tanzania (Misa- Tan), Ayoub Rioba alisema, kama kuna mawasiliano yanayoeleweka, baina ya viongozi na wananchi, matatizo ya kero za muungano yatamalizika.
Kama tutakuwa na mawasiliano imara baina ya pande mbili hizi, tatizo ni dogo sana lakini pia tuthamini michango ya mijadala kama hii, kwa kuwa bado sisi tunayo fursa ya kujadiliana, wenzetu wanatafuta lakini hawapati fursa ya kujadiliana alisena Rioba.
Katika hilo, Dk Lwaitama alisistiza kuwa, dhamira ya waasisi ilikuwa ni umoja na mshikamano wa Watanzania na Waafrika lakini matatizo na kero ni jambo la kawaida.
Kwa upande wake waziri Khatibu alisisitiza kuwa, uhuru, usalama, amani na uchumi wa Zanzibar unategemea serikali ya muungano iliyopatikana baada ya kuungana kwa Zanzibar na Tanganyika mwaka 1964. Muungano ni wa binadamu wala si wa malaika, matatizo hayaepukiki lakini tunafanya jitihada mbalimbali za kutatua kero na matatizo hayo alisema Khatib.
Bara tunaungangania na kuendelea kuwagharamia Zanzibar kwa kuwapangia watawala, na kuwapa income support
Zanzibar washatuchoka kwenye hii ndoa of convenience wanaona wao watakuwa bora kuwa kivyao
lakini cha ajabu mikataba ya huu muungano imekuwa siri ya Taifa, watawala wa bara hawapendi kudadisiwa juu yake
na mbaya zaidi after 40 YEARS nadhani its about time tukauvunja kwani HAUKUWEPO, UKAWEPO na UNAWEZA USIWEPO TENA ni contract ambayo inaweza kuvunjwa kama haina faida kwa pande zote mbili
GT hao wazanzibari unaosema hawautaki muungano ni wazanzibari gani? Maana yake kuna wazanzibari wenye asili ya kiarabu ambao wengi wao ni CUF hawa ni surrogates wa waarabu walioondolewa kwa mapinduzi mwaka 1964; sasa hawa kwa vyovyote vile hawawezi kuupenda muungano na wanatumiwa na jamaa zao waliokonje wafanye chokochoko ili waweze kurudisha utawala wao!!!!. Wale ambao walikuwa wanateswa enzi za Jamshid sidhani kama wangependa muungano uvunjike kwani kwa kufanya hivyo watakuwawanarudi kule walikokuwa wanadhalilishwsa utu wao. Sasa kati ya hawa GT ni wakinanani waliokuambia hawataki muungano na wako wangapi?
Hayo ya betrii yatatufikia baada ya miaka mia,ila habari ndio hiyo ipo ndani ya kasha la habari muhimu huko UN ni muda tu ndio utakao amua wakati wahusika wameshaamua, tuliwaambia hata kikiwa kinibu basi kitatutosheleza.Boiler linachemsha kweli. Ni wewe Mwiba?
Sasa Watumwa wetu mwatupa kilichochetu? Mhhh, hii kali.
Nafikiri tatizo liko kwingine. Au ndiyo mchecheto wa mafuta huo? Wenzio Wafaransa, USA, German nk wako Bolivia ili kufanya utafiti wa magari yanatumia betri ili kuachana na mafuta na nyie ndiyo mnaamka na mafuta? Mambo sasa hivi ni Bolivia ndugu yangu kwa Moralez na si kwa Chavez tena.
Hayo ya betrii yatatufikia baada ya miaka mia,ila habari ndio hiyo ipo ndani ya kasha la habari muhimu huko UN ni muda tu ndio utakao amua wakati wahusika wameshaamua, tuliwaambia hata kikiwa kinibu basi kitatutosheleza.
Kutoka mitandaoni
MGOGORO WA KISIASA WA ZANZIBAR
Tarehe 12.01.1964 Chama cha ASP kiliipindua Serikali ya ZNP na ZPPP
26.04.1964 Chama cha TANU kiliipindua Serikali ya ASP Zanzibar
26.04.1964 Serkali ya Tanganyika iliipindua na kuiondoa Nchi ya Zanzibar
ZANZIBAR INATANGAZA KWAMBA KITAIFA NA KIMATAIFA :
ZANZIBAR NI DOLA, TAIFA NA NCHI HURU SAWA NA NCHI YA TANGANYIKA
Rais wa Zanzibar Sh. Amani Abeid Karume ni Rais Sawa na Rais wa Tanganyika Sh. Jakaya Mrisho Kikwete
Waziri Kiongozi wa Zanzibar Sh. Vuai Nahodha ni sawa na Waziri Mkuu wa Tanganyika Sh. Mizegwe Pinda
Serikali ya Zanzibar ina hadhi sawa na serikali ya Tanganyika ijulikanayo kama Serikali ya Muungano
Baraza la Mawaziri la Serikali ya Zanzibar ni sawa na Baraza la Mawaziri la Serikali ya Tanganyika liulikano kama Baraza la Mawaziri la Serikali ya Muungano
Baraza la Wawakailishi la Zanzibar ni sawa na Bunge la Tanganyika lijulikano kama ni Bunge la Muungano
Wawakilishi wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar ni sawa na Wabunge wa Bunge la Tanganyika wajulikanao kama Wabunge wa Muungano
Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar ni sawa na Spika wa Bunge la Tanganyika
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar ni sawa na Mwanasheria Mkuu wa Tanganyika
Mahakama Kuu ya Zanzibar ni sawa na Makahama Kuu ya Tanganyika
Baraza la Wawakilishi libadilishe Katiba ya Zanzibar na iwe na nguvu sawa na Katiba ya Tanganyika (Muungano)
Serikali ya Zanzibar na BLW wapeleke maombi kwenye Umoja wa Mataifa kukidai Kiti cha Zanzibar katika Umoja wa Mataifa
Zanzibar ijiunge na Mashirika ya Kimataifa kwa maslahi ya Zanzibar
Zanzibar iwe na vyama vyake vya Kisiasa vyenye sifa huru za kitaifa na kimataifa
Serikali ya Zanzibar na Baraza la Wawakilishi wapitishe sheria ya kulinda mali asili yote ya Zanzibar yakiwemo na Mafuta ya Zanzibar yawe chini ya Zanzibar
Serikali na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar waitishe Kura ya Maoni ya Wazanzibari kuwapa Wazanzibari fursa ya kuyakubali au kuyakataa Mapendekezo ya hapo Juu.
porojo tu
hizi hadithi za ndoto. serikali iliyokuwa huru ni ile iliyopinduliwa.
na walioipindua ni akina nyerere na watumwa walio zanzibar na walioletwa kutoka bara kwa mapinduzi.
baada ya hapo kuwekwa asp chama kilichoounganisha
wauaji
watumwa
na wanafiki wachache.
bada ya hapo kwa vile karume alikamatiwa malawi akawa kampambe kuegemea kwa wanafiki kuwadharau wauaji
ndipo wauaji walivyofanya tena mapinduzi kushirikiana na nyerere tena na nyerere kumueka ndugu yake jumbe
ndipo sasa ilipokuja ``mapinduzi daima``
hii ndio maana ya chama cha mapinduzi kilicho sasa tanzania
jina hili (mapinduzi) halikutokana juu ya kuungana vyama vi2 bali ni ukweli watanganyika ndio waliofanya mapinduzi na haya mapinduzi yapo daima.
ndio ukaona zanzibar kila uchaguzi watanganyika wanapelekwa kule pamoja na majeshi.
zanzibar bila ya kuwaandosha wauaji wakarudi kwa bara pamoja na wakuja waliokuja kujaza nchi na makafiri waliokuja kujaza ukafiri basi zanzibar haijawa salama.
visiwa vidogo ambavyo nafasi yake inawatosheleza wazanzibar tu leo imejaa watu kutoka bara. hawa watu wanaishi kama nzi bila ya sheria ila tu ni kujaza kura kwa ccm haya pia ni mapinduzi.
ndio wakatwambia wabara kuwa mapinduzi daima kwa wazanzibar.
kuna wazanzibar na wazanzibara
Mwiba kila siku Zanzibar ijitoe, Zanzibar, Zanzibar. Lakini huishi kuijiingiza kwenye mijadala ya jeshi letu, EPA, Benki zetu, DPP wetu, Pinda, Kikwete, everything Tanganyika umo. Why care? Jamvi la Kitanganyika, umo.
Sitaki nataka type.